Rlechas_3a60
Member
- Oct 4, 2018
- 12
- 27
Nadharia ya Kiswahili
Kiswahili ni lugha ya Kibantu inayotumiwa na watu katika mawasiliano hasa Afrika Mashariki na ya Kati. Lugha ni sauti za nasibu zenye mpangilio maalumu zilizokubaliwa na watu ili zitumike kwa mawasiliano.Historia ya Kiswahili imeanza takriban miaka 1000 iliyopita kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Neno Swahili lina asili ya Kiarabu ‘Sahil’ ina maana ya pwani, “sawahil” “as-sawāhilī” ni wingi wake kwa kumaanisha yote yanayohusiana na pwani, watu au utamaduni wa eneo la Pwani.
Asili ya Lugha ya Kiswahili
Kuna nadharia mbalimbali zinazohusu asili ya lugha ya Kiswahili. Nadharia hizo ni kama vile Kiswahili ni Kikongo, Kiswahili ni Pijini au Krioli, Kiswahili ni Kiarabu, Kiswahili ni lugha ya vizalia, pamoja na Kiswahili ni Kibantu.
Kiswahili asili Yake ni Kikongo
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni huko Kongo ambayo baadaye iliitwa Zaire na sasa inaitwa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo. Dai hili linaimarishwa na wazo lingine linalodai kwamba katika vipindi kongwe vilivyopata kuwako, sehemu za Pwani ya Afrika mashariki hazikuwa zimekaliwa na watu. Kutokana na hali ya vita, uchungaji na biashara, inadaiwa kuwa Wabantu walitoka sehemu za Kongo walisambaa na kuja pwani ya Afrika mashariki kupitia Kigoma. Baadhi ya wabantu hawa walipitia sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao, walieneza pia lugha zao ikiwemo hii ya Kiswahili.
Sababu hizo hazina mashiko kutokana na kuwa wanahistoria hawajaeleza ni lini hasa watu hao walihamia maeneo ya pwani ya Afrika ya Mashariki.
Kiswahili ni Ki-Pijini au Ki-Krioli
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa Kiswahili ni Ki-Pijini. Wataalamu hawa hudai kwamba Ki-Pijini ni lugha ambayo huzaliwa kutokana na kukutanika kwa makundi mawili (A) na (B) yanayotumia lugha mbili tofauti. Ili makundi haya yaweze kuwasiliana kunaundwa lugha ambayo kitabia ni tofauti na zile zinazozungumzwa na makundi yanayohusika. Lugha hii inaweza kuwa na msamiati mwingi kutoka lugha kati ya zile mbili, au inaweza kuwa na msamiati wenye uzito sawa. Lugha hiyo ndiyo inayoitwa Ki-Pijini. Mazingira yanayosababisha kuwepo Ki-Pijini ni kama vile biashara, utumwa, na ukoloni.
Nadharia hii inasema kwamba wakati Waarabu walipokuja pwani ya Afrika ya Mashariki walioa wanawake wa Afrika na hivyo kutokana na mwingiliano wa lugha zao tofauti ilizaliwa lugha mpya ambayo ni aina ya Pijini. Baadae watoto walipozaliwa walikuta lugha hiyo mpya ambayo ni Pijini. Watoto hao waliiendeleza lugha waliyoikuta na baadae ikazaliwa Krioli. Krioli ni Pijini iliyokomaa.
Kwa mantiki ya nadharia hii, wataalamu hawa hukiona Kiswahili kuwa kilianza kama Ki-Pijini kwani ni tokeo la mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki na wageni wa kutoka Mashariki ya Kati, hususan Waarabu. Aidha, husisitiza kuwa lugha ya Kiswahili haikuwepo kabla ya hapo.
Wataalamu pia wanadai kwamba watu wanaozungumza Ki- Pijini wanaweza kuishi pamoja kwa muda wa karne nyingi na kwa hiyo wakaweza kuzoeana na hata kufikia hatua ya kuoana. Wakioana watoto wao huikuta lugha ya ki-Pijini ama lugha yao ya kwanza. Inapofikia hatua ya aina hii kwa watoto wanaozungumza lugha hiyo, wao husemekana sasa wanazungumza lugha ya Ki-Krioli, lugha ambayo ni hatua ya juu ya Ki-Pijini, yaani Ki-Pijini kilichokomaa.
Nadharia hii hutumia kigezo cha msamiati wa Kiswahili kuonesha uhusiano uliopo kati ya Kiswahili na Kiarabu. Wanadai kuwa, msamiati mwingi wa Kiswahili unatokana na Kiarabu. Hivyo huhitimisha kuwa hapana shaka Kiarabu kimehusika katika kuizalisha na kuikomaza lugha ya Kiswahili.
Kiswahili ni Kibantu (Lugha ya Jamii ya Vizalia)
Wanahistoria wanaeleza kuwa Kiswahili kimetokana na Kibantu kwa kutoa sababu mbalimbali. Miongoni mwa sababu hizo ni ushahidi wa kihistoria na ushahidi wa kiisimu.
Ushahidi wa Kihistoria Kwamba Kiswahili ni Kibantu
Baada ya kuangalia ushahidi wa kiisimu kuhusu asili ya Kiswahili, katika sehemu hii Maganga (1997) aliendelea kuchambua ushahidi wa Kihistoria unaothibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa katika upwa wa Afrika Mashariki hata kabla ya ujio wa wageni kama vile Waarabu na Wazungu. Ushahidi huu ulitolewa na wageni mbalimbali waliofika hapa Afrika Mashariki. Wote wanathibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa hapa Afrika Mashariki kabla ya ujio wa wageni.
Ugunduzi wa Ali-Idris ulifanywa huko Sicily yapata mwaka 1100-1166. Kwenye mahakama ya mfalme Roger II. Licha ya kufahamika kuwa Kiswahili, kilipata kuandikwa kabla ya 10BK. Ali-Idris alikuwa wa kwanza kugundua jina la zamani la Zanzibar kuwa ni Unguja. Katika maelezo yake anaandika pia majina kama vile kikombe, mkono wa tembo, muriani, na kisukari, ambayo ni ya ndizi mbalimbali zilizokuwa zikipatikana huko.
Ushahidi wa Marco Polo ambaye alijishughulisha sana na masuala mbalimbali ya kijiografia na alisafiri sehemu nyingi duniani. Marco Polo aliandika “Zanzibari ni kisiwa kizuri ambacho kina ukubwa wa mzunguko wa maili 200. Watu wote wanaabudu (Mungu), wana Mfalme na wanatumia lugha yao, na hawalipi kodi (ushuru) kwa mtu.” Safari za Marco Polo 1958:301
Kiswahili leo
Katika Tanzania Kiswahili kimekuwa lugha rasmi ya Serikali na Taifa. Shule za msingi hutumia Kiswahili lakini shule za sekondari na vyuo bado zinaendelea kufundisha kwa Kiingereza. Februari 15 2015 Rais Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa kubadilisha lugha ya elimu nchini kwa kutumia Kiswahili kwenye ngazi zote hadi shule za sekondari na chuo kikuu.
Kenya imetangaza Kiswahili kuwa lugha ya taifa lakini inaendelea kutumia Kiingereza katika shughuli za Serikali. Watu wa matabaka ya juu mara nyingi hupendelea kutumia Kiingereza wakiona ni lugha bora. Lakini tangu 1986 wanafunzi wote wanatakiwa kujifunza Kiswahili katika shule za sekondari. Tatizo mojawapo ni kuwepo wa makabila makubwa kama Wakikuyu au Waluo wenye wasemaji wengi sana katika eneo moja, hali isiyosaidia kujifunza lugha tofauti. Pia kaskazini na magharibi mwa Kenya wenyeji wengi si wasemaji wa lugha za Kibantu nao hawaoni Kiswahili ni lugha rahisi.
Uganda inatumia Kiswahili kama lugha ya Polisi na Jeshi, hali ambayo haikuongeza upendo wa Waganda kwa lugha kutokana na historia ya Uganda ya kuwa na vita na Serikali za kijeshi. Lakini kinasikika pia kama lugha ya biashara masokoni. Pamoja na kwamba Waganda walikichukulia Kiswahili kama lugha ya kitumwa lakini pia lugha hii ilionekana kuwa na ustaarabu wa Kiarabu zaidi, yaani Uislamu. Lugha ya Kiswahili ilitumika katika kueneza dini hiyo.
Mashariki mwa Kongo Kiswahili kimeenea sana: ni moja kati ya lugha nne za kitaifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kwenye visiwa vya Ngazija (Comoros) kuna lahaja mbalimbali za Kiswahili zinazotumika na wananchi.
Kiswahili ni lugha ya Kibantu inayotumiwa na watu katika mawasiliano hasa Afrika Mashariki na ya Kati. Lugha ni sauti za nasibu zenye mpangilio maalumu zilizokubaliwa na watu ili zitumike kwa mawasiliano.Historia ya Kiswahili imeanza takriban miaka 1000 iliyopita kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Neno Swahili lina asili ya Kiarabu ‘Sahil’ ina maana ya pwani, “sawahil” “as-sawāhilī” ni wingi wake kwa kumaanisha yote yanayohusiana na pwani, watu au utamaduni wa eneo la Pwani.
Asili ya Lugha ya Kiswahili
Kuna nadharia mbalimbali zinazohusu asili ya lugha ya Kiswahili. Nadharia hizo ni kama vile Kiswahili ni Kikongo, Kiswahili ni Pijini au Krioli, Kiswahili ni Kiarabu, Kiswahili ni lugha ya vizalia, pamoja na Kiswahili ni Kibantu.
Kiswahili asili Yake ni Kikongo
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni huko Kongo ambayo baadaye iliitwa Zaire na sasa inaitwa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo. Dai hili linaimarishwa na wazo lingine linalodai kwamba katika vipindi kongwe vilivyopata kuwako, sehemu za Pwani ya Afrika mashariki hazikuwa zimekaliwa na watu. Kutokana na hali ya vita, uchungaji na biashara, inadaiwa kuwa Wabantu walitoka sehemu za Kongo walisambaa na kuja pwani ya Afrika mashariki kupitia Kigoma. Baadhi ya wabantu hawa walipitia sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao, walieneza pia lugha zao ikiwemo hii ya Kiswahili.
Sababu hizo hazina mashiko kutokana na kuwa wanahistoria hawajaeleza ni lini hasa watu hao walihamia maeneo ya pwani ya Afrika ya Mashariki.
Kiswahili ni Ki-Pijini au Ki-Krioli
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa Kiswahili ni Ki-Pijini. Wataalamu hawa hudai kwamba Ki-Pijini ni lugha ambayo huzaliwa kutokana na kukutanika kwa makundi mawili (A) na (B) yanayotumia lugha mbili tofauti. Ili makundi haya yaweze kuwasiliana kunaundwa lugha ambayo kitabia ni tofauti na zile zinazozungumzwa na makundi yanayohusika. Lugha hii inaweza kuwa na msamiati mwingi kutoka lugha kati ya zile mbili, au inaweza kuwa na msamiati wenye uzito sawa. Lugha hiyo ndiyo inayoitwa Ki-Pijini. Mazingira yanayosababisha kuwepo Ki-Pijini ni kama vile biashara, utumwa, na ukoloni.
Nadharia hii inasema kwamba wakati Waarabu walipokuja pwani ya Afrika ya Mashariki walioa wanawake wa Afrika na hivyo kutokana na mwingiliano wa lugha zao tofauti ilizaliwa lugha mpya ambayo ni aina ya Pijini. Baadae watoto walipozaliwa walikuta lugha hiyo mpya ambayo ni Pijini. Watoto hao waliiendeleza lugha waliyoikuta na baadae ikazaliwa Krioli. Krioli ni Pijini iliyokomaa.
Kwa mantiki ya nadharia hii, wataalamu hawa hukiona Kiswahili kuwa kilianza kama Ki-Pijini kwani ni tokeo la mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki na wageni wa kutoka Mashariki ya Kati, hususan Waarabu. Aidha, husisitiza kuwa lugha ya Kiswahili haikuwepo kabla ya hapo.
Wataalamu pia wanadai kwamba watu wanaozungumza Ki- Pijini wanaweza kuishi pamoja kwa muda wa karne nyingi na kwa hiyo wakaweza kuzoeana na hata kufikia hatua ya kuoana. Wakioana watoto wao huikuta lugha ya ki-Pijini ama lugha yao ya kwanza. Inapofikia hatua ya aina hii kwa watoto wanaozungumza lugha hiyo, wao husemekana sasa wanazungumza lugha ya Ki-Krioli, lugha ambayo ni hatua ya juu ya Ki-Pijini, yaani Ki-Pijini kilichokomaa.
Nadharia hii hutumia kigezo cha msamiati wa Kiswahili kuonesha uhusiano uliopo kati ya Kiswahili na Kiarabu. Wanadai kuwa, msamiati mwingi wa Kiswahili unatokana na Kiarabu. Hivyo huhitimisha kuwa hapana shaka Kiarabu kimehusika katika kuizalisha na kuikomaza lugha ya Kiswahili.
Kiswahili ni Kibantu (Lugha ya Jamii ya Vizalia)
Wanahistoria wanaeleza kuwa Kiswahili kimetokana na Kibantu kwa kutoa sababu mbalimbali. Miongoni mwa sababu hizo ni ushahidi wa kihistoria na ushahidi wa kiisimu.
Ushahidi wa Kihistoria Kwamba Kiswahili ni Kibantu
Baada ya kuangalia ushahidi wa kiisimu kuhusu asili ya Kiswahili, katika sehemu hii Maganga (1997) aliendelea kuchambua ushahidi wa Kihistoria unaothibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa katika upwa wa Afrika Mashariki hata kabla ya ujio wa wageni kama vile Waarabu na Wazungu. Ushahidi huu ulitolewa na wageni mbalimbali waliofika hapa Afrika Mashariki. Wote wanathibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa hapa Afrika Mashariki kabla ya ujio wa wageni.
Ugunduzi wa Ali-Idris ulifanywa huko Sicily yapata mwaka 1100-1166. Kwenye mahakama ya mfalme Roger II. Licha ya kufahamika kuwa Kiswahili, kilipata kuandikwa kabla ya 10BK. Ali-Idris alikuwa wa kwanza kugundua jina la zamani la Zanzibar kuwa ni Unguja. Katika maelezo yake anaandika pia majina kama vile kikombe, mkono wa tembo, muriani, na kisukari, ambayo ni ya ndizi mbalimbali zilizokuwa zikipatikana huko.
Ushahidi wa Marco Polo ambaye alijishughulisha sana na masuala mbalimbali ya kijiografia na alisafiri sehemu nyingi duniani. Marco Polo aliandika “Zanzibari ni kisiwa kizuri ambacho kina ukubwa wa mzunguko wa maili 200. Watu wote wanaabudu (Mungu), wana Mfalme na wanatumia lugha yao, na hawalipi kodi (ushuru) kwa mtu.” Safari za Marco Polo 1958:301
Kiswahili leo
Katika Tanzania Kiswahili kimekuwa lugha rasmi ya Serikali na Taifa. Shule za msingi hutumia Kiswahili lakini shule za sekondari na vyuo bado zinaendelea kufundisha kwa Kiingereza. Februari 15 2015 Rais Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa kubadilisha lugha ya elimu nchini kwa kutumia Kiswahili kwenye ngazi zote hadi shule za sekondari na chuo kikuu.
Kenya imetangaza Kiswahili kuwa lugha ya taifa lakini inaendelea kutumia Kiingereza katika shughuli za Serikali. Watu wa matabaka ya juu mara nyingi hupendelea kutumia Kiingereza wakiona ni lugha bora. Lakini tangu 1986 wanafunzi wote wanatakiwa kujifunza Kiswahili katika shule za sekondari. Tatizo mojawapo ni kuwepo wa makabila makubwa kama Wakikuyu au Waluo wenye wasemaji wengi sana katika eneo moja, hali isiyosaidia kujifunza lugha tofauti. Pia kaskazini na magharibi mwa Kenya wenyeji wengi si wasemaji wa lugha za Kibantu nao hawaoni Kiswahili ni lugha rahisi.
Uganda inatumia Kiswahili kama lugha ya Polisi na Jeshi, hali ambayo haikuongeza upendo wa Waganda kwa lugha kutokana na historia ya Uganda ya kuwa na vita na Serikali za kijeshi. Lakini kinasikika pia kama lugha ya biashara masokoni. Pamoja na kwamba Waganda walikichukulia Kiswahili kama lugha ya kitumwa lakini pia lugha hii ilionekana kuwa na ustaarabu wa Kiarabu zaidi, yaani Uislamu. Lugha ya Kiswahili ilitumika katika kueneza dini hiyo.
Mashariki mwa Kongo Kiswahili kimeenea sana: ni moja kati ya lugha nne za kitaifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kwenye visiwa vya Ngazija (Comoros) kuna lahaja mbalimbali za Kiswahili zinazotumika na wananchi.