Hili la maiti kulipishwa madeni Hospitali za Serikali limekaaje?

Nuraty J

JF-Expert Member
Sep 18, 2018
1,729
3,829
Habarini wapendwa,

Wiki hii mzee wetu alikuwa anaumwa Hernia, tarehe 07/11/2019 tukampeleka Mloganzila hospital akitokea hospitali ya Bagamoyo, kufika kule usiku akafanyiwa upasuaji, saa kumi alfajiri akafariki. Sasa tarehe 08/11/2019 tukaenda ili kuchukua mwili wa marehemu akazikwe.

Kufika pale tunaambiwa marehemu anadaiwa jumla ni Tsh 775,000/= tukalalamika mbona hela nyingi hivyo, wakatuambia nendeni ustawi wa jamii labda wanaweza kuwasaidia mkilalamika kuwa hamna uwezo, kwenda kule tukaambiwa kuwa hata iko kiasi mlichotajiwa kapewa punguzo sababu katokea hospitali ya Serikali kuja hapa, kukosa hivyo ingekuwa mara mbili yake.

Tukasema sawa, ndugu wakachangishana ikafika laki sita na ishirini, kuipeleka kule bado wakagoma, wakasema hadi hela itimie yote isipungue hata mia ndo maiti itatoka, basi tukapigia simu watu baki kuwakopa hela ikatimia tukaenda kupeleka tukapewa mwili wa marehemu. Sasa najiuliza hivi huu utaratibu wa kudai maiti ni haki kweli? Mtu amekufa bado mnamdai, sio laana kweli.

Kuna wapemba tumewakuta wanadaiwa milioni tatu za maiti wao, wameshauriana waende wakafanye kisomo cha kuswalia maiti pale hospitali, wakimaliza waondoke mwili wauache pale pale Mloganzila, wao wataisabu kama ndugu yao amekufia baharini na maiti haikupatikana kuliko kulipa hela hiyo.

Hii ni kweli jamani wala sio jambo la kutunga, marehemu katuachia madeni.

Zaidi, soma:




 
Poleni sana. Hospitali nyingi kubwa nilichogundua, matibabu kwa kutumia bima ya afya ni rahisi kuliko kulipa Cash. Kunakipimo kwa kutumia bima ni 300,000 na kama huna bima ni 400,000, na hii ipo kwenye vipimo vyote mpaka gharama za dawa.
 
Watanzania vichwa vizito sana.

Mngeambiwa mlipe kwanza ndio mgonjwa ahudumiwe pia mngelalamika kwamba wamegoma kumhudumia mgonjwa wetu kisa hatuna pesa mpaka akafariki.

Haya, wamefanya ubinaadamu wakampa mgonjwa huduma kabla hamjalipia chochote then kwa kuwa bahati mbaya kafariki eti mnataka msilipe? Does it sound kweli?

Kwa hizi mentality za kijinga za watz ndio maana private hospital HAWAKUPI HUDUMA MPAKA ULIPE. Unalipa kwanza ndio unapewa huduma. Kama hujalipa mgonjwa atakufa huku wanamwangalia.


Unforgetable
 
Kuna Mzee mmoja, aliyefiwa na wake zake wawili pale, hataki hata kuisikia hiyo hospitali. Kwanza anaikosea hata jina na kuiita Mgoganzila. Nirudi kwenye mada, Serikali ilitazame suala hili kwa jicho la huruma. Wananchi wanakimbilia hospitali za Serikali wakiamini kuwa kuna nafuu ya gharama za matibabu. Lakini, Mloganzila inatajwa sana kama hospitali ghali hasa panapotokea kifo. Marehemu wengi huchangiwa ili angalau kuupata mwili wake. Kuna jambo la kufanyika pale!

manengelo nifikishie pole zangu kwa Mina cute
 
Kuna Mzee mmoja, aliyefiwa na wake zake wawili pale, hataki hata kuisikia hiyo hospitali. Kwanza anaikosea hata jina na kuiita Mgoganzila. Nirudi kwenye mada, Serikali ilitazame suala hili kwa jicho la huruma. Wananchi wanakimbilia hospitali za Serikali wakiamini kuwa kuna nafuu ya gharama za matibabu. Lakini, Mloganzila inatajwa sana kama hospitali ghali hasa panapotokea kifo. Marehemu wengi huchangiwa ili angalau kuupata mwili wake. Kuna jambo la kufanyika pale!

manengelo nifikishie pole zangu kwa Mina cute
asnte, kwakweli ni hatari aswaa,
 
Watanzania vichwa vizito sana.

Mngeambiwa mlipe kwanza ndio mgonjwa ahudumiwe pia mngelalamika kwamba wamegoma kumhudumia mgonjwa wetu kisa hatuna pesa mpaka akafariki.

Haya, wamefanya ubinaadamu wakampa mgonjwa huduma kabla hamjalipia chochote then kwa kuwa bahati mbaya kafariki eti mnataka msilipe? Does it sound kweli?

Kwa hizi mentality za kijinga za watz ndio maana private hospital HAWAKUPI HUDUMA MPAKA ULIPE. Unalipa kwanza ndio unapewa huduma. Kama hujalipa mgonjwa atakufa huku wanamwangalia.


Unforgetable

Omba Mungu ikukute wewe uwe na mgonjwa halafu huna pesa za kumtibu uone ujinga wa Watanzania kwa ukaribu.
 
Watanzania vichwa vizito sana.

Mngeambiwa mlipe kwanza ndio mgonjwa ahudumiwe pia mngelalamika kwamba wamegoma kumhudumia mgonjwa wetu kisa hatuna pesa mpaka akafariki.

Haya, wamefanya ubinaadamu wakampa mgonjwa huduma kabla hamjalipia chochote then kwa kuwa bahati mbaya kafariki eti mnataka msilipe? Does it sound kweli?

Kwa hizi mentality za kijinga za watz ndio maana private hospital HAWAKUPI HUDUMA MPAKA ULIPE. Unalipa kwanza ndio unapewa huduma. Kama hujalipa mgonjwa atakufa huku wanamwangalia.


Unforgetable
Fact. Tubadilike, tuache kulialia. Huduma zinalipiwa, hili liko wazi.
 
Back
Top Bottom