Hili la utafunaji wa kodi zetu! Wananchi tuonyeshe hisia zetu!

Trable

JF-Expert Member
Jan 3, 2023
1,783
3,278
Mpaka lini sisi tutaendelea kuitwa masikini? Huu umasikini tunaoitwa nao kila leo, sababu yake ni ipi kama sio hii ya wakubwa kuiba mapesa yetu? Ni kweli kabisa sisi ni masikini au ni upumbavu wetu?

Umasikini upi tulionao sisi ili hali robo nzima ya bajeti yetu, inaishia mifukoni mwa viongozi? Unajua inauma eeh? Pale unapolipa kodi tena kwa vitisho na wakati mwingine unaletewa na maasikari ili tu ulipe kodi! Unalipa na mafaini kibao, unaendelea kudunduliza tena mara ghafula tena, kodi unaodaiwa, unapaswa kulipa!

Inapotokea mambo mabaya kabisa kwa serikali unayopaswa kuitii kwakulipa kodi ili iturahisishie huduma kwa kutusogezea karibu, unaambiwa mabilioni ya kodi hizi zimekwapuliwa na wahusika kuishia kutolewa kwenye nyadhifa zao bila hatua nyinginezo za kuwalazimisha kurudisha pesa hizi! Inauma, inakera! Inatia uchungu na kuhudhunisha sana, pia inakatisha tamaa sana kwa walipa kodi waaminifu na wenye mapenzi na nchi!

Kwa namna hii, wananchi yatubidi kuonyesha hisia zetu bila kujali tofauti ya vyama vyetu!

Hawa wakurugenzi, madiwani na wengine ambao ni wasimamizi wa kodi zetu, hivi tuwafanyeje sisi? Tuwatafune? Tuwameze? Au tudili nao kwa namna gani nzuri ili wawe mfano kwa watakaofyata?

Ikiwezekana sasa, wananchi wote, mikoa yote tuandamane kupinga ulaji wa kodi zetu hizi

😎😎😎

Mh Raisi! Wewe usipate kazi kubwa, onyesha udikiteta kiduchu tu sisi huku tuwakanyage!
 
Mama Samia, piga chini haraka hao wezi jana uliwaambia wajiuzulu ila hadi sasa wako kimya, hawawezi jiuzulu kwa tabia zetu, piga kalamu nyekundu haraka, sisi wananchi wako tunakupenda sana, hao majizi futilia mbali, usiaambie wakupishe, hawataondoka, piga chini haraka sana

Bil 135 tsh sawa na $ 49 mil ni nyingi mno zilitaka kuliwa, Mama yetu, Rais wetu, piga chiniiii, OMG hayo majitu sugu sana.
 
Wananchi gani unawazungumzia waonyeshe hisia? Ni wananchi hawa ninaowajua ambao wapo tayari kulia na kugaragara na kupasua mishipa ya kichwa kwa kumtetea diamond au alikiba au wananchi hawa ambao wapo tayari kwa lolote pale team zao za Simba na Yanga zinapofanya vibaya wataongea kwa hisia na kulia kabisa,lakini kwenye mambo ya msingi yanaogusa maisha yao moja kwa moja hawana muda nayo ndio maana viongozi wanapeta tu kwa sababu hakuna wa kuwapresulize.
 
Usitarajie chochote kwa watanzania hakuna tuwezalo zaidi ya kufuatilia udaku na maneno mengi hakuna vitendo
 
  • Thanks
Reactions: TPP
Hakuna la maana Watanganyika mtafanya na hao viongozi wameisha wajulia mtalalamika tu mwisho mtasahau na kutulia hakuna hatua yoyote mtachukua. Uoga umewajaa sana kwenye nyoyo zenu kama kweli mna uchungu na hizo kodi zenu kiamsheni kama wanavyo fanya jirani zenu wakenya.
 
