Historia ya Bendera ya Zanzibar

Jaman hii bendera ya wenzetu visiwani ina rangi kadhaa ambazo kwazo binafsi sijafahamu zinawakili ni so naomba kujuzwa zinawakilisha nini?
 
Ama kweli hii nchi inaenda orjojo,bendere hiyo ilianzishwa lini maana ninavyoelewa kwa mujibu wa katiba yetu zanzibar siyo nchi,bali ni sehemu ya nchi ya Tanzania
 
Ama kweli hii nchi inaenda orjojo,bendere hiyo ilianzishwa lini maana ninavyoelewa kwa mujibu wa katiba yetu zanzibar siyo nchi,bali ni sehemu ya nchi ya Tanzania
Una umri gani kijana? Nafikiri unaweza kujua ya ufisadi kwani hayo ndiyo unayoweza kuijuwa!
 
Sio miaka mingi imezinduliwa na juu mkono wa kushoto ina bendera ndogo ya TANZANIA
 
Jaman hii bendera ya wenzetu visiwani ina rangi kadhaa ambazo kwazo binafsi sijafahamu zinawakili ni so naomba kujuzwa zinawakilisha nini?

THE ZANZIBAR FLAG ACT NO.12 OF 2004
Section 3. There shall be a Zanzibar Flag which shall be of the description specified in the
Schedule to this Act.


SCHEDULE
{ Made Under Section 3 }


A rectangular flag divided into three equal portions horizontally; the bottom portion is green
(signifying the land of Zanzibar), the middle portion is black (signifying the colour of the original
people of Zanzibar
) and the top portion is light blue (signifying the sea and sky surrounding
Zanzibar
); with an insertion of the Tanzania National Flag at the top of the left hand corner; of
the following design.


zflagbig.gif
 
Jifunze hapa!


Kabla hatujavamiwa na wajerumani, nchi yetu (Bara na Visiwa vya Zanzibar) ilitawaliwa na Sultan wa Zanzibar chini ya Sultan wa Oman. Bendera ya Sultani wa Zanzibar ilikuwa hii hapa chini.
om-old.gif

Baada ya mikataba ya Carl Peters and Berlin conference, nchi yetu yote iliwekwa chini ya utawala wa Mjerumani. Mjerumani hakuwa na interest katika visiwa vya Zanzibar, hivyo akaingia deal na Uingereza. Walitaka Uingereza iwape visiwa vya Heligoland vilivyoko North Sea, wao watoe visiwa vya Zanzibar kwa Uingereza. Hivyo Zanzibar ikwa chini ya mweingereza, ambaye aliamua kumwacha sultan aendelee kuula. Bara ikaitwa Deutsch-Ostafrika (German East Africa). Bendera ya mjerumani hapa bara ilikuwa hii.
deutsch-ostafrika-fahne.jpg
Kwa Zanzibar kulikuwa na bendera mbili. Ya kwanza ilikuwa ya mwingereza; ilikuwa na sura hii hapa:
tz-zzrs.gif
Bendera ya pili huko Zanzibar ilikuwa ya Sultan ambaye alikuwa hana uhusiano na Sultani wa Oman tena kwa vile alikuwa chini ya waingereza. Bendara yake ilibadilishwa na kuwa ifuatavyo:
800px-flag_of_the_sultanate_of_zanzibar_svg.jpg
Baada ya ujerumani kupoteza makoloni yake kufuatia kushindwa vita ya dunia ya kwanza, sehemu ya bara iliwekwa chini ya mwingereza. Huyu ndiye aliita sehemu ya bara kuwa "Tanganyika" akimaanisha ili nyika iliyo nyuma ya Tanga. Bendera ya Tanga ilikuwa hii:
tz-tang.gif
Katika kipindi cha utawala mwingereza, tulitumia bendera za aina kama tatu hivi lama ifuatavyo:

br-tanganyika.jpg


tztgclb.gif


tztgr.gif
Gavana wa kiingereza yeye alikuwa akitumia bendera tofauti kama invyoonyeshwa hapa chini

governors-flag.gif
Kunako May 1961 tulipata madaraka ya ndani chini ya Nyerere. Katika kipindi hicho tukawa tunatumia bendera ya kiingereza zilizoonyeshwa hapo juu na bendera ya madaraka ilikuwa kama ifuatavyo
tztng61.gif

hata hivyo inaaminika kuwa Nyerere alipendelea zaidi ile bendera ya TANU
tztanu.gif
Ilivyofika December 1961 tukapa uhuru na hivyo bendera ya mwingereza ikashushwa. Tukapandisha bendera ya kwanza ya Tanganyika iliyokuwa kama ifuatavyo:
independent-tanganyika.jpg
hata hivyo baada ya uhuru, tuliendelea kubaki chini ya malkia aliyekuwa anawakilishwa na Governor General, Sir Richard Turnbull; bendera ya Governor General ilikuwa kama ifuatavyo:

governor_general.gif

Ilipofika December 1962 tukawa jamhuri na hivyo kuondokana kabisa na alama za kiingereza ispokuwa pesa (Siku nyingine nitatoa historia ya pesa zetu). Kwa bahati mbaya sikuweza kupata bendera ya rais mara baada ya kuwa Jamhuri


Kwa upande wa Zanzibar, waliendelea kuwa chini ya mwingereza na sultani hadi december mwaka 1963 ambao mwingereza aliamua kutoa uhuru kwa zanzibar chini ya Sultan. Bendera ya Zanzibar huru ( Sultanate of zanzibar) ilikuwa sura nyekunu na karafuu mbili. Sura halisi ya karafuu haijulikani sawasawa. Ila bendera hiyo ilionekana kama mojawapo ya hizi mbili:

tz-zan63.gif


tz-zz63.gif

hata hivyo serikali hii haikudumu zaidi ya siku 33, ikapinduliwa kwa nguvu na chama cha ASP. Baada ya mapinduzi, iliundwa serikali ya Jamhuri ya Zanzibar. Mwanzoni, bendera ya Jamhuri ya Zanzibar ilikuwa hii hapa chini
tz-za64a.gif
lakini baada ya muda mfupi ikabadilishwa na kuwa kama ifuatavyo huku ikiwa na rangi za bendera ya ASP
tz-za64b.gif
Katika kipindi kifupi sana wakati wa machafuko ya mapinduzi yale, Pemba ilijitangaza kuwa ni nchi huru ya jamhuri ya pemba, lakini nadhani walidhibitiwa haraka sana na majeshi ya ASP. bendera ya Jamhuri ya Pemba ilikuwa kama ifuatavyo:
tz_pemba.gif

Katika kipindi cha miezi mitatu baada ya mapinduzi, visiwa vya Zanzibar viliunganika tena na bara baada ya kutenganishwa kwa miaka ipatayo 80. Muungano huo ulijulikana kama jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuanzaia wakati huo, bendera ya Tanzania ni kama ifuatavyo:
tz.gif
Ile ya rais wa jamhuri ya muungano iko kama ifuatavyo:
tz_pre.gif

Mwaka 2005, Zanzibar waliamua kuwa na bendera yao. bendera hiyo ni mchanganyiko wa bendera ya mwisho ya jamhuri ya zanzibar na ile ya jamhuriu ya muungano wa Tanzania. Inaonekana kama ilivyoonyeshwa hapa chini.
tz-za05.gif
Rais wa Zanzibar naye akatengenezewa bendera yake ambayo inaonekana kama ifuatavyo hapa chini
tz-zapr.gif
Kama nimekosea sehemu yoyote katika mapitio yangu ya historia ya bendera nchini Tanzania, naomba marekebisho. Safari nyingine nitapitia historia ya fedha zetu; najua itakuwa ndefu sana lakini nitaigawa katika sehemu sita Kipingi cha Mjerumani, Kipindi cha mweingereza, Kipindi cha Nyerere, Kipindi cha Mwinyi na baada ya Mwinyi.
 
Back
Top Bottom