Hili neno ‘Ubeberu’ linatujengea unyonge wa kifikra, ni bora tukatumia maneno mengine

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1576821260099.png
Acknowldgement;

Mada hii imechangiwa na mawazo ya wana jf kadhaa akiwemo FaizaFoxy na wenzake ambao washawahi kuyatoa huko nyuma katika nyakati na mazingira tofauti tofauti.
===============

Beberu “Mbuzi dume aliyekomaa”. Sina uhakika kama walioita nchi zilizoendelea kiuchumi jina hili walifikiri kwa kina, na kama walifikiri kwa kina ni vigumu kuelewa walilenga nini kuwaita jina hili.

Hivi siku mzungu akakusikia unamuita beberu, akakuuliza, what is the meaning of “Beberu” ?utamuauambia “Matured male goat”? akikuuliza “Why you call us “Matured male goats? And if we are matured male goat, what we may call you?” utajibu nini?

Kumbuka kila kitu kina kinyume chake, unapomchagulia mtu jina anaweza pia kukuchagulia jina na wakati mwingine hata asipokuchagulia jina, unaweza kujichagulia mwenyewe bila kukusudia na pengina bila kujua.

Ni sawa na unawaambia watu 'yule jamaa tunalingana kimri ila yeye ni kijogoo'. Au unasema 'huyu mtu tulisoma naye ila yeye ana akili', au unasema 'sote wanaume ila huyu yeye ana nguvu' au unasema 'huyu jamaa ni mwamba' n.k ijapokuwa unakuwa unamwelezea yeye; bila kukusudia pia unakuwa unajielezea wewe.

Nashauri hii lugha ya mabeberu ni bora tukaangalia kama inafaa kuiacha. Lugha hii inatuathiri zaidi sisi tunaoitumia kuliko wale tunaowaita. Inatujengea unyonge usio wa lazima. Nashauri ni bora tu kuwaita 'nchi zilizoendelea kiuchumi…….. (kisha unaendelea unachotaka kusema)'

Ila atakayeona ushauri huu si sahihi, anaweza kuendelea kuwaita mabeberu ila ajue wakati anafanya hivyo, anasababisha mambo mengine mawili bila kukusudia; Kwanza na yeye anakuwa anajiweka kwenye kundi fulani bila kukusudia wala kutamka na pia kujijengea unyonge wa kifikra. Ni ushauri tu ndugu zangu.
 
Mimi nahitimisha kwa kusema mleta Mada ni Beberu pia

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni sawa na unasema 'natangaza vita na beberu' Unaweza kuwa na nia nzuri na pengine vita hiyo ni nzuri na muhimu, lakini neno 'Beberu' lina maana chanya kwenye lugha ya kiswahili. Ni sawa na 'Jogoo' Sasa unakuta tunatangaza vita kwa kuanza kumsifu (bila kujua na pengine bila kukusudia) tunayedhani ni adui.

Hicho ndicho ninachojaribu kusema.

Kuhusu hilo la kwamba mimi beberu, kama wewe umejiridhisha na hilo sawa! hahahha
 
Ikimbukwe, mfumo wetu wa kufikiri unajenga na vile tunavyosikia, kuona, kusoma au kufanya mara kwa mara.
 
Back
Top Bottom