Mpaka lini sisi tutaendelea kuitwa masikini? Huu umasikini tunaoitwa kila leo, sababu yake ni ipi kama sio hii ya wakubwa kuiba mapesa yetu? Ni kweli kabisa sisi ni masikini au ni upumbavu wetu?

Umasikini upi tulionao sisi ili hali robo nzima ya bajeti yetu, inaishia mifukoni mwa viongozi? Unajua inauma eeh? Pale unapolipa kodi tena kwa vitisho na wakati mwingine unaletewa na maasikari ili tu ulipe kodi! Unalipa na mafaini kibao, unaendelea kudunduliza tena mara ghafula tena, kodi unaodaiwa, unapaswa kulipa!

Inapotokea mambo mabaya kabisa kwa serikali unayopaswa kuitii kwakulipa kodi ili iturahisishie huduma kwa kutusogezea karibu, unaambiwa mabilioni ya kodi hizi zimekwapuliwa na wahusika kuishia kutolewa kwenye nyadhifa zao bila hatua nyinginezo za kuwalazimisha kurudisha pesa hizi! Inauma, inakera! Inatia uchungu na kuhudhunisha sana, pia inakatisha tamaa sana kwa walipa kodi waaminifu na wenye mapenzi na nchi!

Kwa namna hii, wananchi yatubidi kuonyesha hisia zetu bila kujali tofauti ya vyama vyetu!

Hawa wakurugenzi, madiwani na wengine ambao ni wasimamizi wa kodi zetu, hivi tuwafanyeje sisi? Tuwatafune? Tuwameze? Au tudili nao kwa namna gani nzuri ili wawe mfano kwa watakaofyata?

Ikiwezekana sasa, wananchi wote, mikoa yote tuandamane kupinga ulaji wa kodi zetu hizi

😎😎😎

Mh Raisi! Wewe usipate kazi kubwa, onyesha udikiteta kiduchu tu sisi huku tuwakanyage!
Kabisa tunapaswa kuandamana na sio kupongeza upuuzi unaoendelea.
 
Wananchi gani unawazungumzia waonyeshe hisia? Ni wananchi hawa ninaowajua ambao wapo tayari kulia na kugaragara na kupasua mishipa ya kichwa kwa kumtetea diamond au alikiba au wananchi hawa ambao wapo tayari kwa lolote pale team zao za Simba na Yanga zinapofanya vibaya wataongea kwa hisia na kulia kabisa,lakini kwenye mambo ya msingi yanaogusa maisha yao moja kwa moja hawana muda nayo ndio maana viongozi wanapeta tu kwa sababu hakuna wa kuwapresulize.
Watanzania wengi wamelaaniwa hawajui haki zao
 
Hapa wengine mnalalamika ila mnaibia mabosi zenu kazini, mnaiba mafuta ya gari za ofisini etc.
 
Hapa wengine mnalalamika ila mnaibia mabosi zenu kazini, mnaiba mafuta ya gari za ofisini etc.
Mkuu, yote hayo tunataka tuyakomeshe' ila tuanze kwanza huko juu kwa viongozi majizi haya
 
hawajaanza kuzitafuna leo, kuna watu hawatishiwi nyau serikali iko mfukoni haya mambo ni mazito sana.
Matatizo yanaanzia kwenye katiba watu wabaya wanaitumia huo dhaifu. Wananchi nao ni wapole/waoga wakijaribu kuinuka wenyenchi wanasimama na nguvu ya dola upepo unapita.
Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, abadi abadi kamba itaka jiwe.
 
hawajaanza kuzitafuna leo, kuna watu hawatishiwi nyau serikali iko mfukoni haya mambo ni mazito sana.
Matatizo yanaanzia kwenye katiba watu wabaya wanaitumia huo dhaifu. Wananchi nao ni wapole/waoga wakijaribu kuinuka wenyenchi wanasimama na nguvu ya dola upepo unapita.
Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, abadi abadi kamba itaka jiwe.
Iko siku!
 
Back
Top Bottom