Historia(2/7/2015) Sinema Bungeni: CCM wapitisha kibabe sheria ya mafuta na Gesi

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,171
103,637
Ndugu mwanaJamiiforums leo tunakuletea sinema jinsi 2/7/2015 Chama cha Mapinduzi CCM kilivyopitisha kibabe sharia ya mafuta na gesi pale bungeni.

Ubabe huo ulipigwa na kambi rasmi ya upinzani ikiongozwa na Mbunge John John Mnyika akiwa Mbunge wa Ubungo. Mnyika alipinga kwa kutumia kanuni za bunge uwasilishwaji wa hati ya dharura. Lakini mwisho ikawa ''Wanaoafiki waseme ndio,.........Wasioafiki waseme sio.............Walioafiki wakashinda. Ikumbukwe kuwa Rais Magufuli alikuwa sehemu ya baraza la mawaziri na sehemu ya bunge akiunga mkono mambo haya. Kama ''Waziri'' Magufuli angekataa huu wizi toka mwanzo kama walivyokataa kina Zitto, Lissu, Mnyika nk labda pengine tusingekuwa tumeibiwa kiasi hiki.

Pamoja na kuwa haya yamepita lakini yanatupa funzo kwamba hata huu ubabe wanaofanyiwa wapinzani wanaohoji MV Bagamoyo, Bombadia na Chato International Airport yatakuja kutufikisha kuundia makamati.

 
Back
Top Bottom