Hili tatizo ambalo kila uchao / siku naona linazidi tu kukua na kuota mizizi lawama natupia Vyuo Vikuu vyetu nchini

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,871
Nimegundua ya kwamba 85% ya Wasomi wa Tanzania na hasa ambao wanafanya Kazi Serikalini au ni Watumishi wa Serikali wana tatizo kubwa sana ' Public Speaking ' na wana Kiwango cha chini mno cha ' Confidence ' mbele ya Wakubwa wao hali ambayo inashangaza na kusikitisha mno.

Haiingii akilini kabisa unakuta Mtu ni Bosi fulani katika ngazi ya Kiserikali lakini akipewa wasaa wa Kuzungumza na ' hadhira ' husika au hata tu Kujieleza utaona anajiumauma, anababaika na kutetemeka mno hali ambayo imenifanya nijiulize maswali mengi kwamba ina maana huko Vyuo walikopita walikuwa hawana ' debating classes ' ili ziweze kuwajenga na kuwapika vyema hasa katika ' Public Speaking ' na kuwa na ' Confidence ' ya kutosha.

Kwa jinsi wanavyotetemeka na kubabaika huku wakijiumauma naogopa katika Kuongea / Kujieleza kuna Siku Mtu ( Kiongozi ) tutashuhudia ama Kiongozi fulani anajikojolea mbele au anajinyea / anaukweka mbele ya hadhira kwa hofu kubwa mbele ya Watu.

Nitoe RAI kwa Vyuo Vikuu nchini Tanzania tafadhalini hebu lifanyieni Kazi hili tatizo kwani sasa linazoeleka halafu linakera pia kwa Watu ambao ni makini. Haiwezekani Mtoto wa Shule ya Msingi tu wa nchini Kenya na Uganda anaweza Kuongea mbele ya ' hadhira / umma ' bila Uwoga / Hofu lakini unalikuta Jitu Zima / Zee Zima lina Cheo katika Halmashauri au Manispaa au Wizara au Kurugenzi au Wilaya au Mkoa halafu akipewa ' mic ' na Mkuu au Mteule wake anabaki ' Kujambajamba ' tu pale mbele japo bahati nzuri ' ushuzi ' wake huwa haunuki.

Wasomi badilikeni katika hili kwani linatudhalilisha na kuwafanya majirani zetu watucheke na waidharau hadi Elimu yetu hii.

Nawasilisha.
 
Mpaka wanyooke walikua wamepinda Sana

Wewe tayari una Cheo / Madaraka huku ukiwa una Hela na fursa zingine nyingi tu tofauti na walizonazo wengine halafu akiitwa tu mbele Kuongea au akipewa Kipaza Sauti ( Microphone ) utaona anavyoanza Kutetemeka na kupatwa na Kizunguzungu cha ghafla. Ni tatizo ambalo bahati mbaya sana naona Watanzania tunalipuuza ila linatuharibia na kutudhalilisha mno Mtu kwani Kisaikolojia tu kama Mtu akiwa hajiamini katika Kuzungumza na anababaika ni jibu tosha kuwa hata Kichwani hakuna Kitu cha maana zaidi ya ' Maji ' tu yasiyo na faida na ambayo pengine nayo yanatafuta njia ya kutokea.
 
Zipo sababu nyingi
1, Asili ya mtu kuwa na uwonga mbele ya umati
2.Ukilaza
3.Hofu ya kutumbuliwa(utawala huu ulijenga hofu kubwa sana kwa watumishi baada ya kutumbia watumishi kwa kasi ya standard gauge,hasa miaka miwili ya mwanzo)
4 Ukosefu wa elimu na ujuzi wa kuongea mbele ya umati( hii ndio point ya mleta mada)
 
Mnapo ambiwa elimu inakuandaa kuwa mtumwa usipojanjaruka mapema huwa mnadhani mtu kajiropokea tu!! freedom of mind and positive Attitude is everything! We huna freedom of mind hiyo confidence utaitolea wapi!!

Tofauti na hapo huko vyuoni wakati wa presentation mwanafunzi anaandaa power point kama Kitabu halafu anafika anakisomaaa akimaliza eti anapewa maksi, sasa najiuliza sijui hiyo ni presentation au kusoma kwa sauti!!!

Cha msingi confidence huja kwa kujitambua kiundani zaidi na kukubaliana na hali yako halisi!! We mtu tokea ulipokuwa chuo ulikuwa hujitambui vema what next kama siyo haya yanayotokea, mkuu uhalisia wako usipoufanyia kazi wewe mwenyewe kujibadilisha hakuna kitu kitakachokibadilisha!!!

Mambo mengine tunayazungumza humu ili hali walioko vyuoni wanashuhudia, tupo nao kibao kule chuo mkuu!!

Kama hujielewi principle ya nature never expect miracle mzee!! Highly self determination is everything!! Na hii ndo hutofautisha success na failure!!

Asije mtu kukutishia mara masters, PhD na degree wakati uhalisia unajulikana!! Watu tuache kuishi kimazoea!!!!
 
Hapo vyuo havihusiki ni malezi tu ya watu waliokulia maana hata kwenye presentation tu chuo watu wanaingia mitini hapo bado hujazungumzia zile debate za secondary watu walikua wanaona ni kujichora. Watoto wa siku hizi hata akiwa class one unaona kabisa confidence.
 
Mtoa mada na wewe pia jifunze mbinu za uwasilishaji wa mada yako kwa lugha ya hekima siyo kutamkatamka tu maneno!! Au unawaponda wenzako we hujioni??!!!
 
Nimekumbuka kuna jamaa alileta vyeti na transcript yake wakati anatafuta ajira, niliona pale st john wanafundisha hadi Debating & Public speaking yani somo kabisa eti unasoma miezi mi4! kumbe umuhimu upo
 
Back
Top Bottom