Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,393
Ni jambo ambalo litawashtua wanawake, hasa walioolewa au ambao wana wapenzi wanaoaminika, kwamba, kila wanaume kumi ambao unakutana nao kila siku, watano kati yao ni lazima wameshakutana na kufanya mapenzi na wanaoitwa makahaba. Ni wepi watano kati ya hao kumi, ni jambo lenye kushangaza zaidi. Unaweza kuhisi kwamba, kati ya hao kumi, ni wale wanaume wahuni na chakaramu, ndio watakaokuwa wamekutana kimwili na makahaba……… Umekosea!
Kwa kawaida kati ya hao kumi, watano ambao watakuwa wameshatembea na makahaba watakuwa ni wale ambao huwezi kuwategemea. Kwa nini? Kwa sababu ni wale wenye kujiheshimu kwa nje, wenye uwezo na pengine waliosoma vizuri. Hapa hata hivyo tunazungumzia makahaba ambao wanajiuza kwa kiwango kinachoweza kukubalika kwa watu wengi wakiwemo wageni kutoka nje. Wale makahaba kama wa Uwanja wa Fisi au Kimboka pale Buguruni hawahesabiwi kama makahaba katika viwango vya kiutafiti kama huu uliofanywa duniani kote.
Kahaba kwa kawaida huhitaji fedha na pengine mahali pa kwenda kufanyia mapenzi na hili linawezekana kwa mwanaume mwenye uwezo kifedha. Kwa hali hiyo, watano kati ya hao wanaume kumi ni lazima wawe ni wale wenye uwezo mzuri kifedha. Kuna tafiti zinazoonesha kwamba, wanaume wanaochukua makahaba angalau mara moja kwenye maisha yao, ni zaidi ya watano kati ya kila kumi. Baadhi ya tafiti zinaonesha kwamba, wanaume sita hadi saba, huchukua makahaba katika maisha yao, hata kama ni mara moja tu.
Lakini jambo la kushangaza na kusikitisha ni kwamba, imebainika sasa kuwa, wanaume wanaochukua makahaba, nusu yake ni wanaume ambao wameoa au wana wapenzi wanaowaamini sana. Kwa haraka mtu anaweza kuichukulia taarifa hii kama jambo lisilo na maana sana au lisilo jipya, lakini ni taarifa isiyopendeza kwa wanandoa au wapenzi.
Tofauti na nyumba ndogo, kuchukua kahaba kunaweza kumfanya mwanaume asikamatwe kwa maisha yake yote, kwani kahaba na mnunuzi wake humaliza biashara huko huko. Kwa wale wakazi wa jijini Dar wanajua vizuri kwamba, makahaba wengi hufanyia mapenzi kwenye magari na hata makaburini na wanaofanya nao kuna miongoni mwao wanaoheshimika katika jamii. Ndio maana wanawake ambao wana waume wenye uwezo kifedha hawapaswi kujidanganya kwamba, waume zao hawawezi kutembea na makahaba. Kwa sehemu kubwa tafiti zinaonesha kwamba, uwezekano huo ni mkubwa sana. Kama watano kati ya kila kumi wanaweza kufanya hivyo, basi idadi ni kubwa
Kwa kawaida kati ya hao kumi, watano ambao watakuwa wameshatembea na makahaba watakuwa ni wale ambao huwezi kuwategemea. Kwa nini? Kwa sababu ni wale wenye kujiheshimu kwa nje, wenye uwezo na pengine waliosoma vizuri. Hapa hata hivyo tunazungumzia makahaba ambao wanajiuza kwa kiwango kinachoweza kukubalika kwa watu wengi wakiwemo wageni kutoka nje. Wale makahaba kama wa Uwanja wa Fisi au Kimboka pale Buguruni hawahesabiwi kama makahaba katika viwango vya kiutafiti kama huu uliofanywa duniani kote.
Kahaba kwa kawaida huhitaji fedha na pengine mahali pa kwenda kufanyia mapenzi na hili linawezekana kwa mwanaume mwenye uwezo kifedha. Kwa hali hiyo, watano kati ya hao wanaume kumi ni lazima wawe ni wale wenye uwezo mzuri kifedha. Kuna tafiti zinazoonesha kwamba, wanaume wanaochukua makahaba angalau mara moja kwenye maisha yao, ni zaidi ya watano kati ya kila kumi. Baadhi ya tafiti zinaonesha kwamba, wanaume sita hadi saba, huchukua makahaba katika maisha yao, hata kama ni mara moja tu.
Lakini jambo la kushangaza na kusikitisha ni kwamba, imebainika sasa kuwa, wanaume wanaochukua makahaba, nusu yake ni wanaume ambao wameoa au wana wapenzi wanaowaamini sana. Kwa haraka mtu anaweza kuichukulia taarifa hii kama jambo lisilo na maana sana au lisilo jipya, lakini ni taarifa isiyopendeza kwa wanandoa au wapenzi.
Tofauti na nyumba ndogo, kuchukua kahaba kunaweza kumfanya mwanaume asikamatwe kwa maisha yake yote, kwani kahaba na mnunuzi wake humaliza biashara huko huko. Kwa wale wakazi wa jijini Dar wanajua vizuri kwamba, makahaba wengi hufanyia mapenzi kwenye magari na hata makaburini na wanaofanya nao kuna miongoni mwao wanaoheshimika katika jamii. Ndio maana wanawake ambao wana waume wenye uwezo kifedha hawapaswi kujidanganya kwamba, waume zao hawawezi kutembea na makahaba. Kwa sehemu kubwa tafiti zinaonesha kwamba, uwezekano huo ni mkubwa sana. Kama watano kati ya kila kumi wanaweza kufanya hivyo, basi idadi ni kubwa