Hili la watumishi Serikalini kutakiwa wataje makabila yao na dini zao lingetendeka Kenya, humu hakungekalika

MK254 amekuuliza swali zuri Sana, na amekuwekea hotuba ya Nyerere, sidhani Kama umejibu swali lake, kujua dini na kabila la mtu itasaidia nini katika dunia ya Sasa inayotumia alama za vidole(Biometric data) katika kujua utambulisho wa mtu?
 
Kutaja dini na kabila ipo sehemu nyingi tu hata mahakamani nia yake hasa ili uhudumiwe vizuri kwa kuwa kuna utofauti kwenye dini na dini mfano mahakamani unahitajika kuapa pia kujua kabila lako linasaidia pia kwenye mahakama kama itahitajika mkalimani. Kwenye utumishi wa umma inasaidia katika kumpangia mwajiriwa sehemu ya kufanyakazi au kutoa huduma isije ukajikuta kabila au dini fulani wamepangia sehemu au idara fulani pekee yao. Ila TZ hakuna ukabila kama ulivyo Kenya mimi nilifanyakazi Kenya miaka kama nne nilichokiona huko kazini ni aibu hata kwenye bar hasa wajaluo na wakikuyu ukijichanganya tu mjaluo au mkikuyu akaenda kunywa kwenye bar ya wakikuyu au wajaluo anaweza kuwekewa hata sumu wakati TZ hicho kitu hakipo kabisa.
Pumba tuu... Mfano mahakamani sijawahi kuona faida ya kuapa kwani bado hao walioapa wanasema uongo na kuleta vielelezo vya uongo/forgery na hakimu/jaji anaona na hafanyi lolote... Nitajie case ambapo mtu alishindwa kuongea Kiswahili akaletewa mkalimani aongee kikwao...
 
Kama huna kabila ni wewe and it's your problem. Hata hivyo nami napinga vikali kuwa kabila na dini kwenye CV za watumishi. Ndiyo maana CAG Pror Assad alisema hatuna viongozi wenye uwezo...
Kutokua au kuwa na kabila ni tatizo?
 
MK254 amekuuliza swali zuri Sana, na amekuwekea hotuba ya Nyerere, sidhani Kama umejibu swali lake, kujua dini na kabila la mtu itasaidia nini katika dunia ya Sasa inayotumia alama za vidole(Biometric data) katika kujua utambulisho wa mtu?
Na wew pia tupe madhara ya kujua dini na kabila lako
 
Kwa hiyo performance ya mtumishi wa serikali inategemea dini na kabila lake siyo?
Wewe una wasiwasi gani hawajasema kwamba iyo ni kuongoza performance ishu ni kuleta uswa mlishachomekana sana huko nyuma Magufuli akaja na vyeti feki wengi walikamatwa

Sasa hapa ni balance we una wasiwasi gani kwani ikiwezekana wanabalance hakuna mtu wa kanda ya pwani aliye na ubaguzi ishu izo za ubaguzi zipo huko bara kwenu kujifanya wajuaji

Hao wanaondika makala wote ni wa kanda moja tu wanajijua huu mtego watanasa kuna mabank wanafanya kazi wachaga tu mengine wasukumu ulisikia wapi kanda ya pwani ina uwezo ubaguzi wanavyopenda wageni

Raisi ana aminika 100% kama una lingine sema
 
Back
Top Bottom