Hili suala la wanawake kuvaa nguo fupi halafu wakianza kutembea/kukaa wanapata tabu, mnakera sana.

Mwifwa

JF-Expert Member
Apr 3, 2017
46,918
122,175
Kichwa cha uzi kinajieleza.

Huu mtindo wa wanawake hasa wanaoishi mjini wa kuvaa nguo/sketi fupi zinazoishia magotini au juu ya magoti halafu wakiwa wanatembea utawaona wanajishika shika hiyo sketi fupi na kuivuta chini ili ifunike vizuri magoti ilihali ni fupi na mwenyewe anajua ni fupi jambo ambalo anajua kabisa haliwezekani ila anafanya tu ama kwa kuona aibu akiangaliwa/akikudolewa macho na mtu mwingine hasa wanaume, mnakera sanaaa.

Mwanamke aliyevaa hiyo sketi fupi akitaka kukaa, sketi inajivua na kurudi nyuma huku ikiacha sehemu yote ya magoti ikiwa wazi hadi mapajani na hapo utamuona anachukua kamkoba kake alichokuwa nacho na kukiweka mapajani hasa kwenye sehemu anayoona iko wazi ili afunike, mnajisumbua na kuhangaika hivyo ilihali unauwezo wa kuvaa nguo zenye kukusitiri vizuri, mnakera sanaaa, mtapata tabu sanaaa maana wanaume rijali lazima wapige chabo kwa kwenda mbeleee

Wengine unakuta hawajafunga kufuli halafu anajisahau anapokaa ama akiwa anapiga stori na mwenzio au akiwa busy kuperuzi hapa JF kufuatilia habari za hapa na pale ama MMU au ana chit-chatika, ukipiga jiko hadi unaona aibu, mnakera sanaa, mtapata taabu sana kupigwa chaboo na marijali.

Badilikeni bana, vaeni nguo za heshima zenye kusitiri mwili vizuri ili iwe kioo kwenye jamii na kukuza maadili mema hasa kwa watoto wadogo ambao wanakua maana mtoto anatabia kuiga kitu/tabia anayoina na kuifuta kadri anavyoendelea kukua.
 
Kichwa cha uzi kinajieleza.

Huu mtindo wa wanawake hasa wanaoishi mjini wa kuvaa nguo/sketi fupi zinazoishia magotini au juu ya magoti halafu wakiwa wanatembea utawaona wanajishika shika hiyo sketi fupi na kuivuta chini ili ifunike vizuri magoti ilihali ni fupi na mwenyewe anajua ni fupi jambo ambalo anajua kabisa haliwezekani ila anafanya tu ama kwa kuona aibu akiangaliwa/akikudolewa macho na mtu mwingine hasa wanaume, mnakera sanaaa.

Mwanamke aliyevaa hiyo sketi fupi akitaka kukaa, sketi inajivua na kurudi nyuma huku ikiacha sehemu yote ya magoti ikiwa wazi hadi mapajani na hapo utamuona anachukua kamkoba kake alichokuwa nacho na kukiweka mapajani hasa kwenye sehemu anayoona iko wazi ili afunike, mnajisumbua na kuhangaika hivyo ilihali unauwezo wa kuvaa nguo zenye kukusitiri vizuri, mnakera sanaaa, mtapata tabu sanaaa maana wanaume rijali lazima wapige chabo kwa kwenda mbeleee

Wengine unakuta hawajafunga kufuli halafu anajisahau anapokaa ama akiwa anapiga stori na mwenzio au akiwa busy kuperuzi hapa JF kufuatilia habari za hapa na pale ama MMU au ana chit-chatika, ukipiga jiko hadi unaona aibu, mnakera sanaa, mtapata taabu sana kupigwa chaboo na marijali.

Badilikeni bana, vaeni nguo za heshima zenye kusitiri mwili vizuri ili iwe kioo kwenye jamii na kukuza maadili mema hasa kwa watoto wadogo ambao wanakua maana mtoto anatabia kuiga kitu/tabia anayoina na kuifuta kadri anavyoendelea kukua.
Uzungu babu weeee wasipo vaa vimini utawaonaje kua ni wamjini .......heri yangu mie nanjilinji huku najivalia madera safi tu .....hizo kero za kutembea na kukaa kwa karaha siziwezi kwa kweli
 
Na ieleweke kwamba

Kuniburudisha siyo dhambi.

Mimi kula kwa macho siyo dhambi.

Wewe kunitumia nudes siyo dhambi.

Tafadhali waache.
 
Mi juzi nilimwacha mmoja kituoni baada ya kushindwa kunyanyua mguu aingie kwenye gari maana nilisimama sehemu isiyo halali nikaona nasababisha foleni bila sababu nikamwambia funga mlango kwanza nipaki vizuri akafunga huwezi amini nilisogea mbele kidogo nikanyoosha zangu moja kwa moja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom