Hili la NBC Je Huu si Udini Jamani?

Mzalendo_Mkweli

JF-Expert Member
Jan 30, 2012
1,985
1,166
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua kampeni ya miezi miwili na nusu kwa ajili ya wateja wake wa huduma za kibenki zinazofuata sheria za Kiislamu, ili kupata washindi wawili watakao kwenda kuhiji Makkah Oktoba mwaka huu kwa kulipiwa kila kitu na benki hiyo.

___________________________________________________________________________________________

Nadhani kwa hali ya kidini iliyopo nchini kwa sasa, NBC hawakutumia BUSARA kuendesha hili zoezi kwa sasa.NBC ina wateja mchanganyiko WAISLAM na WASIO waislamu SASA kama mshindi atakuwa si MWISLAMU, je naye atagharimiwa kwenda ROMA, Israel au INdia AU KWINGINEKO? Je ikitokea Bank inayoendeshwa kwa utaratibu wa kibuda, Kikikristo au ya wasio na dini, hiyo Bank itaruhusu KWELI taratibu kama hizi za NBC bila kuzingatia matakwa ya wateja wasio wa Imani hiyo.Nawakilisha.Ahsante
 
Mi navyojua islamic banking ni kwa wale wanaokubaliana na system hiyo.hata kama utakua si wadini hiyo na ukashinda sidhani kama watakulazimisha uende maka kuhiji,nadhani vigezo lazima uwe mtu wa dini hiyo.
Jamaa wanajua waislam wengi ndo wafanyabiashara wakubwa wakatarget soko.
 
Kukosa maarifa ni mzigo, sasa unataka wawape wakristu zawadi ya kuhij Makkah?
Malalamiko mengine hayana hata mantiki

Wenzio wanawaza kuongeza wateja wa sharia account, wewe unalalama na udini.
 
Usijibu kwa hamaki mheshimiwa. Unajua NBC wana watu wa media wanaofuatilia kurasa kama hizi , hivyo maoni ya wachangiaji yanaweza kuwafumbua macho. Ahsante
Hili swali unatakiwa uiulize benki inayohusika.

Kuleta thread kama hii hapa ni kutafuta uchochezi usiokufaidisha wewe wala wananchi
 
Naomba nikae kimya juu ya uliyoandika.Ahsante
Mi navyojua islamic banking ni kwa wale wanaokubaliana na system hiyo.hata kama utakua si wadini hiyo na ukashinda sidhani kama watakulazimisha uende maka kuhiji,nadhani vigezo lazima uwe mtu wa dini hiyo.
Jamaa wanajua waislam wengi ndo wafanyabiashara wakubwa wakatarget soko.
 
Nimekusamehe kwa matusi yako.Ahsante
Kukosa maarifa ni mzigo, sasa unataka wawape wakristu zawadi ya kuhij Makkah?
Malalamiko mengine hayana hata mantiki

Wenzio wanawaza kuongeza wateja wa sharia account, wewe unalalama na udini.
 
NA je CRDB kuwamwagia mapesa wakatoliki kujenga kitega uchumi pale Msasani huoni huo nao ni udini? Acheni uchochezi nyie! wakifanyiwa maprotestants ni sawa waislamu udini?! mna kazi kweli kweli !
Wamewapa kama wateja I hope ni mkopo!Na sidhani kama ata mkopo hutolewa kwa misingi ya dini?
Ilo la NBC sidhani kama kuna shida maana Kuna Islamic Banking ambayo wakristu hawana na kwa kuwa kuna suala la kwnda hiji ambalo ni la msingi kwa waislamu unlike wakristu then wakaona waliunganishe na ilo
 
NA je CRDB kuwamwagia mapesa wakatoliki kujenga kitega uchumi pale Msasani huoni huo nao ni udini? Acheni uchochezi nyie! wakifanyiwa maprotestants ni sawa waislamu udini?! mna kazi kweli kweli !
Tafadhali futa kauli yako pale msasani si wakatoliki ni KKKT, nyie watu mna tatizo gani na wakatoliki, mkristo akifanya lolote mnarukia ukatoliki tu
 
Kukopa Bank ni ruksa kwa mtu binafsi, Taasisi za kidini, mashirika yasiyo ya kiserikali nk
NA je CRDB kuwamwagia mapesa wakatoliki kujenga kitega uchumi pale Msasani huoni huo nao ni udini? Acheni uchochezi nyie! wakifanyiwa maprotestants ni sawa waislamu udini?! mna kazi kweli kweli !
 
Pole, lakini ndio hivyo

Kila biashara lazima ujue jinsi ya kuongeza wateja, ukizubaa biashara itakufa

Na usikubali kuwa upande wa kulalamika tu, waweza jifunza toka NBC, ukaanzisha mgahawa, ukiona noah haitoki ukatoa zawadi ya kutembelea shamba la noah pale kilimanjaro kwa wateja wako wa noah wataoshinda.

Kila kitu ukikiangalia hasi, utaona hasi tu bila kujali hali halisi. Je hakuna chanya kwenya jambo hilo?

Nimekusamehe kwa matusi yako.Ahsante
 
Wapendwa kwa mtazamo wangu: Naamini hii ni mbinu za kibiashara only, Kwani ukitafakari utaona Matangazo ya biashara mbalimbali hushiriki katika namna ya kuwachota wateja..Mfano shirika la ndege likitangaza kuwa Mwenye kuchukuwa tiketi ya kusafiri katika kipindi fulani tutampa nyongeza mileage au usafiri wabure wakwenda hija/world cup/ Dubai festival nk.
" Ukweli kwa muumini wa kiislamu hana haja ya kuchukuwa pembejeo au faida ya Benki kwa kuifanyia ibadaa" kwa sababu
nyongeza za benki ni RIBA'a (interest) an RIBAA ni haramu" kwa hiyo Muisilamu hatumii fedha za haramu kuhijia.... anahitaji atumie PURE rasilimali ilokuwa safi kwa ibadaa yake ya Hija. MwenyEzzi Mungu hahitaji uchafu wala hana haja ya mali iliyokuwa na chembe cha haramu, Hapokei ila liloSafi na Muruwa na Tayibu. Kwa sababu MwenyEzzi mungu hakulazimishi uende Hija ila kwa uwezo wako na halali ya mali yako. Allah atukubalie machache yetu kwani bado tunaupungufu na kasoro zetu.AMIN
 
Kongosho naomba ukumbuke historia ya NBC.Hizi taratibu za Sharia zilianzishwa miaka si mingi na hivyo ziliwakuta wateja wa imani mbali mbali.Je, hili jambo liliwekwa wazi kwa Stakeholder wote na wakalikubali? Lets look this matter from different angles.Ahsante
Pole, lakini ndio hivyo

Kila biashara lazima ujue jinsi ya kuongeza wateja, ukizubaa biashara itakufa

Na usikubali kuwa upande wa kulalamika tu, waweza jifunza toka NBC, ukaanzisha mgahawa, ukiona noah haitoki ukatoa zawadi ya kutembelea shamba la noah pale kilimanjaro kwa wateja wako wa noah wataoshinda.

Kila kitu ukikiangalia hasi, utaona hasi tu bila kujali hali halisi. Je hakuna chanya kwenya jambo hilo?
 
Lakini wao jamaa wa NBC hawaoni athari ya hii promotion? Ahsante
Wapendwa kwa mtazamo wangu: Naamini hii ni mbinu za kibiashara only, Kwani ukitafakari utaona Matangazo ya biashara mbalimbali hushiriki katika namna ya kuwachota wateja..Mfano shirika la ndege likitangaza kuwa Mwenye kuchukuwa tiketi ya kusafiri katika kipindi fulani tutampa nyongeza mileage au usafiri wabure wakwenda hija/world cup/ Dubai festival nk.
" Ukweli kwa muumini wa kiislamu hana haja ya kuchukuwa pembejeo au faida ya Benki kwa kuifanyia ibadaa" kwa sababu
nyongeza za benki ni RIBA'a (interest) an RIBAA ni haramu" kwa hiyo Muisilamu hatumii fedha za haramu kuhijia.... anahitaji atumie PURE rasilimali ilokuwa safi kwa ibadaa yake ya Hija. MwenyEzzi Mungu hahitaji uchafu wala hana haja ya mali iliyokuwa na chembe cha haramu, Hapokei ila liloSafi na Muruwa na Tayibu. Kwa sababu MwenyEzzi mungu hakulazimishi uende Hija ila kwa uwezo wako na halali ya mali yako. Allah atukubalie machache yetu kwani bado tunaupungufu na kasoro zetu.AMIN
 
NBC wana haki ya kuongeza products zao as long as haziwazuii wateja wengine kufanya shughuli zao

Sijaona tatizo hadi sasa

Kongosho naomba ukumbuke historia ya NBC.Hizi taratibu za Sharia zilianzishwa miaka si mingi na hivyo ziliwakuta wateja wa imani mbali mbali.Je, hili jambo liliwekwa wazi kwa Stakeholder wote na wakalikubali? Lets look this matter from different angles.Ahsante
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom