Historia inapiga king’ora kwa suala la Wamachinga duniani, nani anasikia?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Dunia iko kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda (4th Industrial Revolution) ambapo matumizi ya teknolojia ya kisasa yanachukuwa nafasi kubwa kwenye uzalishaji na ubora wakati hasara ya mapinduzi haya ya nne ni rasilimaliwatu kukosa fursa za ajira ambazo zimechukuliwa na teknolojia (mashine na mitambo).

Historia ina Kawaida ya Kujirejeleza (Kujirudia)
Mapinduzi ya viwanda (Industrial Revolution) yalitukia karne ya 18 ambapo matumizi ya mashine yaliondoa rasilimaliwatu (wafanyakazi) nje ya ajira na hawa walioondolewa kujikuta wanakuwa Wamachinga wasio na fursa wala maamuzi kwenye mfumo huo mpya wa maisha ya binadamu ulioibuka duniani nyakati hizo.

Ni hawa Wamachinga ndiyo baadaye wakaja kuwa rasilimali ya kufanikisha mapinduzi ya mfumo kandamizi wa itikadi ya kibepari kwa kusikiliza mafundisho ya Muasisi wa mfumo mbadala wa Ukomunisti Karl Marx ambaye aliwashawishi kwamba ili kuondokana na mfumo dhalili wa Kibepari inawabidi kufanya mapinduzi tena ya moto (siyo ya baridi) ili wawezekuwa huru toka kwenye ukandamizaji.

Machinga hawa wa wakati huo walikosa hata vipande vidogo vya ardhi oevu na za rutuba ambazo zilimilikiwa na mapapa wa ardhi kwa jina la Makabaila na kuwafanya Wamachinga hawa kuwa wapangaji kwenye ardhi ya nchi zao na kushurutishwa kulipa kodi ya pango la kuishi kwenye ardhi zao wenyewe. Karne nne zimepita sasa 17 – 20 bado dunia ya leo inashuhudia jeshi kubwa la Wamachinga likizaliwa na kuzagaa katika mabara yote na nchi zote bila kuwa na mpango maalum wa kuwaratibu.

Tahadhari
Wakati tunatambua umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika uzalishaji mali na utoaji huduma na kwamba matumizi ya mitulinga haina budi kupungua, ni vivyo hivyo kwa pamoja katika mkondo huo wa uelewa tunatambua umuhimu wa Wamachinga walioondolewa na teknolojia ya mapinduzi ya viwanda kuhakikisha usalama wa dunia na mitaji ya wanaonufaika na mfumo huo mpya ili kwamba dunia isije ikajikuta imetengeneza akina Karl Marx wapya ambao wao wataona umuhimu wa kutumia Wamachinga kupindua mfumo mpya uliowafanya kuwa Wamachinga wasio na hatima zao mikononi mwao.

Athari za Siasa Katika Mifumo ya Uchumi Duniani
Maamuzi ya kisiasa duniani ndiyo yanaathiri na kuamua mifumo ya uchumi ambayo hiyo huja na faida na hasara huku kundi dogo ndilo linafaidi faida na kundi kubwa linaangamia kwa hasara. Mzigo wa Wamachinga unaelemea dunia kiasi kwamba kutokuwepo kwao hata kwa siku moja kutaokoa mengi katika mfumo wa maisha ya wanadamu licha ya faida zao zinazojulikana pia kuwepo, kwahiyo hapa ni suala la gharama ya fursa (Opportunity Cost).

Tafakari hii Modeli (Model) Katika Sura ya Agenda ya Machinga:-
If Motorbike commuters in Tanzania stopped using the transport for a day, that will be equivalent to health facilities discharging half of the admissions (hospitalized patients), save approximately 70% of daily traffic accidents across the nation, relieve Traffic Officers of excess routine work by 50%, cut Magistrates’ backlogs by 30%, reduce orphans, desolates, widows and widowers by at least 10% and free Inmate Prisons Cells by 25%, Majwala, D. O. (2021)


Kama abiria wa pikipiki wataacha kutumia usafiri huo kwa siku, hiyo itakuwa sawa na kuruhusu nusu ya wagonjwa toka walikolazwa Tanzania, kuokoa ajali za barabarani kwa 70% kwa siku nchini, kuwapunguzia kazi za ziada za siku Maafisa wa usalama barabarani kwa 50%, kuwapunguzia Mahakimu mlundikano wa kazi kwa 30%, kupunguza yatima, wakiwa, wajane na wagane angalao kwa 10% na kupunguza msongamano kwenye Magereza ya Mahabusu kwa asilimia 25%, Majwala, D. O. (2021)
 
Mkuu usicheke, dunia imepoa sana na tabaka lililojuu limekaa muda sana. Tuombee kutokee mabadiriko ya Koo za utawala na mfumo mpya wa maisha na kitu pekee kitacholeta mabadiriko hayo ni Vita ya dunia. No war no new tycoon.
Kwa silaha zilizopo duniani leo hii vita kuu ya tatu ya dunia itahitimisha civilization. Hakuna kitakachosalia.
 
Kwa silaha zilizopo duniani leo hii vita kuu ya tatu ya dunia itahitimisha civilization. Hakuna kitakachosalia.
Hapana lazima maisha yaendelee. Kama wanadamu walivuka kwenye great death ama black death aka Prague na pia viumbe hai walivuka kipindi Cha permian triasic extinction. Who will stop us?
 
hii imekaaje, karne ya 17 watu kukoswa ardhi meanwhile population ilikuwa less!!.
Maeneo yaliyokuwa yakikaliwa na binadamu yalikuwa machache kuliko maeneo yaliyokuwa yakikaliwa na wanyama pori wakali, nani angeweza kwenda kushi na Simba porini kisa ardhi ni kubwa? Mfano ardhi ya Tz sehemu inayokaliwa na binadamu ni 25% tu, sehemu iliyosalia ni mapori ya wanyama na hifadhi.
 
Maeneo yaliyokuwa yakikaliwa na binadamu yalikuwa machache kuliko maeneo yaliyokuwa yakikaliwa na wanyama pori wakali, nani angeweza kwenda kushi na Simba porini kisa ardhi ni kubwa? Mfano ardhi ya Tz sehemu inayokaliwa na binadamu ni 25% tu, sehemu iliyosalia ni mapori ya wanyama na hifadhi.
itoshe kwa kusema kwamba:, shida haikuwa Ardhi na bado dunia haijawa na shida ardhi. shida ili kuwa ni hofu yao dhidi ya wanyama wakali, wangeliondolewa/ondoa hofu yao dhana ya shida ya ardhi ingelibaki ni pumbao tu. hata new York ilikuwa ni pori ile wenyewe guts na risk takers wameibadili na kuwa maghorofa.
 
Mkuu usicheke, dunia imepoa sana na tabaka lililojuu limekaa muda sana. Tuombee kutokee mabadiriko ya Koo za utawala na mfumo mpya wa maisha na kitu pekee kitacholeta mabadiriko hayo ni Vita ya dunia. No war no new tycoon.
Mkuu THE LOST,
Hawa jamaa wako smart, kwasababu wanajuwa yanayoweza kuwakuta kwa mfumo walioujenga ambao siyo rafiki kwa wanyonge ambao ndiyo wengi, tayari waliishajiandaa zamani kwa kutengeneza mfumo mwingine (wameuficha kwenye madroo) ambao utatumika endapo Wamachinga watafanya mapinduzi ya pili ya Marxism. Mfumo huo mpya wameutambulisha kwa jina la NEW WORLD ORDER, wewe unadhihirisha kwa mchango wako huo kuwa ni Mwanazuoni mzuri sana, hivyo fuatilia hiyo New World Order, ni hatari kuliko mfumo tulio nao hivi sasa ambao wanyonge hawana chao wala sauti. Wakati fulani nakubaliana na wewe kuwa dawa inaweza kuwa ni WW tu.
 
Dunia iko kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda (4th Industrial Revolution) ambapo matumizi ya teknolojia ya kisasa yanachukuwa nafasi kubwa kwenye uzalishaji na ubora wakati hasara ya mapinduzi haya ya nne ni rasilimaliwatu kukosa fursa za ajira ambazo zimechukuliwa na teknolojia (mashine na mitambo).

Historia ina Kawaida ya Kujirejeleza (Kujirudia)
Mapinduzi ya viwanda (Industrial Revolution) yalitukia karne ya 18 ambapo matumizi ya mashine yaliondoa rasilimaliwatu (wafanyakazi) nje ya ajira na hawa walioondolewa kujikuta wanakuwa Wamachinga wasio na fursa wala maamuzi kwenye mfumo huo mpya wa maisha ya binadamu ulioibuka duniani nyakati hizo.

Ni hawa Wamachinga ndiyo baadaye wakaja kuwa rasilimali ya kufanikisha mapinduzi ya mfumo kandamizi wa itikadi ya kibepari kwa kusikiliza mafundisho ya Muasisi wa mfumo mbadala wa Ukomunisti Karl Marx ambaye aliwashawishi kwamba ili kuondokana na mfumo dhalili wa Kibepari inawabidi kufanya mapinduzi tena ya moto (siyo ya baridi) ili wawezekuwa huru toka kwenye ukandamizaji.

Machinga hawa wa wakati huo walikosa hata vipande vidogo vya ardhi oevu na za rutuba ambazo zilimilikiwa na mapapa wa ardhi kwa jina la Makabaila na kuwafanya Wamachinga hawa kuwa wapangaji kwenye ardhi ya nchi zao na kushurutishwa kulipa kodi ya pango la kuishi kwenye ardhi zao wenyewe. Karne nne zimepita sasa 17 – 20 bado dunia ya leo inashuhudia jeshi kubwa la Wamachinga likizaliwa na kuzagaa katika mabara yote na nchi zote bila kuwa na mpango maalum wa kuwaratibu.

Tahadhari
Wakati tunatambua umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika uzalishaji mali na utoaji huduma na kwamba matumizi ya mitulinga haina budi kupungua, ni vivyo hivyo kwa pamoja katika mkondo huo wa uelewa tunatambua umuhimu wa Wamachinga walioondolewa na teknolojia ya mapinduzi ya viwanda kuhakikisha usalama wa dunia na mitaji ya wanaonufaika na mfumo huo mpya ili kwamba dunia isije ikajikuta imetengeneza akina Karl Marx wapya ambao wao wataona umuhimu wa kutumia Wamachinga kupindua mfumo mpya uliowafanya kuwa Wamachinga wasio na hatima zao mikononi mwao.

Athari za Siasa Katika Mifumo ya Uchumi Duniani
Maamuzi ya kisiasa duniani ndiyo yanaathiri na kuamua mifumo ya uchumi ambayo hiyo huja na faida na hasara huku kundi dogo ndilo linafaidi faida na kundi kubwa linaangamia kwa hasara. Mzigo wa Wamachinga unaelemea dunia kiasi kwamba kutokuwepo kwao hata kwa siku moja kutaokoa mengi katika mfumo wa maisha ya wanadamu licha ya faida zao zinazojulikana pia kuwepo, kwahiyo hapa ni suala la gharama ya fursa (Opportunity Cost).

Tafakari hii Modeli (Model) Katika Sura ya Agenda ya Machinga:-
If Motorbike commuters in Tanzania stopped using the transport for a day, that will be equivalent to health facilities discharging half of the admissions (hospitalized patients), save approximately 70% of daily traffic accidents across the nation, relieve Traffic Officers of excess routine work by 50%, cut Magistrates’ backlogs by 30%, reduce orphans, desolates, widows and widowers by at least 10% and free Inmate Prisons Cells by 25%, Majwala, D. O. (2021)


Kama abiria wa pikipiki wataacha kutumia usafiri huo kwa siku, hiyo itakuwa sawa na kuruhusu nusu ya wagonjwa toka walikolazwa Tanzania, kuokoa ajali za barabarani kwa 70% kwa siku nchini, kuwapunguzia kazi za ziada za siku Maafisa wa usalama barabarani kwa 50%, kuwapunguzia Mahakimu mlundikano wa kazi kwa 30%, kupunguza yatima, wakiwa, wajane na wagane angalao kwa 10% na kupunguza msongamano kwenye Magereza ya Mahabusu kwa asilimia 25%, Majwala, D. O. (2021)
Kuna hoja fikirishi! Hii 4IR inatusukuma mahala ambapo si salama sana, hivyo inabidi Serikali za Dunia kujipanga na kuona ni namna gani ya kukabiliana na hili dude ambalo tayari lipo ndani. IoT, AI, BC, nk ni majinamizi ambayo yataifanya dunia kuwa tofauti sana. Utafika wakati watu hatuendi ofisini (kama zitakuwepo) badala yake tutafanya kazi tukiwa kwenye sebule zetu! Ni wakati sasa ukijenga nyumba ufikirie kutenga kaeneo ka ofisi nyumbani kwako. Naona kazi zitaisha. Kuna nchi hakuna traffic barabarani (ajira imepunguzwa) badala yake kuna camera zinafanya kila kitu. Hapa kwetu ukitoka Moshi kwenda Arusha unakutana na traffic police zaidi ya 100! Zikija Camera (AI) zinalamba wote hao!
Kwa kifupi tujiandae tu! Watu wengi wataendelea kukosa kazi, uzalishaji utaongezeka lakini pia kwa kuwa watu hawana kazi basi bidhaa zinazozalishwa zitakosa wateja kwa kuwa watu hawatakuwa na kipato; hapo ndipo itakuja shida.
 
Kwa kifupi tujiandae tu! Watu wengi wataendelea kukosa kazi, uzalishaji utaongezeka lakini pia kwa kuwa watu hawana kazi basi bidhaa zinazozalishwa zitakosa wateja kwa kuwa watu hawatakuwa na kipato; hapo ndipo itakuja shida.
HILI NALO NENO mkuu:

Nakunukuu.

"Kwa kifupi tujiandae tu! Watu wengi wataendelea kukosa kazi, uzalishaji utaongezeka lakini pia kwa kuwa watu hawana kazi basi bidhaa zinazozalishwa zitakosa wateja kwa kuwa watu hawatakuwa na kipato; hapo ndipo itakuja shida."
 
Hapo Bukoba tu watu walinyanyaswa na Makabaila! Hujasoma political economy au historia inayoelezea utumwa na jinsi watumwa walivyojikomboa toka kwenye makucha ya Makabaila?
Unyarubanja alioutokomeza Mwl Nyerere au? Nyerere alikuwa jabali kwelikweli, alimwambia Mzee Burito Nyerere kuwa Uchifu wako full stop, sasa taifa linachukuwa mwelekeo mpya wa kuondokana na Machifu.
 
Hapana lazima maisha yaendelee. Kama wanadamu walivuka kwenye great death ama black death aka Prague na pia viumbe hai walivuka kipindi Cha permian triasic extinction. Who will stop us?
Ndugu ficha ujinga wako halafu hebu tafuta taarifa za Tsar Bomba.
 
itoshe kwa kusema kwamba:, shida haikuwa Ardhi na bado dunia haijawa na shida ardhi. shida ili kuwa ni hofu yao dhidi ya wanyama wakali, wangeliondolewa/ondoa hofu yao dhana ya shida ya ardhi ingelibaki ni pumbao tu. hata new York ilikuwa ni pori ile wenyewe guts na risk takers wameibadili na kuwa maghorofa.
Ni kweli mkuu, ila nadhani siyo jambo la kufanyika overnight, ni mchakato mrefu kufikia hapo; ambao hauwezi kujibu mahitaji ya ardhi toshelevu kwa watu wote kwa wakati huo wa dharura ya mapinduzi ya Marxism. Mkuu, niruhusu nitumie reference ya Msahafu hivi:-

Kumbukumbu la Torati 7:22​

"Naye BWANA, Mungu wako, atayatupilia mbali mataifa yale mbele yako kidogo kidogo; haikupasi kuwaangamiza kwa mara moja, wasije wakaongezeka kwako wanyama wa mwitu"

Yaani wanyama wangekuwa wengi kuliko binadamu na kuanza kuwararua.

NB.
Ila umepresent vizuri sana.
 
Hii mada ni nzuri sana na inafikirisha sana hatima ya mwanada kipindi kijacho.
Kwa mwelekeo wa maisha na mwenendo wa maisha kwa sasa ni wazi huko mbele kazi ipo!

Serikali za dunia zinaendesha siasa na mambo yao kwa maslahi mapana ya wachache na maslahi duni kwa walio wengi.

Hii inatufikirisha sisi wazazi, ikiwa haya yanafanyika kipindi chetu hiki huko mbeleni watoto na wajukuu wetu watakuwepo katika hali gani?

Elimu inayotolewa huko shuleni kwa nyakati hizi imekua haina msaada kwa maisha yetu na ndio maana tunaona watu wengi waliomaliza elimu ya juu wakiwa wako mtaani hawana mbele wala nyuma na wala hawajui wafanye nini,zaidi ya kusubiria serikali na watu wengine wawape cha kufanya, hii maana yake hii elimu inayotolewa sio lolote wala chochote.


Cha kufanya kwa kua muda bado upo ni muhimu mno kuiangalia kesho kwa jicho makini sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom