Historia ya Sarafu Yetu Tanzania

aiseee ngoja nikimbile Bank nikazichange zile gunia mbili za shilingi tano zangu maana niliziacha kama ukumbusho kumbe PESA IPO ndani Na mm nalia njaa
 
Shukrani sana Kichuguu kwa historia nzuri sana.
Umenifumbua macho na kuona mengi niliyokuwa siyajui hasa kwa sarafu za nchi yetu na Afrika Mashariki kwa ujumla.
Pia nimejua chanzo cha neno Dala dala.

Big up mkuu.

 
  1. Nimekuwa natafiti pole pole kutafuta picha za pesa tulizowahi kutumia hapa kwetu, nikaona nizitundike hapa kukumbushana tulikotoka. Kuna sarafu ambazo nimeshindwa kupata picha zake, lakini hata hivyo nadhani nimefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 90 kukusanya ukweli kuhusu sarafu yetu. Najua kuwa hadithi hii ni ndefu sana, hata hivyo kama unataka kujua historia ya sarafu yetu jipe dakika kumi hivi kuisoma yote hapa; ni burudani ya aina yake.


    Kabla ya mwaka 1884, nchi yetu ilikuwa inatumia sarafu moja ya Riyal iliyokuwa imetolewa na Sultan wa Zanzibar chini ya Sultani wa Oman. Sarafu za Riyal zilikuwa kama ifuatavyo

    Riyal
    ryal1.jpg


    riyal2.jpg


    riyal3.jpg

    Baada ya 1884, Zanzibar ilitumia sarafu za aina tatu kwa mpigo. Sarafu ya kwanza ilijulikana kama Maria Theresa Thaler iliyotolewa Italy, ilikuwa na sura ifuatayo.

    Maria Theresa Saler

    mariatheresa-thaler.jpg

    Sarafu ya pili ilikuwa ni rupia ya kihindi pamoja na visehemu vyake ambavyo vilikuwa vingi kidogo. Sehemu kubwa za rupia zilikuwa ni Anna, pice , robo rupia na nusu rupia:

    1 Anna
    anna.jpg


    1/4 rupee

    quarter_rpee.jpg


    1/2 rupee
    half_rupee.jpg

    1 rupee

    1rupee.jpg


    Pesa hizi zilikuwa ngumu sana hasa kwa vile Anna ilikuwa na vipande vingine kama 1/12 ya Anna, 1/6 ya Anna, 1/4 ya Anna na kadhalika. Sikuweka picha za vipande hivi ingawa ninavyo.

    Sarafu ya tatu ilikuwa inajulikana kama Zanzibari Rupee ambao kimsingi ilikuwa sawa na rupee ya kiingereza iliyokuwa ikutumika Kenya na Uganda. Sikupata picha yake.

  2. senti 20
    senti201966-1988.jpg


    senti 50
    senti501966-1988.jpg


    Shilingi 1
    shilingi11966-1988.jpg


    Sarafu hizi zinaendelea kutumika hadi leo ingawa thamani ya shilingi imeshuka kiasi kuwa zinaonekana hazina thamani yoyote. Ilipofika mwaka 1971 wakati wa sherehe za miaka kumi ya uhuru, sarafu mpya ya shilingi tano iliyokuwa na pembe kumi na mbili ilitolewa. Wakati huo exchange rate ya dola kwa shilingi ilikuwa ni shilingi tano kwa dola moja ya kimarekani. Kwa hiyo sarafu hii ya shilingi tano ilijuikana pia kama "dola" au "DALA" ingawa kwenye mikoa ya ziwa ilijulikana zaidi kama "Scania." Nadhani mnakumbukua chanzo cha neno "dala dala" ni kutokana na nauli ya mabasi hayo wakati huo kuwa shilingi tano. Sarafu hii ya miaka kumi ya uhuru haikudumu sana na mwaka 1972 ikabadilishwa sura na kuwa na pembe kumi kama ifuatavyo.

