Zipuwawa
JF-Expert Member
- Nov 28, 2010
- 3,053
- 653
Mara nyingi huwa ninajiuliza maswali na kukosa majibu.Kwanini Tanzania tujisifu kila siku kuwa ni Nchi ya Amani wakati Watanzania wake mioyoni mwetu tumejaa Manung'uniko kila kukicha? Kila kukicha matatizo yanaiandama Tanzania Umasikini,Mgao wa Umeme,Huduma Mbovu za Afya,Miundo mbinu Mibovu,Ufisadi, Magonjwa na matatizo mengine mengi ambayo hata wewe unaweza kuyaongeza.
Je ni wazi kuwa Nchi ili iwe ya Amani tunaiangalia tu kuwa hatupigani vita? Je kama watanzania wa Leo hawana Amani Mioyoni mwao kuna haja gani ya kusema Watanzania wana Amani?
Kila nikijiuliza huwa nabaki bila majibu, basi tuache unafiki kwa kujisifia wakati tunaandamwa na Amatatizo kila Kona.
December 9 tunatimiza miaka 49 ya UHURU ambayo ni Nusu karne ila hatujui tunako kwenda hadi sasa.
Je ni wazi kuwa Nchi ili iwe ya Amani tunaiangalia tu kuwa hatupigani vita? Je kama watanzania wa Leo hawana Amani Mioyoni mwao kuna haja gani ya kusema Watanzania wana Amani?
Kila nikijiuliza huwa nabaki bila majibu, basi tuache unafiki kwa kujisifia wakati tunaandamwa na Amatatizo kila Kona.
December 9 tunatimiza miaka 49 ya UHURU ambayo ni Nusu karne ila hatujui tunako kwenda hadi sasa.