Hili Ndio Jeshi Letu

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Unapoenda sehemu yoyote labda kwa uzuri na ubaya na ukifanikiwa kutoka eneo hilo ukiwa salama basi unashukuru sana , lakini hautakiwi uache mambo yale nyuma , kama mambo hayo ni zawadi kwa binadamu wengine hakuna budi kuyahadithia kwa watu wengine ili wapate kujifunza mengi ya dunia na hata serikali husika ipate muda wa kuweza kujua jinsi baadhi ya watendaji walivyo .

Nami nilipata changamoto nyingi kujifunza hapo mahabusu kutoka kwa wale wengine waliomo mule ndani na kutoka kwa polisi wengine hadithi walizokuwa wanapigiana na mikasa mingine mbali mbali .

Kuna jamaa mmoja aliletwa kule ndani kwa kosa la wizi wa simu pale stendi ya mabasi mwenge , huyu kijana aliiba simu na kumrushia mwenzake ambaye alikimbia na hiyo simu watu wakaanza kumpiga lakini vibaka wenzake walikuja kumuokoa na kumpeleka polisi ambako ndio alikuwa salama .

Asubuhi hiyo jamaa mmoja ambaye inasemekana ndio mkuu wa kituo cha mwenge bosi wa wale vibaka alikuja kumtolea dhamana atoke , kabla ya yote hayo , yule kibaka akaomba dawa yaani madawa ya kulevya , polisi mmoja akamwambia asubiri kidogo .

Ghafla polisi akaja na unga sikujua ule unga ni aina gani , lakini akampa yule kibaka atumie , kibaka hakuridhika akaomba tena aletewe bangi na moto ili achanganye hizo dawa za kulevya na ile bangi yake .

Kweli polisi yule alienda officini kwake na kumpa mambo yote hayo ndio kijana yule akaanza kuwa na nguvu na kuanza kuwa na furaha kufanya na kuongea mambo yake .

Jiulize madawa ya kulevya yanafanya nini kituo cha polisi , bangi zinafanya nini kituo cha polisi ? inawezekana kuna watu wengine wanakuja pale wanawekewa mifukoni ili baadaye watolewe pesa kwa urahisi zaidi .

HII NDIO NCHI YETU BWANA , YAANI WALE WATU TUNAOWATEGEMEA WAWE WATIIFU NA WAADILIFU KULIKO WOTE NDIO WAKO TOFAUTI KULIKO WENGINE NA NDIO WANAONGOZA KATIKA MAMBO MENGINE YASIYOPENDEZA KWA JAMII

HILI NDIO JESHI LETU
 
Asubuhi hiyo jamaa mmoja ambaye inasemekana ndio mkuu wa kituo cha mwenge bosi wa wale vibaka alikuja kumtolea dhamana atoke , kabla ya yote hayo , yule kibaka akaomba dawa yaani madawa ya kulevya , polisi mmoja akamwambia asubiri kidogo .

Ghafla polisi akaja na unga sikujua ule unga ni aina gani , lakini akampa yule kibaka atumie , kibaka hakuridhika akaomba tena aletewe bangi na moto ili achanganye hizo dawa za kulevya na ile bangi yake .

Kweli polisi yule alienda officini kwake na kumpa mambo yote hayo ndio kijana yule akaanza kuwa na nguvu na kuanza kuwa na furaha kufanya na kuongea mambo yake .

Polisi alipokuja na unga alilipwa kiasi gani? (Kama sio mkuu mwenyewe aidha alimtuma kachero). Je kulikuwa na uhusiano gani kati ya mwombaji unga na polisi (Kachero) aliyeleta unga? Walikuwa wanafahamiana na huyu polisi au ni mwenyewe mkuu wa kituo? Je huyo polisi (mkuu wa kituo I presume) alichukua hivyo vitu ofisini kwake? Unaweza kuweka vielelezo vya siku na tarehe haya yalipotokea n.k.
 
"HII NDIO NCHI YETU BWANA , YAANI WALE WATU TUNAOWATEGEMEA WAWE WATIIFU NA WAADILIFU KULIKO WOTE NDIO WAKO TOFAUTI KULIKO WENGINE NA NDIO WANAONGOZA KATIKA MAMBO MENGINE YASIYOPENDEZA KWA JAMII

HILI NDIO JESHI LETU"

Shy, ulifanya nini juu ya hilo kama raia mwema?
 
Hii sio habari ya Udaku, this is purely about corruption within the police force. Kama watu wanawaserve vibaka unategemea polisi watawafanya nini? May be polisi wengi zadi wako kwenye payroll ya vibaka.
 
Shy mbona hujajibu niliyouliza kwenye post number mbili? Where are you?
 
Polisi alipokuja na unga alilipwa kiasi gani? (Kama sio mkuu mwenyewe aidha alimtuma kachero). Je kulikuwa na uhusiano gani kati ya mwombaji unga na polisi (Kachero) aliyeleta unga? Walikuwa wanafahamiana na huyu polisi au ni mwenyewe mkuu wa kituo? Je huyo polisi (mkuu wa kituo I presume) alichukua hivyo vitu ofisini kwake? Unaweza kuweka vielelezo vya siku na tarehe haya yalipotokea n.k.

Thread Imeshaharibika kwa kuwa imeshaitwa Udaku sioni sababu zozote za kuendeleza mada

Tuendelee na maisha
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom