Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Wiki chache zilizopita ilizinduliwa kampeni kabambe ya kumchangia Tundu Lissu kupitia akaunti ya benki na kwenye mitandao ya simu.
Zoezi lilipokelewa kwa hisia kali na makamanda waliotaka wapiga kura milioni sita waliompigia Lowassa wachange kila mmoja angalau shilingi 1000.
Nakumbuka hamasa ilikuwa kubwa kabla Mbowe hajapata dhamana na mara alipotoka jela zoezi likafifia. Je, mkono wa chuma umepita?
Huenda wale wapiga kura milioni sita walikasirishwa na matusi na dhihaka za wafuasi wa Chadema dhidi ya Edward Lowassa na familia yake baada ya kurejea CCM. Ni dalili kuwa wananchi waliompigia kura Lowassa walihuzunika.
Je, hawa makamanda waliobaki mitandaoni aka "keyboard worriors" ni maneno matupu?
Nimetumia vyanzo vyangu kutoka benki husika na wamekiri kuwa hakuna chechote zaidi ya salio la kufungulia akaunti, kwenye mitandao ya simu nako ni ukame huenda ndio sababu Lissu kaamua kupambania hali yake kortini.
Ni dhahiri kishindo cha watu milioni sita kimeondoka kimyakimya, tujifunze kuweka akiba ya maneno.Ikumbukwe kipindi Lissu kapigwa risasi michango ilipatikana fasta bila shaka watu hawa milioni sita wameondoka na Lowassa.
Muda utatujibu, mambo mengi mno.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wiki chache zilizopita ilizinduliwa kampeni kabambe ya kumchangia Tundu Lissu kupitia akaunti ya benki na kwenye mitandao ya simu.
Zoezi lilipokelewa kwa hisia kali na makamanda waliotaka wapiga kura milioni sita waliompigia Lowassa wachange kila mmoja angalau shilingi 1000.
Nakumbuka hamasa ilikuwa kubwa kabla Mbowe hajapata dhamana na mara alipotoka jela zoezi likafifia. Je, mkono wa chuma umepita?
Huenda wale wapiga kura milioni sita walikasirishwa na matusi na dhihaka za wafuasi wa Chadema dhidi ya Edward Lowassa na familia yake baada ya kurejea CCM. Ni dalili kuwa wananchi waliompigia kura Lowassa walihuzunika.
Je, hawa makamanda waliobaki mitandaoni aka "keyboard worriors" ni maneno matupu?
Nimetumia vyanzo vyangu kutoka benki husika na wamekiri kuwa hakuna chechote zaidi ya salio la kufungulia akaunti, kwenye mitandao ya simu nako ni ukame huenda ndio sababu Lissu kaamua kupambania hali yake kortini.
Ni dhahiri kishindo cha watu milioni sita kimeondoka kimyakimya, tujifunze kuweka akiba ya maneno.Ikumbukwe kipindi Lissu kapigwa risasi michango ilipatikana fasta bila shaka watu hawa milioni sita wameondoka na Lowassa.
Muda utatujibu, mambo mengi mno.
Sent using Jamii Forums mobile app