Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Inaelezwa kwamba kuna uhusiano kati ya wanawake waliofanikiwa kwenye ajira kwa kuwa na kipato kikubwa zaidi ya waume zao na talaka. Labda nisema tu kwamba, binafsi sikubaliani na jambo hilo. Sikubaliana na dhana hiyo kwa sababu kuna idadi kubwa tu tena ya kutosha ya wanawake waliofanikiwa kwenye ajira zao kwa kuwa na kipato kikubwa zaidi ya waume zao lakini ndoa zao zimeendelea kuwa na Amani, imara na furaha tele.
Kama zipo ndoa ambazo zimetikiswa kwa sababu ya mke kumzidi mume kwa kipato, nafikiri sababu haitakuwa ni mume kuzidiwa kwa kipato, bali kuna jambo lingine ambalo wengi tunashindwa kuling'amua , inawezekana kwa makusudi au kwa kutojua. Kuna swala la kutojiamini ambalo ni tatizo linalowakabili wanandoa wengi. Kama ikitokea mume au mke ana tatizo la kutojiamini katika ndoa, basi ni vigumu kwa ndoa hiyo kuwa na amani.
Hebu chukulia kwamba, mwanamke ndiye anayefanya kazi na mwanaume hana shughuli ya kumuingizia kipato. Mwanamke huyu anaporejea jioni kutoka kazini anakuta nyumba ni kama jalala. Vitu vimetupwa huku na kule, mwanaume pengine kalala kwenye makochi, huku TV inakoroma. Lakini, kando kuna chupa mbili tatu za pombe. Hebu niambie, hapo mwanamke afanye kitu gani? Ni lazima atazungumzia kukerwa na hali ile. Kwa kutojiamini kwake, mwanaume ataanza kusema, mwanamke anamnyanyasa kwa sababu ya kazi yake au cheo chake.
Hivi hapo kuna uhusiano gani kati ya ajira au cheo na kauli au madai hayo ya mwanaume kwamba, anaonewa. Hapa kuna mtu kushindwa kukua. Mwanaume hapa anashindwa kukua na kuwajibika kwa maisha yake. Kama mwanaume hana shughuli na bado anashindwa hata kupanga vitu nyumbani na bado anaamini kwamba kunywa pombe ndiyo suluhu kwa matatizo yake ya kukosa ajira, inahusiana vipi na mke kumnyanyasa mume?
Kama mume hana shughuli ya kumuingizia kipato au anayo lakini ina kipato kidogo ukilinganisha na kipato cha mwanamke, lakini mume huyo anajitahidi kupata shughuli itakayolipa zaidi, ni vigumu mwanamke kumzonga. Kama ikitokea mwanamke kumzonga, hapo ndipo naweza kusema, mwanamke ana matatizo. Kwa hiyo tatizo hapa ni kukua, yaani mwanamke au mwanaume anaposhindwa kukua, ndipo matatizo kama hayo ya kuoneshana ubabe na ujuaji kati yao yanapojitokeza. Kwa hiyo siyo suala la mwanamke kuwa nacho zaidi ya mwanaume.
Lakini pia labda niseme tu kwamba, kuna suala la malezi, kwa nini kuna baadhi ya wanawake wanapopata fedha wanaamini kwamba hawana sababu ya kuwajali waume zao? Hapa kuna suala la malezi. Je mwanamke huyo aliaminishwa nini juu ya fedha? Kwa hiyo siyo kila mwanamke aliyesoma sana au ambaye ana kipato kuliko mume, anakuwa mkorofi, hapana. Kuna wakati ni kweli na kuna wakati siyo kweli. Na mara nyingi wanawake wenye tabia hizo ni wachache sana na ni wale walioathiriwa na malezi.
Kama zipo ndoa ambazo zimetikiswa kwa sababu ya mke kumzidi mume kwa kipato, nafikiri sababu haitakuwa ni mume kuzidiwa kwa kipato, bali kuna jambo lingine ambalo wengi tunashindwa kuling'amua , inawezekana kwa makusudi au kwa kutojua. Kuna swala la kutojiamini ambalo ni tatizo linalowakabili wanandoa wengi. Kama ikitokea mume au mke ana tatizo la kutojiamini katika ndoa, basi ni vigumu kwa ndoa hiyo kuwa na amani.
Hebu chukulia kwamba, mwanamke ndiye anayefanya kazi na mwanaume hana shughuli ya kumuingizia kipato. Mwanamke huyu anaporejea jioni kutoka kazini anakuta nyumba ni kama jalala. Vitu vimetupwa huku na kule, mwanaume pengine kalala kwenye makochi, huku TV inakoroma. Lakini, kando kuna chupa mbili tatu za pombe. Hebu niambie, hapo mwanamke afanye kitu gani? Ni lazima atazungumzia kukerwa na hali ile. Kwa kutojiamini kwake, mwanaume ataanza kusema, mwanamke anamnyanyasa kwa sababu ya kazi yake au cheo chake.
Hivi hapo kuna uhusiano gani kati ya ajira au cheo na kauli au madai hayo ya mwanaume kwamba, anaonewa. Hapa kuna mtu kushindwa kukua. Mwanaume hapa anashindwa kukua na kuwajibika kwa maisha yake. Kama mwanaume hana shughuli na bado anashindwa hata kupanga vitu nyumbani na bado anaamini kwamba kunywa pombe ndiyo suluhu kwa matatizo yake ya kukosa ajira, inahusiana vipi na mke kumnyanyasa mume?
Kama mume hana shughuli ya kumuingizia kipato au anayo lakini ina kipato kidogo ukilinganisha na kipato cha mwanamke, lakini mume huyo anajitahidi kupata shughuli itakayolipa zaidi, ni vigumu mwanamke kumzonga. Kama ikitokea mwanamke kumzonga, hapo ndipo naweza kusema, mwanamke ana matatizo. Kwa hiyo tatizo hapa ni kukua, yaani mwanamke au mwanaume anaposhindwa kukua, ndipo matatizo kama hayo ya kuoneshana ubabe na ujuaji kati yao yanapojitokeza. Kwa hiyo siyo suala la mwanamke kuwa nacho zaidi ya mwanaume.
Lakini pia labda niseme tu kwamba, kuna suala la malezi, kwa nini kuna baadhi ya wanawake wanapopata fedha wanaamini kwamba hawana sababu ya kuwajali waume zao? Hapa kuna suala la malezi. Je mwanamke huyo aliaminishwa nini juu ya fedha? Kwa hiyo siyo kila mwanamke aliyesoma sana au ambaye ana kipato kuliko mume, anakuwa mkorofi, hapana. Kuna wakati ni kweli na kuna wakati siyo kweli. Na mara nyingi wanawake wenye tabia hizo ni wachache sana na ni wale walioathiriwa na malezi.