    Shilingi 5
    shilingi51972-1988.jpg


    Kuna taarifa kuwa mwaka 1974 sarafu mpya za shilingi 25 na shilingi 1000 zilitolewa ingawa benki kuu haikutunza picha zake. Ingawa sikuweza kupata sura ya sarafu ya shillingi 1000, nimefanikiwa kupata picha ya sarafu ya shillingi 25 ambayo ilikuwa na sura ifuatayo:

    shilingi 25
    1974tanzania25shillingsworldwildlifefundobv240.jpg


    Mara baada ya kuzaliwa kwa CCM mwaka 1977, thamani ya pesa ilianza kupunguka pole pole kiasi kuwa kulikuwa na haja ya kuwa na sarafu kati ya senti ishirini na senti tano. Hivyo sarafu ya senti kumi iliingizwa kwenye mzunguko; sarafu hii ilikuwa kama ifuatavyo.

    senti 10
    senti101977-1984.jpg


    Kufuatia mkutano wa FAO uliofanyika Arusha mwezi September mwaka 1978, sarafu chache za shillingi 5 zilitolewa kukumbukia mkutano huo; sarafu hizo zikuwa na sura ifuatayo

    Shillingi 5
    tan-p2b.jpg


    Baada ya hapo, hakukuwa na sarafu mpya hadi mwaka 1982 wakati wa sherehe za miaka 20ya uhuru ambapo sarafu mpya ya shillingi 20 ilitolewa ikiwa na sura ifuatayo.
.................Inaendelea.
 
  1. Shillingi 20.
    tan-p2c.jpg


    Hiyo ndiyo iliyokuwa sarafu ya mwisho kutolewa wakati wa utawala wa Nyerere. Rais Mwinyi alipochukua madaraka mwaka 1985, aliendelea na sarafu zenye picha ya Nyerere hadi mwaka 1986 zilipotolewa sarafu zenye picha ya Mwinyi. Sarafu za senti tano,
    kumi, na ishirini hazikutolewa tena. Sarafu zilizotolewa wakati huo zilikuwa za senti 50, Shilingi 1, shilingi tano na shilingi kumi ambayo ilikuwa na sura ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Sarafu hizo ni hizi hapa:


    senti hamsini

    senti50_1987.jpg


    Shilingi moja

    shilling1_1987.jpg


    Shilingi tano
    shillingi5_1987.jpg


    Shilingi 10
    shillingi10_1987.jpg



    Kadri thamani ya shilingi ilivyoendelea kudorora, ilibdi kutengeneza sarafu nyingine ambapo sarafu ya shilingi 20 ilitolewa mwaka 1990 ikiwa na sura ya Mwinyi kama ifuatavyo.

    Shilingi 20

    shillingi20_1990.jpg


    Mwaka huo huo sarafu nyingine ya shilingi 5 ilitolewa kwa kumbukumbu ya jengo jipya la benki kuu. Kwa bahati mbaya sikufanikiwa kupata picha yake. Mwishoni mwa utawala wa mwinyi, thamani ya shilingi ilikuwa chini kiasi kuwa sarafu ya Baba wa Taifa yenye thamani ya shilingu kumi ilikuwa inakimbilia kuishiwa nguvu yake. Hivyo sarafu mpya yenye sura wa baba wa taifa ikatengezwa ikiwa na thamani ya shillingi 100.

    Shilingi 100
    shillingi100_1994.jpg


    Rais Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995, akapiga marufuku matumizi ya sura za raisi aliyeko madarakani kwenye sarafu: alipendelea sura za waasisi wa taifa tu na picha alama za asili za nchi ndizo zitumike. Hata hivyo hakutaka kuondoa kabisa sura ya rais Mwinyi kwenye sarafu, hivyo ikatengezwa sarafu mpya ya shilingi 50 iliyokuwa na sura ya Mwinyi kama ionekanavyo hapo chini iliyotolewa mwaka 1996.

    Shilingi 50
    shilling50_1996.jpg


    Wakati huo huo sarafu tatu zilitolewa kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 35 ya uhuru pamoja ni michezo ya 26 ya olimpiki iliyofanyika Atlanta Marekani mwaka huo. Sarafu hizi zilionyesha wachezaji wa kutupa tufe, riadha, na karate kama ifuatavyo.

    tufe
    olympic_11996.jpg


    riadha
    olympic_31996.jpg



    karate
    olympic_21996.jpg


    Mwaka 1997 kulitolewa sarafu mbili mpya: moja ilikuwa na thamani ya shillingi 500 ikiwa inakumbukia miaka 75 tangu malkia Elizabeth mama wa malkia Elizabeth II alipotembelea nchi yetu mwaka 1923. Sarafu ya pili ilikuwa na thamani ya shillingi 200 ikiwa inatukuza mbuga za wanyama pori wa Afrika. Sarafu hizo zilikuwa na sura zifuatazo

    Shilingi 200

    wildlife1998.jpg



    Shilingi 500
    queenmother_1997.jpg


    Mwaka 1998, ilitolewa sarafu nyingine ya kudumu ya shilingi 200 kuchukua nafasi ya sarafu zote za kumbukumbu zilizokuwa na thamani hiyo. Sarafu hiyo ilikuwa na picha Karume na inaonekana kama ifuatavyo:

    Shilingi 200
    tan-p3a.jpg


    Mwaka huo huo, ilitolewa sarafu nyingine ya thamani ya shilingi mia tano kutukuza mbuga za Serengeti. Sarafu hiyo ilikuwa na sura ifuatayo.

    Shilingi 500
    seremgeti_1998.jpg



    ........................Inaendelea

  2. Kuanzia mwaka 1998, sarafu yetu ilikuwa imara tena na haijatolewa sarafu nyingine mpya kwa karibu miaka tisa sasa. Mpaka sasa sarafu kubwa zinazotumika ni zile za shillingi 50, 100 na 200 zionekazo hapa chini:

    Shilingi 50
    shilling50_1996.jpg


    Shilingi 100
    shillingi100_1994.jpg


    Shilingi 200
    tan-p3a.jpg


    Hata hivyo, sarafu zote zilizowahi kutolewa na benki kuu ya Tanzania bado ni halali ingawa ama hazipatikani tena kwenye mzunguko au zimashekuwa na thamani ndogo kiasi kuwa zinahitajika nyingi sana ili kufanya manunuzi ya aina yoyote. Katika historia ya benki kuu, hakuna sarafu yake iliyowahi kufutwa.

    Usisahau kusoma Historia ya Noti na Sarafu za Tanzania
 
  1. Nimekuwa natafiti pole pole kutafuta picha za pesa tulizowahi kutumia hapa kwetu, nikaona nizitundike hapa kukumbushana tulikotoka. Kuna sarafu ambazo nimeshindwa kupata picha zake, lakini hata hivyo nadhani nimefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 90 kukusanya ukweli kuhusu sarafu yetu. Najua kuwa hadithi hii ni ndefu sana, hata hivyo kama unataka kujua historia ya sarafu yetu jipe dakika kumi hivi kuisoma yote hapa; ni burudani ya aina yake.


    Kabla ya mwaka 1884, nchi yetu ilikuwa inatumia sarafu moja ya Riyal iliyokuwa imetolewa na Sultan wa Zanzibar chini ya Sultani wa Oman. Sarafu za Riyal zilikuwa kama ifuatavyo

    Riyal
    ryal1.jpg


    riyal2.jpg


    riyal3.jpg

    Baada ya 1884, Zanzibar ilitumia sarafu za aina tatu kwa mpigo. Sarafu ya kwanza ilijulikana kama Maria Theresa Thaler iliyotolewa Italy, ilikuwa na sura ifuatayo.

    Maria Theresa Saler

    mariatheresa-thaler.jpg

    Sarafu ya pili ilikuwa ni rupia ya kihindi pamoja na visehemu vyake ambavyo vilikuwa vingi kidogo. Sehemu kubwa za rupia zilikuwa ni Anna, pice , robo rupia na nusu rupia:

    1 Anna
    anna.jpg


    1/4 rupee

    quarter_rpee.jpg


    1/2 rupee
    half_rupee.jpg

    1 rupee

    1rupee.jpg


    Pesa hizi zilikuwa ngumu sana hasa kwa vile Anna ilikuwa na vipande vingine kama 1/12 ya Anna, 1/6 ya Anna, 1/4 ya Anna na kadhalika. Sikuweka picha za vipande hivi ingawa ninavyo.

    Sarafu ya tatu ilikuwa inajulikana kama Zanzibari Rupee ambao kimsingi ilikuwa sawa na rupee ya kiingereza iliyokuwa ikutumika Kenya na Uganda. Sikupata picha yake.

  2. senti 20
    senti201966-1988.jpg


    senti 50
    senti501966-1988.jpg


    Shilingi 1
    shilingi11966-1988.jpg


    Sarafu hizi zinaendelea kutumika hadi leo ingawa thamani ya shilingi imeshuka kiasi kuwa zinaonekana hazina thamani yoyote. Ilipofika mwaka 1971 wakati wa sherehe za miaka kumi ya uhuru, sarafu mpya ya shilingi tano iliyokuwa na pembe kumi na mbili ilitolewa. Wakati huo exchange rate ya dola kwa shilingi ilikuwa ni shilingi tano kwa dola moja ya kimarekani. Kwa hiyo sarafu hii ya shilingi tano ilijuikana pia kama "dola" au "DALA" ingawa kwenye mikoa ya ziwa ilijulikana zaidi kama "Scania." Nadhani mnakumbukua chanzo cha neno "dala dala" ni kutokana na nauli ya mabasi hayo wakati huo kuwa shilingi tano. Sarafu hii ya miaka kumi ya uhuru haikudumu sana na mwaka 1972 ikabadilishwa sura na kuwa na pembe kumi kama ifuatavyo.

    Shilingi 5
    shilingi51972-1988.jpg


    Kuna taarifa kuwa mwaka 1974 sarafu mpya za shilingi 25 na shilingi 1000 zilitolewa ingawa benki kuu haikutunza picha zake. Ingawa sikuweza kupata sura ya sarafu ya shillingi 1000, nimefanikiwa kupata picha ya sarafu ya shillingi 25 ambayo ilikuwa na sura ifuatayo:

    shilingi 25
    1974tanzania25shillingsworldwildlifefundobv240.jpg


    Mara baada ya kuzaliwa kwa CCM mwaka 1977, thamani ya pesa ilianza kupunguka pole pole kiasi kuwa kulikuwa na haja ya kuwa na sarafu kati ya senti ishirini na senti tano. Hivyo sarafu ya senti kumi iliingizwa kwenye mzunguko; sarafu hii ilikuwa kama ifuatavyo.

    senti 10
    senti101977-1984.jpg


    Kufuatia mkutano wa FAO uliofanyika Arusha mwezi September mwaka 1978, sarafu chache za shillingi 5 zilitolewa kukumbukia mkutano huo; sarafu hizo zikuwa na sura ifuatayo

    Shillingi 5
    tan-p2b.jpg


    Baada ya hapo, hakukuwa na sarafu mpya hadi mwaka 1982 wakati wa sherehe za miaka 20ya uhuru ambapo sarafu mpya ya shillingi 20 ilitolewa ikiwa na sura ifuatayo.
.................Inaendelea.
Kumbe hata zamani kulikuwa na wapmbav
 
Ni historia nzuri sana inasisimua ila mi ninasikitakita kuona thamani ya sarafu yetu ilivyoporomoka leo dola moja ya Marekani ni imependa thamani mara 440 zaidi ya ilivyokua miaka 45 iliyokwisha inasikitisha sana
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom