Historia Fupi ya CHADEMA, Dr. Slaa na Wilaya ya Karatu

STEIN

JF-Expert Member
Aug 29, 2010
1,770
552
Ndugu zangu wana JF naomba niwaletee historia fupi ya Dr. Slaa na Chadema katika wilaya ya karatu tangu 1995 hadi leo hii.

Kwanza kabisa Karatu ni sehemu mambayo imekuwa na historia ya kipekee katika siasa za nchi hii na hii imetokana na ukweli kwamba jamii ya watu wengi walioko karatu wametoka katika wilaya Mbulu. Sehemu ambayo hata mwanzishi wa Taifa hili hataisahau kutokana na kumpinga Nyerere ambaye alikuwa aliataka Dodo awe Mbunge wa mbulu ile hali wananchi wanataka Sarwat ndo awe mbunge wao na hilo likafanikiwa kwani baada ya malumbano Nyerere alikubali Sarwat chaguo la wananchi awe mbunge .

Baada ya kuanza kwa vyama vingi vya siasa, na karatu kuwa jimbu la uchaguzi ndani ya wilaya ya mbulu, historia nyingine inakuja pale ambapo katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi kijiji cha Gongali ilipo msimamisha mgombea wa mwenyekiti wa kijiji kupitia Chadema mwaka 1994 na kushinda kwa kura nyingi sana na kuandika katika historia ya nchi kuwa kijiji cha kwanza kuongozwa na upinzani na ndio kijiji ambacho anaishi Dr. W.P.Slaa.

Mwaka 1995 watu wa karatu waliamua kumwondoa madarakani Mbuge wa wakati ule Patric Qorro ambeye alikuwa ni mbabe na asiyejali maendeleo ya wananchi wa Karatu kwa Kumwomba Dr Slaa kurudi nyumbani na kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM. Kwenye kura za maoni alimwacha Qorro kwa mbali sana lakini ccm kwa utawala wao wa kidicteta wakamwengua kule dodoma ndo wananchi walipo mwomba na kumtaka achukue fomu kupitia chadema ili agombee kuwa mbunge.

Ndipo Dr. Slaa alipokubali watu wakaunganisha nguvu zao dhidi ya Pesa za CCM na kumpigia kampeni Slaa akashinda kwa kishindo.

Kuanzia 1995 hadi 2000 Dr Slaa aliweza kutekeleza miradi ya maji hasa kwa vijiji vinavyozunguka wilaya ya karatu ila kwa taabu sana kwa kuwa viongozi wengi walikuwa wa CCM walikuwa hawamungi mkono lakini alipowaambia wananchi wakamwunga mkono na kuanza kuwabana viongozi wa wakati ule.

Kwenye uchaguzi wa 2000 Dr. Slaa aliwaomba wananchi wa karatu jambo maja tu wampe madiwani, hata kura yake hakuwa anaomba, ndipo walipompa madiwani 9 kati ya 12 na wakachukua halimasharuri na kuanza kutekeleza ilani ya chadema kwa karatu ikiwemo kupunguza kudi ya kichwa toka 5000 hadi 2000 ndipo CCM wakafuta kwa nchi nzima 2004. Vile kila diwani aliweza kuhamasisha wananhi kujenga Dispensary kila kijiji na Shule ya sekondari kila kata na kupanua huduma ya maji kwa kila kijiji na yote hayo yakafanikiwa ndani ya miaka mitano.

Mwaka 2005 Dr Slaa alikuwa na agenda ya kutafuta waalimu pamoja na madaktari na manesi, hilo nalo lilifanikiwa kwa kuhamasisha wananchi kushiriki kujenga nyumba za waalimu na madaktari na manesi kwani, kuwa mfanyakazi wa karatu ni dili kwa sababu unapata nyumba ya bure karibu na shule au hospitali/zahanati.
Na kwenye uchaguzi wa 2005 kazi yake ilikuwa ni kuhakikisha kuna shule za A-level/ Chuo ambazo hadi sasa zipo shule kama nne za A level, Chuo cha manesi na madaktari moja na Chuo kikuu kimoja ambacho kitachukua wanafunzi mwaka kesho.

Hadi sasa halmashauri ya wilaya ya karatu iko chini ya chadema na ina madiwani 10 kati ya 14, kwa hiyo wananchi wa karatu wanajivunia kuwa upinzani.

HITIMISHO:
Si vibaya kwa wabunge wengi wa upinza wakamwomba ushauri wa namna ya kujipanga ili uweze kutimiza majukumu yako vizuri kwa wananchi wako kwani amefanikiwa kwa mambo mengi.

Peoples Power Mabadiliko ya Katiba lazima



 
karatu ni moja ya sehemu zinazoheshimika sana katika historia ya vuguvugu la demokrasia nchini.
 
karatu ni moja ya sehemu zinazoheshimika sana katika historia ya vuguvugu la demokrasia nchini.

Wananchi wa karatu huwaambii kitu kuhusu chadema na hata sasa wana amini wakichagua chama kingine kitaharibu miundombinu iliyowekwa na chadema kupitia Dr. Slaa

Peoples Power
 
Yes, kuna kazi ya kufanya majimbo yote kuwa kama karatu kisiasa, kwani ni mfano
 
mimi pia najivunia kuwa chadema

Mimi najivunia kuwa mpinzani wa wabaya, mpenda mabadiliko, mtetea haki, mwanamapinduzi wa kweli, na mkweli.

kujivunia -uchama mwisho wake ni kuwa kama wana ccm , ukisukumwa huku unavutika, ukisukumwa huku unaenda!!!
 
Yes, people's power is a good weapon to fight dictatorship!!!!! Wananchi wa Karatu waliona mbali, na wananchi wengine Tanzania pia wanaona mbali wakati huu. Kwa hiyo wabunge wetu wa Chadema wanapaswa kufanya kazi nzuri ili upinzani usiwe tu lelemama na watu kushindwa kuona tofauti kati ya CCM na Chadema. Kama Wilaya ndogo na mpya kama Karatu inaweza ku-make a big statement like that, I am sure we can all make a great statement for the great good of our country....kama constitution, fair electorate Commission nk.
 
Yes, kuna kazi ya kufanya majimbo yote kuwa kama karatu kisiasa, kwani ni mfano

Mimi nafikiri kazi ya chadema sasa ni moja tu kuhakikisha viongozi wote walioshinda, walioshindwa, vijana, wazee na akina mama kuhimiza mabadiliko na kushiriki katika shughuli za jamii kwa pamoja.
Ila kuna changamoto kama wameanza kuizuia chadema kisifanye mikutano ya hadhara, itabidi hili swala lipelekwe mahakamani mara moja.
 
Mimi najivunia kuwa mpinzani wa wabaya, mpenda mabadiliko, mtetea haki, mwanamapinduzi wa kweli, na mkweli.

kujivunia -uchama mwisho wake ni kuwa kama wana ccm , ukisukumwa huku unavutika, ukisukumwa huku unaenda!!!

Nakubaliana na wewe maana hata Dr. Slaa kwenye kampeni zake kuna sehemu anawambia kabisa kwamba wakiwa madiwani wote chadema itakuwa tatizo maana wataleta uchama wakati wamechaguliwa na watu kutoka vyama tofauti.

Kwa hiyo yeye anachowaambia watu wa karatu ni kuchanganya ila halmashauri iwe Chadema. Kwa hili watu wanamsifu sana na kumkubali.
 
kUPIUNGWA, KUHUJUMIWA na KUPUUZWA kumewafanya watu wa Karatu waikifu ka bisa CCM. Ndivyo itakavyokuwa kwa majimbo mengine mengi ambako CCM wanawadhalilisha wananchi kwa l.engo la kuwaonyesha ubabe wao, lakini in return itakula kwao kote huko.
 
...Maendeleo ya sehemu yeyote duniani huletwa na jamii. Kinachohitajika cha zaidi ni leadership.

...Tatizo la Tanzania si serikali kutopeleka/fanya maendeleo sehemu hii au ile, bali ni ukosefu wa leadership na uelewa mdogo wa wananchi, kwamba wao ndio wameshika hatamu za maendeleo yao.
 
...Maendeleo ya sehemu yeyote duniani huletwa na jamii. Kinachohitajika cha zaidi ni leadership.

...Tatizo la Tanzania si serikali kutopeleka/fanya maendeleo sehemu hii au ile, bali ni ukosefu wa leadership na uelewa mdogo wa wananchi, kwamba wao ndio wameshika hatamu za maendeleo yao.

Issue kubwa hapa ni tunatakiwa tupate chama ambacho kina sera nzuri za kuwa aminisha waTZ kwamba kama elimu itakuwa bure maana yake watu engi wataelewa mambo mengi ya afya kwa hiyo hawataugua, wataweza kujitafutia chakula wenyewe na kujenga makazi bora hatimaya baada ya miaka mitano hadi kumi Wzara ya Afya itakuwa na bajeti ndogo kuliko zote.

Maana sasa kwa hali tuliyofikia hata watanzania wanafika mahali wanaona kuwa masiki, kuishi makazi duni ni kama mpango wa mungu ile hali si kweli.
 
Huyu Qorro alipokumbushiwa tatizo la maji akasema sio shughuli yake yeye wala si yeye aloleta tatizo la maji na kwamba watu hawalaimishwi kuishi Kartu isiyo na amaji wanaweza kuhamia sehemu nyiongine au wakojolee ndoo zao kupata maji zaidi....jeuri yake ni uswahiba na Ben...kwa kauli hiyo alimtosa kabisa sasa hivi yuko hoi kimaisha...tunapanda nae Mwaibula
 
Issue kubwa hapa ni tunatakiwa tupate chama ambacho kina sera nzuri za kuwa aminisha waTZ kwamba kama elimu itakuwa bure maana yake watu engi wataelewa mambo mengi ya afya kwa hiyo hawataugua, wataweza kujitafutia chakula wenyewe na kujenga makazi bora hatimaya baada ya miaka mitano hadi kumi Wzara ya Afya itakuwa na bajeti ndogo kuliko zote.

Maana sasa kwa hali tuliyofikia hata watanzania wanafika mahali wanaona kuwa masiki, kuishi makazi duni ni kama mpango wa mungu ile hali si kweli.

...Stein, usiwe na wasi. Watanzania washaanza kuelimika bila hata kwenda darasani na kupata elimu ya bure. Matatizo yanayowakabili ni shule tosha!

...Vile vile, uozo wa uongozi, ubinafsi na uzembe uliopo kwenye kila ngazi ya utendaji unawafumbua macho na kuwapa moyo wa kujiletea mabadiliko katika jamii zao. Hiki ndio kitu cha muhimu kuliko hata kupewa elimu na afya bure. Ukombozi wa mtu huanzia kwenye fikra!
 
...Maendeleo ya sehemu yeyote duniani huletwa na jamii. Kinachohitajika cha zaidi ni leadership.

...Tatizo la Tanzania si serikali kutopeleka/fanya maendeleo sehemu hii au ile, bali ni ukosefu wa leadership na uelewa mdogo wa wananchi, kwamba wao ndio wameshika hatamu za maendeleo yao.

Hakika mkuu uko sahihi, leadership na wananch wenyewe ndio matatizo ya nchi hii, kwani viongozi wetu hawajui maana ya uongozi na kuongoza, na hata wakati mwingine wanafumba machoma nakwenda kinyume na maadili ya uongozi hata kama wanayafahamu.

Wananchi nao hawako tayari kutumia sanduku la kura kuwatia adabu, wanaridhika na rushwa za elfu tano wanampa mtu uongozi kwa miaka mitano (yaani kila mwaka 1000). Nafikiri tuendelee kuamshana tu hadi wote tuamke na ndipo patakapo chimbika kwelikweli
 
Huyu Qorro alipokumbushiwa tatizo la maji akasema sio shughuli yake yeye wala si yeye aloleta tatizo la maji na kwamba watu hawalaimishwi kuishi Kartu isiyo na amaji wanaweza kuhamia sehemu nyiongine au wakojolee ndoo zao kupata maji zaidi....jeuri yake ni uswahiba na Ben...kwa kauli hiyo alimtosa kabisa sasa hivi yuko hoi kimaisha...tunapanda nae Mwaibula

Na katika kijiji kingine walipokuwa wadai maji na mengine akawaambia watu" "ninyi watu wa ....vichwa vyenu vigumu kama hayo mawe yenu.."Hicho kijiji kilikuwa na mawe mengi. Then wakamwambia kama sisi tuna vichwa vigumu basi tutaonana wakati wa uchaguzi, akafikiri wanatania. Na kwa kuwa alikuwa na back up kubwa ya CCM, alijua kuwa he was unshakeable; only to be proven wrong when opposition won. Hakuamini masikio wala macho yake!!!! That is how it should be elsewhere where people's wishes are taken for granted
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom