Hili la Pinda kuchangia Tshs10m kwa USDM limekaa vipi hili?

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Jana Waziri Mkuu ameahidi kuchanga milion 10 kila mwaka mpaka ukomo wa utumishi wake ili pesa hizi zitumike kuwasaidia wanafunzi kutatua matatizo yao ya malazi, huyu ni Waziri Mkuu na mtendaji mkuu wa serikali!

Jamani kama hii ndiyo aina ya viongozi tulio nao basi tuna kazi ya ziada, utafanya nini na milioni 10 kwenye ujenzi? Hivi kuna ulazima wowote wa Pinda kuingia mfukoni mwake kutatua kero za wananchi? Au anatuambia kuwa analipwa hela nyingi mno kiasi hiki?

Kama ningekuwa Pinda, nisingeahidi chochote kwa wanafunzi, ningewaahidi kulichukua na kulifanyia kazi. Ningewatafuta wawekezaji wa ndani hasa hasa mashirika ya Pension na kuwaomba wawekeze kwenye ujenzi kwa ubia na UDSM, UDSM wana ardhi ya kutosha ambayo sasa inamezewa mate na walafi kwa ajiri ya kujenga shopping mall, which as good as it is it is the not the first priority for UDSM!

Pinda jiuzuru kama kazi uliyopewa ni kubwa kuliko uwezo wako!

Habari kamili soma hapa:http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/6851-pinda-apokewa-kwa-bango-udsm
 
Jana Waziri Mkuu ameahidi kuchanga milion 10 kila mwaka mpaka ukomo wa utumishi wake ili pesa hizi zitumike kuwasaidia wanafunzi kutatua matatizo yao ya malazi, huyu ni Waziri Mkuu na mtendaji mkuu wa serikali!

Jamani kama hii ndiyo aina ya viongozi tulio nao basi tuna kazi ya ziada, utafanya nini na milioni 10 kwenye ujenzi? Hivi kuna ulazima wowote wa Pinda kuingia mfukoni mwake kutatua kero za wananchi? Au anatuambia kuwa analipwa hela nyingi mno kiasi hiki?

Kama ningekuwa Pinda, nisingeahidi chochote kwa wanafunzi, ningewaahidi kulichukua na kulifanyia kazi. Ningewatafuta wawekezaji wa ndani hasa hasa mashirika ya Pension na kuwaomba wawekeze kwenye ujenzi kwa ubia na UDSM, UDSM wana ardhi ya kutosha ambayo sasa inamezewa mate na walafi kwa ajiri ya kujenga shopping mall, which as good as it is it is the not the first priority for UDSM!

Pinda jiuzuru kama kazi uliyopewa ni kubwa kuliko uwezo wako!

Habari kamili soma hapa:http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/6851-pinda-apokewa-kwa-bango-udsm

Ni usanii tu.
 
Pinda hajui hata wajibu wake, ndo maana huamua kulia lia tu. Kama ameona kuna tatizo pale kwa nini asi adjust sera zilizopo? yeye anaacha kazi after five years sasa itakuwaje baada ya hapo? ila msimseme sana atalia na mimi sitaki kumuona msanii akilia maaana aibu
 
Kama unataka kuwa radical kuhusu Pinda, ana matatizo mengi (si Waziri Mkuu halali kwa sababu si mbunge wa kuchaguliwa kwa mfano) lakini sioni vipi hili la kutoa linakuwa tatizo, ukiondoa swala la anapata wapi milioni kumi za kutoa spontaneously hivyo. Tusitake kuwavunja moyo hata wenye kutaka kuanza tu kutatua matatizo.

Hili swala Pinda ana lawama zake za serikali kiujumla, kwamba walitakiwa kulijua na kulifanyia kazi hata kabla ya aibu hii.

Lakini kwa jinsi alivyolihandle, siwezi kumlaumu. Amekubaali tatizo lipo, hajawapa Kiswahili cha "tutalishughulikia" ambacho kingeweza kuwa ndicho kitu rahisi kabisa kufanya, ameonyesha kujitoa yeye binafsi kwa kuchangia pesa zake, na kaleta chachu ya kutaka viongozi wenzake wachangie - ingawa sijui hata wanachochangia specifically ni nini, it may be too early to specify at this point anyway- lakini angalau mtu unaona huyu hili jambo limemuuma na kalianzia kwa vitendo.

Na kutoa hivi hakuna maana kwamba mtu hawezi kwenda kutafuta fumbuzi nyingine zinazojikita katika sera zaidi na mipango kabambe ya kiuwekezaji (na wala hakumaanishi kwamba mipango hii itafanyika pia).

Wasomi waliojaliwa neema kuchangia vyuo walivyosomea ni kitendo cha kawaida kabisa dunia nzima. Wahitimu wa UDSM waliofanikiwa kimaisha wako wapi? Kabla ya kuinyooshea vidole serikali, sisi wenyewe wananchi tuko tofauti vipi na serikali hii tunayotaka kuilaumu ?

Pindakama mtu binafsi msemeni kwa mengine, siyo hili. Kama mnalaumu serikali kwa kuachia hili mpaka lifika hapa, of course lawama zipo kedekede na Pinda hawezi kuzkwepa.
 
unataka we uchangie au umeona nini mtu anasaidi we unapinga ili waeendelee kuteseka au? Kila kitu ni kupinga unataka aijie ushauri kwako? Pinda ndo mzalendo 4memuuma mpaka akaamua atoe naye kutokana na mshahara wake we unataka atoe ahadi ambazo hazina maana?
 
Pinda ana haki ya kuchangia kama Pinda. sioni tatizo. na hapa kachangia specifically kwa malazi. Hajachangia kuondoa tatizo la mikopo ambalo ni jikumu la serikali.
 
Kama unataka kuwa radical kuhusu Pinda, ana matatizo mengi (si Waziri Mkuu halali kwa sababu si mbunge wa kuchaguliwa kwa mfano), lakini sioni vipi hili la kutoa linakuwa tatizo, ukiondoa swala la anapata wapi milioni kumi za kutoa spontaneously hivyo. Tusitake kuwavunja moyo hata wenye kutaka kuanza tu kutatua matatizo.

Hili swala Pinda ana lawama zake za serikali kiujumla, kwamba walitakiwa kulijua na kulifanyia kazi hata kabla ya aibu hii.

Lakini kwa jinsi alivyolihandle, siwezi kumlaumu. Amekubaali tatizo lipo, hajawapa Kiswahili cha "tutalishughulikia" ambacho kingeweza kuwa ndicho kitu rahisi kabisa kufanya, ameonyesha kujitoa yeye binafsi kwa kuchangia pesa zake, na kaleta chachu ya kutaka viongozi wenzake wachangie - ingawa sijui hata wanachochangia ni nini- lakini angalau mtu unaona huyu hili jambo limemuuma na kalianzia kwa vitendo.

Na kutoa hivi hakuna maana kwamba mtu hawezi kwenda kutafuta fumbuzi nyingine zinazojikita katika sera zaidi na mipango kabambe ya kiuwekezaji (na wala hakumaanishi kwamba mipango hii itafanyika pia).

Wasomi waliojaliwa neema kuchangia vyuo walivyosomea ni kitendo cha kawaida kabisa dunia nzima. Wahitimu wa UDSM waliofanikiwa kimaisha wako wapi? Kabla ya kuinyooshea vidole serikali, sisi wenyewe wananchi tuko tofauti vipi na serikali hii tunayotaka kuilaumu ?

Pindakama mtu binafsi msemeni kwa mengine, siyo hili. Kama mnalaumu serikali kwa kuachia hili mpaka lifika hapa, of course lawama zipo kedekede na Pinda hawezi kuzkwepa.

Nyie acheni upuuzi, tafuta chanzo cha tatizo then find a solution. Ni sawa una dependants wako kwenu then unawapa pesa kila siku it doesnt help wapeleke shule wasome wajitegemee. Je ukifa leo nani atawapa pesa tena>??? kama ungewapeleka shule wangeendelea kujitegemea. Hivyo jamaa kwa great thinkers wanaona hajatatua tatizo ila kalifunika tu tatizo bado liko pale pale
 
Pinda ana haki ya kuchangia kama Pinda. sioni tatizo. na hapa kachangia specifically kwa malazi. Hajachangia kuondoa tatizo la mikopo ambalo ni jikumu la serikali.

