Hili la kupulizia kinga ya Dengue Mabasi ya mikoani ni siasa pofu!

SHILINDE

Member
Jul 23, 2010
14
6
Taifa lolote duniani linapopatwa na majanga na dharula serikali yake inapaswa kusimamia kifua mbele. Tanzania tumepatwa na ugonjwa wa Dengue ambapo serikali katika kutimiza jukumu lake la kukinga na kuzuia maambukizi yasiwapate watanzania ikabidi kuamuru mabasi yote yanayoenda mikoani kupuliziwa dawa ya kinga (fumigation) sasa kinachotokea ni kutupiana mpira kati ya serikali na wamiliki wa vyombo vya usafiri juu ya gharama za dawa hizo.

Busara ndogo na sahihi hapa ni kwamba Serikali iwajibike na ichukuwe jukumu hilo na si kuwabambika wamiliki wa mabasi kwa sababu kubwa zifuatazo,
1. ni jukumu la serikali kuzuia/kukinga wananchi wake kwenye majanga
2. wamiliki wa mabasi hawahusiki katika kupelekea/kuzalisha mbu wanaoambukiza dengue, ingepasa waombwe na si kuamuriwa kama ilivyo sasa

Natoa hoja.


Iko hivi: wamiliki wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri DSM walikutana na mkuu wa mkoa wa Dsm pamoja na SUMATRA na wakakubaliana kwamba wafanye fumigation ndani ya mabasi hayo kwa hiyari.

Leo, Afisa Mfawaidhi wa Sumatra kanda ya Mashariki Condrad Shio amesema kwamba mpaka kufika jana saa mbili na robo usiku, takribani mabasi 580 Yamekwisha puliziwa dawa hizo za homa ya dengi.

Na si mabasi yote yaendayo mikoani yatahusika na zoezi hilo..La Hasha! bali ni mabasi yatoayo huduma kwa mikoa ya Dsm, Morogoro, Lindi na Mtwara..Zoezi lote hadi hivi sasa Serikali inaligharimia na wala si kweli kwamba kuna kutupiana mpira!

Sosi-Mimi Mwenyewe!
 
Taifa lolote duniani linapopatwa na majanga na dharula serikali yake inapaswa kusimamia kifua mbele. Tanzania tumepatwa na ugonjwa wa Dengue ambapo serikali katika kutimiza jukumu lake la kukinga na kuzuia maambukizi yasiwapate watanzania ikabidi kuamuru mabasi yote yanayoenda mikoani kupuliziwa dawa ya kinga (fumigation) sasa kinachotokea ni kutupiana mpira kati ya serikali na wamiliki wa vyombo vya usafiri juu ya gharama za dawa hizo.

Busara ndogo na sahihi hapa ni kwamba Serikali iwajibike na ichukuwe jukumu hilo na si kuwabambika wamiliki wa mabasi kwa sababu kubwa zifuatazo,
1. ni jukumu la serikali kuzuia/kukinga wananchi wake kwenye majanga
2. wamiliki wa mabasi hawahusiki katika kupelekea/kuzalisha mbu wanaoambukiza dengue, ingepasa waombwe na si kuamuriwa kama ilivyo sasa

Natoa hoja.


Iko hivi: wamiliki wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri DSM walikutana na mkuu wa mkoa wa Dsm pamoja na SUMATRA na wakakubaliana kwamba wafanye fumigation ndani ya mabasi hayo kwa hiyari.

Leo, Afisa Mfawaidhi wa Sumatra kanda ya Mashariki Condrad Shio amesema kwamba mpaka kufika jana saa mbili na robo usiku, takribani mabasi 580 Yamekwisha puliziwa dawa hizo za homa ya dengi.

Na si mabasi yote yaendayo mikoani yatahusika na zoezi hilo..La Hasha! bali ni mabasi yatoayo huduma kwa mikoa ya Dsm, Morogoro, Lindi na Mtwara..Zoezi lote hadi hivi sasa Serikali inaligharimia na wala si kweli kwamba kuna kutupiana mpira!

Sosi-Mimi Mwenyewe!
 
Iko hivi: wamiliki wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri DSM walikutana na mkuu wa mkoa wa Dsm pamoja na SUMATRA na wakakubaliana kwamba wafanye fumigation ndani ya mabasi hayo kwa hiyari.

Leo, Afisa Mfawaidhi wa Sumatra kanda ya Mashariki Condrad Shio amesema kwamba mpaka kufika jana saa mbili na robo usiku, takribani mabasi 580 Yamekwisha puliziwa dawa hizo za homa ya dengi.

Na si mabasi yote yaendayo mikoani yatahusika na zoezi hilo..La Hasha! bali ni mabasi yatoayo huduma kwa mikoa ya Dsm, Morogoro, Lindi na Mtwara..Zoezi lote hadi hivi sasa Serikali inaligharimia na wala si kweli kwamba kuna kutupiana mpira!

Sosi-Mimi Mwenyewe!
Mkuu vipi kuhusu Meli na boti ziendazo Zanzibar? mia
 
Mh amechomokea kipande hicho leo asubuhi wakati akitaka kuuliza swali la nyongeza na akachombeza kwamba ikiwa hilo ni basi moja vipi mtz anayetaka kupuliza nyumba yake?

..............yaani hakuna aliyeonekana kustuka kabisa na hili.....

Ama kweli kufa kufaana

chanzo: TBC TV na siikio langu
 
Wenye mabasi wanachajiwa 65000. Receipt imeandikwa 1000-MANI JF PHOTO
 
Iko hivi: wamiliki wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri DSM walikutana na mkuu wa mkoa wa Dsm pamoja na SUMATRA na wakakubaliana kwamba wafanye fumigation ndani ya mabasi hayo kwa hiyari.

Leo, Afisa Mfawaidhi wa Sumatra kanda ya Mashariki Condrad Shio amesema kwamba mpaka kufika jana saa mbili na robo usiku, takribani mabasi 580 Yamekwisha puliziwa dawa hizo za homa ya dengi.

Na si mabasi yote yaendayo mikoani yatahusika na zoezi hilo..La Hasha! bali ni mabasi yatoayo huduma kwa mikoa ya Dsm, Morogoro, Lindi na Mtwara..Zoezi lote hadi hivi sasa Serikali inaligharimia na wala si kweli kwamba kuna kutupiana mpira!

Sosi-Mimi Mwenyewe!

Mkuu mbona kuna mvutano asubuhi kwenye kipindi east africa redio wamiliki walikuwa wanalalamika kutozwa 65000 na receipt kuandikwa 1000.
 
Ni kama moto umeanza kuwaka katika store ya kuhifadhia mbao ambapo mbao chache tayari zimeshika moto,sasa kinachofanywa na waokoaji ni kuangaika kuuzima moto na Ndoo za michanga badala ya kutoka nnje mbao ambazo hazijashika moto, ili moto usindelee kuwa mkubwa.
 
Mkuu mbona kuna mvutano asubuhi kwenye kipindi east africa redio wamiliki walikuwa wanalalamika kutozwa 65000 na receipt kuandikwa 1000.

Kwa bahati mbaya sina taarifa kuhusu hilo..ndio kwanza unaijuza!
 
Iko hivi: wamiliki wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri DSM walikutana na mkuu wa mkoa wa Dsm pamoja na SUMATRA na wakakubaliana kwamba wafanye fumigation ndani ya mabasi hayo kwa hiyari.

Leo, Afisa Mfawaidhi wa Sumatra kanda ya Mashariki Condrad Shio amesema kwamba mpaka kufika jana saa mbili na robo usiku, takribani mabasi 580 Yamekwisha puliziwa dawa hizo za homa ya dengi.

Na si mabasi yote yaendayo mikoani yatahusika na zoezi hilo..La Hasha! bali ni mabasi yatoayo huduma kwa mikoa ya Dsm, Morogoro, Lindi na Mtwara..Zoezi lote hadi hivi sasa Serikali inaligharimia na wala si kweli kwamba kuna kutupiana mpira!

Sosi-Mimi Mwenyewe!

Kwa hiyo Mbu akiona basi la Dar-Mwanza anajishukia anatafuta ya mikoa hiyo!!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom