Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,489
- 13,608
Kuna video moja fupi inazunguka mitandaoni anaonekana mbunge wa baraza la wawakilishi akiwaongelea kwa dharau samaki wa Ziwa Victoria. Anasema wao kwa maana ya watu wa visiwani hawana utamaduni wa kula samaki wa aina hiyo, kwamba isitokee mbegu zao zikawekwa kwenye bahari iliyo karibu na visiwa vya Unguja na Pemba!.
Hii ni kebehi mbovu sana, ina maana watu wa visiwani wanaoishi kule mikoa ya Ziwa Victoria hawali samaki wanaovuliwa kutoka kwenye maji yale!!?. Huku kujiona wa maana kunakojionyesha katika maneno ya yule mheshimiwa kunaleta taswira ya dharau kwa jamii pana ya Tanzania.
Waunguja na wapemba tumeishi nao tangu utoto mwetu, tukasoma nao vyuo vikuu na kufanya nao kazi. Na ninao uhakika vyakula vingi vinavyolisha visiwa hivyo na vile vya Comoro vinatoka huku Bara. Ni mazao yanayolimwa na wakulima wa mikoa ya Bara. Kama familia moja ya Kiembesamaki au Mwanakwerekwe inaweza kula wali unaotokana na mchele wa Mbeya lipi la hatari kwa afya ya familia hiyo iwapo itakula samaki wa maji baridi?.
Mbunge huyo wa baraza la wawakilishi kwa lugha ya kweli isiyo ya kuremba ni kwamba ameropoka, tena bila ya kujua madhara ya kauli yake. Alipaswa kutumia aina ya maneno yasiyoleta ukakasi kwa wavuvi wa Ziwa Victoria na wakazi mamilioni wanaoishi maeneo ya kanda ile. Wabunge kutoka Zanzibar wanaoingia ndani ya bunge la Jamhuri wanakula kila aina ya vyakula ambavyo baadhi vinalimwa na wakulima wa kanda ya Ziwa.
Wapo wazanzibari wengi tu waliokuzwa na Sato pamoja na Sangara kule kanda ya Ziwa, wanaujua utamu wa samaki hao. Hivyo mbunge yule atahadharishwe tu na waungwana kwamba kauli yake ndani ya kikao cha baraza la wawakilishi, inaweza kuwa imekera watu.
Hii ni kebehi mbovu sana, ina maana watu wa visiwani wanaoishi kule mikoa ya Ziwa Victoria hawali samaki wanaovuliwa kutoka kwenye maji yale!!?. Huku kujiona wa maana kunakojionyesha katika maneno ya yule mheshimiwa kunaleta taswira ya dharau kwa jamii pana ya Tanzania.
Waunguja na wapemba tumeishi nao tangu utoto mwetu, tukasoma nao vyuo vikuu na kufanya nao kazi. Na ninao uhakika vyakula vingi vinavyolisha visiwa hivyo na vile vya Comoro vinatoka huku Bara. Ni mazao yanayolimwa na wakulima wa mikoa ya Bara. Kama familia moja ya Kiembesamaki au Mwanakwerekwe inaweza kula wali unaotokana na mchele wa Mbeya lipi la hatari kwa afya ya familia hiyo iwapo itakula samaki wa maji baridi?.
Mbunge huyo wa baraza la wawakilishi kwa lugha ya kweli isiyo ya kuremba ni kwamba ameropoka, tena bila ya kujua madhara ya kauli yake. Alipaswa kutumia aina ya maneno yasiyoleta ukakasi kwa wavuvi wa Ziwa Victoria na wakazi mamilioni wanaoishi maeneo ya kanda ile. Wabunge kutoka Zanzibar wanaoingia ndani ya bunge la Jamhuri wanakula kila aina ya vyakula ambavyo baadhi vinalimwa na wakulima wa kanda ya Ziwa.
Wapo wazanzibari wengi tu waliokuzwa na Sato pamoja na Sangara kule kanda ya Ziwa, wanaujua utamu wa samaki hao. Hivyo mbunge yule atahadharishwe tu na waungwana kwamba kauli yake ndani ya kikao cha baraza la wawakilishi, inaweza kuwa imekera watu.