Kuona tatizo ni lazima uwe na macho ya ziada, wewe hamtofautiani na pinda naye ambaye tatizo aliiona vibaya na solution yake ikawa kama hiyo aliyotoa.
 
Nyie acheni upuuzi, tafuta chanzo cha tatizo then find a solution. Ni sawa una dependants wako kwenu then unawapa pesa kila siku it doesnt help wapeleke shule wasome wajitegemee. Je ukifa leo nani atawapa pesa tena>??? kama ungewapeleka shule wangeendelea kujitegemea. Hivyo jamaa kwa great thinkers wanaona hajatatua tatizo ila kalifunika tu tatizo bado liko pale pale

Mazee hakuna aliyesema kutoa milioni kumi kila mwaka kunamzui mtu kutafuta permanent solution. Kama serikali inashindwa kupata permanent solution, isemeni kwa kukosa permanent solution, sio kumuandama Pinda kwa sababu kaleta challenge ya watu kuchangia vyuo walivyohitimu, kitu kinachofanyika dunia nzima.
 
Fredy Azzah
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jana walimkaribisha chuoni kwao Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa bango lililoandikwa "Mtoto wa Mkulima, Tunalala Nje", kilio kilichomsukumu mtendaji huyo mkuu wa serikali kuahidi kukichangia Sh10 milioni kila mwaka kwenye ujenzi wa malazi yao hadi ukomo wa uongozi wake.

Huyu kweli ni "Mtoto wa Mkulima"? Jameni, idadi ya wakulima nchini ni 80% ya wananchi wote, je watoto wa wakulima wenye uwezo wa kutoa mchango kama huu nchini ni wangapi? Nasemea "watoto wa wakulima" wanao tegemea kilimo kujikimu, siyo watoto wa mafisadi. Au ndo muendelezo wa usanii? Watoto wa mafisadi wametoa ngapi? Kumbe Bongo hatuhitaji misaada, kama mtoto wa mkulima anatoa zote hizo msaada wa nini? Vinginevyo naona kama ni muendelezo wa filamu ya KISANII TU!
 
Kuona tatizo ni lazima uwe na macho ya ziada, wewe hamtofautiani na pinda naye ambaye tatizo aliiona vibaya na solution yake ikawa kama hiyo aliyotoa.

Ok Mimi siko tofauti na Pinda nakubali wewe hauko tofauti na nani au uko sawa na nani ? Kesho akichangia Yatima utasemaje? Before u criticise someone walk a mile on his shoes.

Ebu sema serikali au Pinda inatakiwa kufanya nini kuhusu tatizo la Malazi UDSM.hii ni kazi ya Uongoi wa UDSM wenyewe. Kuna mipaka.
 
Fredy Azzah
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jana walimkaribisha chuoni kwao Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa bango lililoandikwa "Mtoto wa Mkulima, Tunalala Nje", kilio kilichomsukumu mtendaji huyo mkuu wa serikali kuahidi kukichangia Sh10 milioni kila mwaka kwenye ujenzi wa malazi yao hadi ukomo wa uongozi wake.

Huyu kweli ni "Mtoto wa Mkulima"? Jameni, idadi ya wakulima nchini ni 80% ya wananchi wote, je watoto wa wakulima wenye uwezo wa kutoa mchango kama huu nchini ni wangapi? Nasemea "watoto wa wakulima" wanao tegemea kilimo kujikimu, siyo watoto wa mafisadi. Au ndo muendelezo wa usanii? Watoto wa mafisadi wametoa ngapi? Kumbe Bongo hatuhitaji misaada, kama mtoto wa mkulima anatoa zote hizo msaada wa nini? Vinginevyo naona kama ni muendelezo wa filamu ya KISANII TU!

Mazee, ingawa swali lako la msingi lina mantiki, na mimi nimeliuliza hapo juu, ulivyosema kwamba mtoto wa mkulima hawezi kupata hizo pesa nakushangaa. Kwanza kuna wakulima wa aina tofauti, pili, hata kama Pinda ni mtoto wa wakulima masikini, yeye si mkulima masikini, yeye ni PM kwa miaka kadhaa sasa.

Kwa hiyo kusema mtoto wa mkulima hawezi kupata 10 million kila mwaka si sawa. Na hatujui Pinda atapata wapi hizi hela, si lazima zitoke mfukoni mwake, anaweza kuanzisha mfuko or something like that.

Hizo hela mbona ni kujinyima extravagances za safari moja tu ? Wakiamua hawa wanajenga Chuo Kipya kabisa, achilia mbali kuboresha makazi ya hiki kilichopo.
 
Mazee hakuna aliyesema kutoa milioni kumi kila mwaka kunamzui mtu kutafuta permanent solution. Kama serikali inashindwa kupata permanent solution, isemeni kwa kukosa permanent solution, sio kumuandama Pinda kwa sababu kaleta challenge ya watu kuchangia vyuo walivyohitimu, kitu kinachofanyika dunia nzima.

Kaka hujui kuwa pinda ndio serikali? ndio maana tunasema its wrong for him to introduce such an idea.
 
Ok Mimi siko tofauti na Pinda nakubali wewe hauko tofauti na nani au uko sawa na nani ? Kesho akichangia Yatima utasemaje? Before u criticise someone walk a mile on his shoes.

Ebu sema serikali au Pinda inatakiwa kufanya nini kuhusu tatizo la Malazi UDSM.hii ni kazi ya Uongoi wa UDSM wenyewe. Kuna mipaka.

Inabidi tuulizane pia, wanaomshutumu Pinda wamechangia nini?
 
Kaka hujui kuwa pinda ndio serikali? ndio maana tunasema its wrong for him to introduce such an idea.

Nimesema hapo juu Pinda ana lawama za serikali, lakini hilo halimaanishi kwamba kupromote philanthropy kushutumiwe.

Moja ya sababu huduma zetu za jamii zinazorota ni kwamba watu wanategemea serikali kwa kila kitu, hawachangii, hawalipi kodi, wanasubiri serikali itoe tu.

Sasa Pinda kaonyesha kuna sehemu ya watu binafsi kuchangia pia, mbali na serikali. Nothing wrong with that.

Na hakusema kwa kutoa milioni kumi ananunua kutoulizwa maswali kuhusu suluhisho lingine la kimsingi zaidi.
 
Ok Mimi siko tofauti na Pinda nakubali wewe hauko tofauti na nani au uko sawa na nani ? Kesho akichangia Yatima utasemaje? Before u criticise someone walk a mile on his shoes.

Ebu sema serikali au Pinda inatakiwa kufanya nini kuhusu tatizo la Malazi UDSM.hii ni kazi ya Uongoi wa UDSM wenyewe. Kuna mipaka.

UDSM wana serikali yao? Kaka pinda hakutakiwa kutoa pesa zake pale alichotakiwa ni kukaa na uongozi wa udsm na kujadili ili kupata permanent solution sasa milioni kumi inatosha nini kama sio kuongeza ufisadi tu. Zitamfikia nani? ni msaada ambao uko verge
 
Nimesema hapo juu Pinda ana lawama za serikali, lakini hilo halimaanishi kwamba kupromote philanthropy kushutumiwe.

Moja ya sababu huduma zetu za jamii zinazorota ni kwamba watu wanategemea serikali kwa kila kitu, hawachangii, hawalipi kodi, wanasubiri serikali itoe tu.

Sasa Pinda kaonyesha kuna sehemu ya watu binafsi kuchangia pia, mbali na serikali. Nothing wrong with that.

Angekaa na watu hao wangeweza hata kujenga majengo na sio mil 10 tu.
 
Inabidi tuulizane pia, wanaomshutumu Pinda wamechangia nini?

Tatizo watu sometime tunakuwa na unreliastic expectation . No wonder hata CHADEMA ingekuwa ikulu watu kama Johnsecond wangekuwa ni kuponda tu .
 
Kazi ipoooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
 
Back
Top Bottom