Hili nalo halionekani tatizo kwenye Chama...

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Naamini wapo watakaoona nakiandama Chadema lakini ninayayazungumza humu wakiyachukulia kama changamoto yatawasaidia sana kujenga chama kikawa cha "demokrasia" na maendeleo kwa muonekano chanya. Nimefikiria sana haya maneno yanayorushwa kuwa pale Chadema kuna suala la kujuana na kubatizwa kuwa chama cha kifamilia. Nitatoa mfano hai.

1. Ndesamburo yeye ni mbunge halali wa kuchaguliwa kwa kura halali ana mwanae Owenya na mkwe wake Kihwelu.

2. Chama kinaongonzwa na mkwe wa mwasisi wake na pia ni mbunge wa kupigiwa kura.

3. Tundu Lisu amechaguliwa ila dada yake pia ni mbunge wa viti maalum hatujui pengine mbele ya safari na yeye atataka aongeze mmoja ili aende sawa na mzee ndesapesa.

4. Dr. Slaa kwa bahati mbaya hajarudi bungeni ila yupo mzazi mwenzie Bi Rose Kamili, nina uhakika Mshumbusi na yeye 2015 ataungana na Rose Kamili bungeni.

Hii ni kansa inayokiandama chama cha demokrasia na maendeleo naomba niweke wazi kuwa nina nia njema na hiki chama ndio maana nayazungumza sasa hivi singojei mpaka ifike wakati wa kampeni na kwa kufahamu kina Kitila Mkumbo na Zitto wamo humu basi watafanyia kazi.

Asanteni sana....


 
Hao niliowalist ni tunawaowajua bila kuangalia ujamaa wa ukaribu na viongozi kwa waliobakia...
 
hilo na mimi naona ni tatizo.ila miafrika ndivyo ilivyo sisi tunakomaa na mafisadi wao wanajazana kindugu kwenye chama shauri yao wakileta zao tunawakacha tunaangali kwingine.
ccm si mama yangu.
na chadema si kaka yangu.
mpinzani wa kweli ndiye tutamsapoti kuikomboa tanzania.
aluta kontinua.
 
hilo na mimi naona ni tatizo.ila miafrika ndivyo ilivyo sisi tunakomaa na mafisadi wao wanajazana kindugu kwenye chama shauri yao wakileta zao tunawakacha tunaangali kwingine.
ccm si mama yangu.
na chadema si kaka yangu.
mpinzani wa kweli ndiye tutamsapoti kuikomboa tanzania.
aluta kontinua.

Nilipata kusikia hili jambo linamkera sana Zitto na alikuwa na mpango kumsimamia mama yake na yeye apata viti maalum sijui liliishia wapi......
 
Hassan Mwinyi na Hussein Mwinyi, Kikwetes' family haya Riz1 anasomewa taarifa za utendaji na wakuu wa mikoa, Kawawas' Kigoma Malimas' Samuel Sita Magret Sita, John Malecela Anna Kirango Malecela, Anna Abdalah Pius Msekwa, unata niendelee kukutajia mlundikano wa watoto wa vigogo wa ccm kwenye nafasi nyeti za Bongo?? acha majungu hiyo ndiyo Bongo
 
Hassan Mwinyi na Hussein Mwinyi, Kikwetes' family haya Riz1 anasomewa taarifa za utendaji na wakuu wa mikoa, Kawawas' Kigoma Malimas' Samuel Sita Magret Sita, John Malecela Anna Kirango Malecela, Anna Abdalah Pius Msekwa, unata niendelee kukutajia mlundikano wa watoto wa vigogo wa ccm kwenye nafasi nyeti za Bongo?? acha majungu hiyo ndiyo Bongo

Well Rizwani ni mbunge wa jimbo gani labda? Hussein Mwinyi nadhani kama sikosei ni mbunge wa mkuranga na sio wa viti maalum. Malecela na Anne Kilango wamechaguliwa kwa Kura na Anne Kilango hakuwa viti maalum alipoolewa na Malecela. Sijui labda sina Kumbukumbu vizuri maana sijawahi kusikia Pius Msekwa kuwa ni Mbunge wa jimbo fulani na kikubwa tunazungumzia viti vya upendeleo vinavyogawiwa ndani ya chama sio kusimama kugombea ubunge....
 
Kawawa's n Sitta's

Duh pengine sijui nipe majina yao maana nimeatilia list ya viti vyao maalum sijaona jina la kawawa labda mke wa Sita na vyama vya upinzani wanatakiwa waspot makosa hayo ili wasiyafanye maana kuchaguana kikoo italeta picha mbaya.... Sisiemu wao japo wanautaratibu lakini pia kumejaa kujuana hatutaki hili liwe gonjwa pia kwa chadema....
 
Acha unafiki, mbona huongelei ya akina Makamba and family, Kikwete and family, na mengine mengi kwenye taasisi nyeti za serikali kama BoT, Ikulu, etc.

Halafu haya ya Chadema hayakuhusu kama wewe si mwanacham, tutayashugulikia kichama
 
Watu wenye upeo mdogo huangalia opportunities za mjengoni tu na kutoa judgement. But our country has more opportunities outside the Parliement na huko ndo wakubwa wa siasa wamejaza watoto wao ndugu zao na wake zao. My mind ilivuka hiyo level ya kujadili mjengoni. Sitta alikuwa Spika juzi tu mke wake akiwa waziri! Malecela na Mkewe juzi tu walikuwa wote mjengoni, and again the country is developing leanage type of leadership through ccm, baada ya KArume mzee akaja karume mtoto, Mwinyi sasa tuna Hussein Mwinyi, Kawawa Rashid Kawawa Victor, Kigoma Malima, Adam Malima, Yusuph Makamba January Makamba,! msururu ni mrefu ukiachilia mbali maofisa mbalimbali hapo juu! Hiyo ndiyo Bongo mtoto wa mkulima ashike jembe kwa bidii maana mpenyo haupo
 
bora hata hao Chadema kulliko CCM kwasababu mke yupo kwenye mhimili mmoja wapo na mume yupo kwenye mhimili mwingine hamuoni kama hiyo ni hatari zaidi katika mstakabali mzima wa maamuzi ya nchi?vipi ilivyokuwa Kigoda na dada yake Aisha kigoda na shemejiKhatib aliyekuwa Waziri katika baraza liliisha muda wake,acheni hizo tuchape kazi ndio la msingi!!
 
Hao niliowalist ni tunawaowajua bila kuangalia ujamaa wa ukaribu na viongozi kwa waliobakia...


Naona hapa unataka kuonyesha kwa msisitizo jinsi unavyo tumiwa kuwatoa watanganyika kwenye masuala ya muhimu. Tunataka katiba mpya, tume huru ya uchaguzi itakayotupa rais tumtakaye sio rais wa tume, tunataka muungona wenye mariziano ya pate zote husika sio muungano wenye kigugumizi, tunataka mgawanyo mzuri wa rasmali za nchi yetu sio sasa ambapo zina wanufasha wachache. 4ur information bila ya mambo haya kupatiwa ufumbuzi hamna atakaye kuwa salama kwenye nji hii ni suala la muda tu haya yataanza kujitokeza moja juu ya jingine. Sasa wewe na hao wanao kutumia, jidanganye tu kuwa mnavuta subira madai haya yataisha kwa natural death. Endeleeni kujidangaya kwani wa jinga ndo wali wao.
 
Acha unafiki, mbona huongelei ya akina Makamba and family, Kikwete and family, na mengine mengi kwenye taasisi nyeti za serikali kama BoT, Ikulu, etc.

Halafu haya ya Chadema hayakuhusu kama wewe si mwanacham, tutayashugulikia kichama

Sote tunakereka na hilo haiamanishi tuwaige kwa kujaza ndugu zetu kwenye nafasi za chama huo ni mwanzo tu kama alivyotanguliza mwenzetu tupo "bize" na mafisadi wenzetu wanajaza ndugu zao kwenye chama "wanapeana ulaji"
 
Naona hapa unataka kuonyesha kwa msisitizo jinsi unavyo tumiwa kuwatoa watanganyika kwenye masuala ya muhimu. Tunataka katiba mpya, tume huru ya uchaguzi itakayotupa rais tumtakaye sio rais wa tume, tunataka muungona wenye mariziano ya pate zote husika sio muungano wenye kigugumizi, tunataka mgawanyo mzuri wa rasmali za nchi yetu sio sasa ambapo zina wanufasha wachache. 4ur information bila ya mambo haya kupatiwa ufumbuzi hamna atakaye kuwa salama kwenye nji hii ni suala la muda tu haya yataanza kujitokeza moja juu ya jingine. Sasa wewe na hao wanao kutumia, jidanganye tu kuwa mnavuta subira madai haya yataisha kwa natural death. Endeleeni kujidangaya kwani wa jinga ndo wali wao.


Kama kutumwa utakua umenituma wewe nakereka kuona watu makini kama mimi tunashindwa kujua tukimbilie wapi maana huko CCM Kuna nuka kwa uvundo na huku kwenye vyama vyetu vingi kila kimoja kina matatizo yake kuna vya kidini vingine tunaambiwa vya kidini na kifamilia basi hata hujui ni wapi ukimbilie.

Well nadhani hata Chadema wanahitaji katiba mpya ya chama kabla ya kudai ya taifa maana kwa mfano katiba yao haisemi jinsi ya kuchagua watu wa viti maalum wao wamevigeuza "maaluum" kwa watu wao "maalum"
 
Kama kutumwa utakua umenituma wewe nakereka kuona watu makini kama mimi tunashindwa kujua tukimbilie wapi maana huko CCM Kuna nuka kwa uvundo na huku kwenye vyama vyetu vingi kila kimoja kina matatizo yake kuna vya kidini vingine tunaambiwa vya kidini na kifamilia basi hata hujui ni wapi ukimbilie.

Well nadhani hata Chadema wanahitaji katiba mpya ya chama kabla ya kudai ya taifa maana kwa mfano katiba yao haisemi jinsi ya kuchagua watu wa viti maalum wao wamevigeuza "maaluum" kwa watu wao "maalum"

Kwa wale tunaofanya mambo kwa kuya prioritise katiba ya nchi hii ndio msingi wa sheria nyingine zote. Hivyo basi priority hapa ni katiba ya nchi si za vyama. Naunavyo zidi kufafanua ndivyo unafojifafanua zaidi kuwa wanakutumia.
 
Back
Top Bottom