Hili ndilo limbwata la kumteka mwanaume

ILI KUMTEKA MUMEO FANYA HAYA

1. Muite kwa jina lake la utani, jina lile analolipenda sana.

2. Muache atumie mamlaka yake kama
kichwa cha nyumba.

3. Usimcheke akiwa ameumizwa na
jambo fulani.

4. Kaa kimya pale anapokuwa na hasira.
Unaweza ukaenda kumuomba msamaha
na kumueleza kwanini ulimkosea pale
hasira zinapokua zimemuisha.

5. Kuwa na haraka ya kuomba msamaha
pale unapokosea, sisitiza juu ya msamaha na mbusu pale anapokusamehe.

6. Ongelea mazuri yake na yeye kabla
ndugu, jamaa na marafiki hawajafanya
hivyo.

7. Waheshimu wazazi wake. 8. Msisitize kuhusu kwenda kuwasalimia wazazi wake na kuwapelekea chochote. Na afanye hvyo na kwa wazazi wako pia.

9. Msuprise kwa chakula akipendacho,
hasa kipindi kile anapokuwa na msongo
wa mawazo. Na kamwe usimcheleweshee chakula chake.

10. Usiruhusu dada wa kazi amhudumie
chakula mume wako ukiwa nyumbani.

11. Mkaribishe kwa kumkumbatia
anapotoka kwenye mihangaiko yake,Msaidie mizigo aliyokuja nayo au hata begi.

12. Tabasamu pale unapomtizama, vaa
vizuri na jipendezeshe pale mnapotoka
wote kwenda kwenye warsha mbalimbali.

13. Mpigie simu na umwambie kwamba
unampenda na umemkumbuka

14. Muamshe asubuhi na umpe romance
kiasi kwamba ifike hatua ya kuhitaji, mpe
na hata jishughulisha na wanawake
wengine siku hiyo.

15. Kamwe usithubutu kutamka kuwa
hakuridhishi na tendo la ndoa. Tafuta njia muafaka ya kufikisha ujumbe wako.

16. Mwambie ni kiasi gani una bahati
kuwa nae kama mume wako.

17. Mkumbatie tu bila sababu yoyote ile.

18. Mshukuru Mungu kwa kukupa Adamu
wako katika maisha yako.

19. Kumbuka kumuombea na kumkabidhi
mikononi mwa Mungu.

20. Tengenezeni utaratibu wa familia
nzima kumshukuru Mungu kwa pamoja
kila asubuhi na usiku kabla ya kulala.
Mungu abariki ndoa yako.

Copied from
Didas Tumaini
Jf member
Umewahi kuyatekeleza haya au unashauri tu.
 
22. Marufuku kuhoji chochote kinachomhusu mumeo, hata akikurudia asubuhi mpokee kwa mabusu motomoto, ukigundua ana kamchepuko huruhusiwi kukasirika sanasana mtie moyo kuwa unaelewa kwa nini anachepuka na umuombe radhi kwa kufuatilia maisha yake binafsi.
Niendelee?
This is real limbwata now hata kama usipofanya ayo mengine
 
Mimi sitekwi kirahisi hivyo.
Ukweli mtupu

Ila haters watasema limbwata la kumteka mwanamke ni kumpa pesa
sasa kwan nyie wanawake mnataka nn zaid ya pesa??
Vingi tu
A dick
A hug
Care
Understanding
Itaendelea.....
I'd be that 'hater'
We uliyeleta hii mada unayafanya yote hayo......mie nipikie chakula kizuri tu nitadata kwako sina mbwembwe nyingi sana
 
Mkuu unawajua wanaume au unawasikia?
Unaweza kufanya yote alafu tukaenda kuchepuka na mtoto wa jangwani sec. Apo ndio utajua kwanini tuna ndevu
 
Unamfanyia hivyo mwenye shukrani, hawa pasua kichwa tunapasuana tu.
 
22. Marufuku kuhoji chochote kinachomhusu mumeo, hata akikurudia asubuhi mpokee kwa mabusu motomoto, ukigundua ana kamchepuko huruhusiwi kukasirika sanasana mtie moyo kuwa unaelewa kwa nini anachepuka na umuombe radhi kwa kufuatilia maisha yake binafsi.
Niendelee?
Hhhhhh
unataka watu watengeneze sumu ndani ya miili yaoo...!!!!
 
Back
Top Bottom