Hili la kuongea/kusikiliza kero za wananchi namuunga mkono Mkuu wa Mkoa wa Dar

Do santos

JF-Expert Member
Feb 7, 2011
635
337
Habari wadau.
Naangalia kituo cha Televisheni cha Clouds TV kuna kipindi kinarushwa Live ambacho ni mkutano
wa Mkoa wa dar es salaam Ndugu Paul Makonda na wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam Wilaya ya kinondoni kata ya Tandale kwa Tumbo.

Nimefurahi kuona wananchi wanapata fursa ya kutoa kero zao na wengine kutoa ushauri. Na baadhi ya malamiko yanatolewa majibu kutoka kwa wahusika wa ngazi mbalimbali.

Sehemu kubwa majibu yake yanapatikana ambayo kwa muda mrefu hayakuwa yanapata majibu aidha kwa kwa uzembe au kuna harufu ya rushwa.

Ni jambo zuri na la kuigwa. Aina hii ya kuonana na wananchi moja kwa moja na kusikiliza kero zao ni jambo zuri na linalovunja wigo wa viongozi wajanja wanaotengeneza ugumu wa kuwasaidia wananchi katika kupata haki zao wanazodhulumiwa na wenye pesa.

Kesi mbili za malalamiko ya ardhi nimeona zimepata ufumbuzi kutoka kwa wahusika ambao katika wakati wote hawakuweza kutoa haki kwa wahusika.

Ni jambo la kumpongeza mkuu wa mkoa kwa kazi nzuri anayoifanya. Kwa hili namuunga mkono
aendelee kukutana na wananchi kutatua kero zao.
 
Naona Ufumbuzi na haki kwa wanyonge unapatikana Papo kwa hapo. Ni jitihada njema.
 
Ni jba ja ila kama una mtindio wa ubongo utapinga tu jakuna namna nyingine
 
Hili ni muhimu sana,
kero zinapata ufumbuzi.
Wenye mamlaka wanalazimika kutenda haki
hata kama walishakula kitu kidogo.
Naona Ufumbuzi na haki kwa wanyonge unapatikana Papo kwa hapo. Ni jitihada njema.
 
Nampongeza pia, ni jambo jema sana. Watu wana kero nyingi na mamlaka husika zimekaa kimya tu.
 
Hili ni jambo jema ambalo hata Mhe Rais analiunga mkono pamoja na wananchi,na hata wakati anatoa ufafanizi wa kutanua barabara ya Morogoro,kutoka Ubungo kuelekea Chalinze aliwaasa wakuu wa mikoa wengine waige mfano huo,kama unaona kuiga style hiyo si vyema basi amuru wakuu wako wa wilaya wafanye hivyo,then ww ufanye monitoring and supervision kwani wananchi wana matatizo mengi ambayo mengine yanaweza kupatiwa majibu nje ya ofisi,na hili limefanya wananchi kumfahamu mkuu wa mkoa wakati hata wakati mwingine DC wao hawamjui,ni wakati sasa wakuu wa mikoa na wa wilaya wawafikie wananchi wanakoishi,wasisubiri mpaka migogoro ipambe moto ndiyo waende kwa wananchi kwani kinga ni bora kuliko tiba.
 
Nimegundua huku mitaani watu wanakero lukuki, huenda vifo vingi vinachangiwa Na dhuluma ya viongozi wa serikali wakishirikiana Na matajiri wachache matapeli

Hongera Makonda, naamini ulikopita umepunguza kitu mioyoni mwa wananchi husika.
 
Back
Top Bottom