Hili la Mwenge Waziri Liweke Vizuri. Ni Kero kwa walimu

Mar 7, 2014
47
6
Nianze kwa kusema nawapa Tano wabunge wa upinzani kwa utetezi wao wa wanyonge hasa sisi walimu. Ukweli tunanyanyaswa na mchango huo wa mwenge. Niwape historia fupi kuwa mimi ni mwalimu wa hapa MISUNGWI MWANZA. Mwaka jana nilikuwa mwl Mkuu lakini nilivuliwa madaraka kwa kukataa kutoa mchango wa mwenge. Ninao ushaidi nina barua ya kunivua madaraka na Sababu imeandikwa pia Kwenye log book imeandikwa. Hivyo nathubutu kusema mheshiwa Lukuvi na Wazirikuu wamelidanganya bunge kusema hawalazimishwi kutoa huo ni uongo kabisa. Watanzania wenzangu ukweli ndo huo mimi sasa na mwl wa kawaida mwenge umenitosa madaraka yangu. Mchango wenu tafadhari.
 
Pole sana,ila kwakuwa umetambua mchango wa wapinzani basi mwakani tuwape nafasi kama india wameweza nasisi tunaweza.
 
Nianze kwa kusema nawapa Tano wabunge wa upinzani kwa utetezi wao wa wanyonge hasa sisi walimu. Ukweli tunanyanyaswa na mchango huo wa mwenge. Niwape historia fupi kuwa mimi ni mwalimu wa hapa MISUNGWI MWANZA. Mwaka jana nilikuwa mwl Mkuu lakini nilivuliwa madaraka kwa kukataa kutoa mchango wa mwenge. Ninao ushaidi nina barua ya kunivua madaraka na Sababu imeandikwa pia Kwenye log book imeandikwa. Hivyo nathubutu kusema mheshiwa Lukuvi na Wazirikuu wamelidanganya bunge kusema hawalazimishwi kutoa huo ni uongo kabisa. Watanzania wenzangu ukweli ndo huo mimi sasa na mwl wa kawaida mwenge umenitosa madaraka yangu. Mchango wenu tafadhari.

pole kamanda kweli waalimu kwa upande mwingine tunateswa kwa kutojitambua huku kwetu mbeya tulikataa kulipa ila tukalazimishwa kusimama njiani ukipita wenye msimamo hawakwenda watu walikaa kuanzia saa 4 asbh mwenge ukapita saa 9 alasiri
 
Peter pole sana ila ninakusifu kwa uwezo wako mkubwa wa kujiamin hasa hata pale unapokuwa na madaraka flan huogopi kuvuliwa,endelea hivyo hivyo,utakuwa kiongoz mzur baadae
 
Pole sana ;;unaonekana wewe sio mzalendo na huna imani na nchi yako kabisa ,,kwani ungechanga kungekuathiri nini
 
Pole kwa yaliyo kupata, serikali yetu kila mwanasiasa mbabe, hata mwenyekiti wa mtaa anaweza kukukoromea mwalimu mkuu ukawa mdogo kama pilton! Ila najua kama ulionewa malipo hapa hapa duniani, watalipwa na mtoa hukumu wewe kaa kimya na omba Mola atuokoe 2015.
 
Inategemea na msimamo wako bwana, mm nlishakataa mara nyingi kuchangia na nna dunda bila tabu
 
Back
Top Bottom