Historia ya Sarafu Yetu Tanzania

Mwl. Prof Kichuguu,

Nashukuru sana kwa hiyo elimu.............nimeprint hiyo story na kuwapa wanangu wamefurahia sana

Once again thanks

Mzee Ogah, umerudi kusoma hii kitu tena leo baada ya miaka mitano tungu tuiongelee? Nimepata notification na kuisoma nikakuta ni Mzee Ogah bado anatoa kudos tena: asante sana.

Wakati ule nilifanya research ya kina sana kuhusu tofauti ya pesa zetu (Kenya Uganda na Tanzania) ndipo nikaibua stori hii ndefu sana.

Nashukuru kama imekuwa na impact ya muda mrefu kwa watu wengi kwa muda mrefu kwa sababu nakumbuka tulimaliza kuijadili mwaka 2007, na kuanzia hapo nimekuwa napata messages za wanachama wapya mara kwa mara kila wanapoisoma. Ni miaka mitano imepita tangu niiandike; nilianza research hii kipindi ambacho Saddam Hussein alipokuwa ananyongwa.

Nakumbuka sana wakati huo kwa sababu niliacha project hii kwa muda kama wa mwezi mmoja hivi ku-reflect thamani ya uhai kutokana na video ya sadama alipokuwa anwekwa kitanzi na baadaye kuonekana akiwa kwenye sanda. Baada ya kuwa nimekusanya data za kutosha, sikuweza kupata muda wa kuziweka zote sawasawa mpaka wakati wa summer kwa vile nilikuwa na picha nyingi sana ambazo zilihitaji kupangwa kulingana na timeline ya stori yenyewe.

Hata hivyo summer ilipofika nikajikuta nalazimika kuzunguka barabarani na familia kwa takribani miezi miwili hadi mwishoni mwa July tuliporudi nyumbani ndipo nikaanza kuiweka sawasawa kwa makini (subject to typing errors).

Again, nafurahi kuwa kuna watu wengi wameiona ni both entertaining and educative!
 
Hapana, sarafu ndogo kabisa kutolewa na Benki Kuu ya Tanzania ilikuwa ya senti tano. Website ya benki kuu haina record nzuri ya kuonyesha historia ya sarafu yetu.

Nimeshindwa kupata baadhi ya sarafu kadhaa za kumbukumbu mbalimbali zilizotolewa nyakati za Nyerere na Mwinyi kwa mfano kumbukumbu ya mwaka wa mtoto wakati wa Nyerere, kumbukumbu ya kufunguliwa kwa jengo jipya benki kuu wakati huo n.k.

Nimeshakamilisha historia ya noti zetu; nitaipost baadaye nikipata muda wa kutosha, kwa hiyo wale wote wanaofurahia historia ya mambo ya nchi yetu kama mimi kaeni mkao wa kula tu.
Many thanks kichuguu for this.
 
Kichuguu!


Mkuu ina maana kabla ya uhuru nchi za Africa mashariki zilikuwa zinatumia sarafu au hela ya aina moja?je kabla ya uhuru kila nchi haikuwa na hela yake,maana kwenye hizo sarafu naona kuna 1952 halafu imeandikwa East Africa Sh.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Ousofia, Kuanzia mwaka 1920 nchi za Afrika ya mashariki zilikuwa zinatumia sarafu moja; sarafu ya kwanza ilikuwa ni East African Florin, ambayo ilikuwa replaced na East African Shilling baada ya muda mfupi usiozidi miezi sita. Nchi hizo zilitengana mwaka 1966 ambapo kila nchi ikawa na sarafu yake ingwa zote zileiendelea kutumia Shillingi; yaani kukawa na shilingi ya Kenya, shillingi ya Uganda na Shillingi ya Tanzania.
 
Last edited by a moderator:
Baada ya vita ya dunia mwaka 1919, Bara na Zanzibar pamoja na Kenya na Uganda zilikuwa chini ya himaya ya mwingereza ingawa kwa mikataba tofauti. Kuanzia hapo nchi hizo zilianza kutumia sarafu moja. Katika kipindi kifupi kuanzia mishoni mwaka 1919 hadi kati kati ya mwaka 1920, bara walitumia rupie za kijerumani pamoja na rupie za kiingereza zilizokuwa zikitumika nchini Kenya, Uganda na Zanzibar. Baada ya hapo, sarafu mpya ya Florin ya Afrika Mashariki iliingizwa kwenye mzunguko badala ya rupie na rupee. Kwa bahati mbaya sarafu hii ya Florin haikudumu muda mrefu na mwanzoni mwa mwaka 1921 ikabadilishwa na Shillingi ya Afrika ya Mashariki. Kwa hali hiyo kuna sarafu chache sana za Florin zilizotolewa katika kipindi hicho na sikufanikiwa kupata picha yake. Sarafu ya Shilingi ya Afrika Mashahariki ni kati ya sarafu imara sana zilizokaa kwenye mzunguko kwa muda mrefu bila kufanyiwa mabadiliko yoyote. Ilitolewa katika vipande vya senti 1, senti 5, senti 10, senti 50(nusu shillingi) na shilingi 1. Upande mmoka wa sarafu hizo ulionyesha jina la mtawala wa himaya ya uingereza, na upande wa pili ama ulikuwa na ama pembe za tembo au picha ya simba dume. Pembe za tembo zilikuwa kwenye sarafu za senti 1, senti 5 na senti 10 wakati simba dume alikuwa kwenye sarafu za senti hamsini na shilingi moja kama ifuatavyo

Nyuma ya sarafu

bronze.jpg


cupronickel.jpg

Upande ulioonyesha mtawala wa uingereza ulifanyiwa mabadiliko ya mara kwa mara kulingana na mabadiliko ya kiutawala. Kuanzia mwaka 1921 mpaka mwanzoni mwa mwaka 1936 wakati wa utawala wa Mfalme George wa tano sarafu zilikuwa na sura ifuatayo.
geoge5a.jpg


george5b.jpg

Baada ya kifo cha Mfame George wa tano na utawala kuchukuliwa na Mfalme Edward wa nane, ni sarafu moja tu iliyobadilishwa kwa vile mfalme huyu alivuliwa madaraka baada ya muda mfupi tu kutokana na uamuzi wake wa kuoa mwanamke aliyekuwa ameachika Marekani. Sarafu iliyobadilika wakati huo ilikuwa ya senti tano tu, ambayo ilionekana kama ifuatavyo

senti 5
edwardviii.jpg

Mfalme George wa sita aliyekuwa mdogo wa mfalme Edward wa nane alichukua madaraka mwishoni mwa mwaka huo huo wa 1936. Sarafu zilizotengezwa wakati wa utawala wake zilikuwa na sura za aina mbili. Sura ya kwanza ilionyesha mfalme kama GEORGIVS VI. Sarafu za aina hii zilitolewa kati ya mwaka 1937 hadi mwaka 1946; zilikuwa na sura ifuatayo.

gerge6ia.jpg


george6ib.jpg

Sarafu za aina ya pili cghini ya Mfalme george wa sita silikuwa na maneno ya GEORGIVS SEXTVS REX. Hizi zilitolewa kati ya

mwaka 1949 hadi mwaka 1952 alipofariki. sarafu hizo zilionekana kama ifuatavyo.
george6iia1.jpg


george6iib.jpg

Baada ya mfalme George wa sita kufariki, alirithiwa na binti yake Malkia Elizabeth wa pili mwaka 1952. Chini ya malkia huyu sarafu ziliokena kama ifuatavyo.
elizabeth2a.jpg


elizabeth2b.jpg

Sarafu hizi zilendelea kutumika hata baada ya kupata uhuru wetu. Kwa mafano sarafu zilizotolewa mwaka 1963 (baada ya uhuru)
zilionekana ifutavyo.

uhuru1.jpg

Ilipofika mwaka 1964, kukafanyika mabadiliko kidogo katika sura ya sarafu yetu kwa kuondoa maneno yanayoonyesha mtawala wa himaya ya kiingereza. Sarafu za senti tano na senti kumi zilizotolewa mwaka 1964 zilikuwa zinaonekana kama ifuatavyo.


uhuru2.jpg

Hata hivyo sarafu ya pamoja ya Afrika Mashariki ilifikia kikomo chake mwaka 1966 wakati Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilipovunjwa na kuundwa kwa benki kuu za Tanzania, Kenya na Uganda. Sijaelewa sababu ya kuvunjika kwa bodi hiyo ya sarafu, bado ninafanya utafiti. Nikizpta nitawagawieni.

..........................Inaendelea

Hizi nimewahi kuzitumia. Kabla Nyerere hajaleta visungura na visamaki vyake.
 
Umaskini kuondoka lazima tuanzie huku mara Lowassa awapo Magogoni.

Ili kurudisha heshima ya Pesa yetu Shillingi kuna haja hili kuwa halisi na tuache uchumi wa kwenye makaratasi!

The current coins in circulation are as follows: =/05, =/10, =/20, =/50, 1/=, 5/=, 10/=, 20/=, 50/=, 100/= and 200/=.

[h=3][/h]
Profesa Ndulu kuelekea 25/10/2015 kuna haja vijana wako kubadilika maana Mabadiliko haya epukiki.





[h=2]Banknotes and Coins[/h] [h=3]Banknotes Series[/h] The Bank of Tanzania introduced a new series of banknotes in January 2011. The Banknotes series are in the denominations of Shillings 500, 1000, 2000, 5000 and 10000.
The previous series of banknotes issued in 2003 continues to circulate in parallel with the new issue. These will be withdrawn from circulation gradually until a date when they will be declared demonetized.


[h=3]Currently Circulating Coins[/h] The current coins in circulation are as follows: =/05, =/10, =/20, =/50, 1/=, 5/=, 10/=, 20/=, 50/=, 100/= and 200/=.

[h=3][/h]

CC Ben Saanane.
 
Last edited by a moderator:
shukrani na nitaanza kuhifadh baadh ya sarafu za sasa kwa ajili ya kumbukmbu ya wanangu na vijukuu na vitukuu
 
Ahsante Kichuguu kwa shule.. Ila nakumbuka sijui ni shule ya msingi au sekondari tulisoma Mji wa kwanza kutengeneza Fedha yake yenyewe ni kilwa. Ila nimeshangaa sijaona popote pale Zanzibar ikitajwa.. Nahitaji ufafanuzi
 
A very useful thread! Mimi nimehifadhi shilingi tano ya Afrika mashariki, ya mwaka 1958: I hope itakua useful huko mbeleni!
 
Mkuu, Asante sana. Ama kwa hakika hili ni shamba darasa, cha kufanya naomba u-update huu uzi, ni miaka 11 sasa.
 
Dah uzi murua wa kumbukumbu.Hiyo senti hamsini ya kasungura tukiwa wadogo tuliitumia kununua pipi za vidonge kwenye duka la mzee mmoja kijijini kwetu
 
Back
Top Bottom