The Sunk Cost Fallacy
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 19,586
- 14,137
Pamoja na Nia njema ya kuleta unafuu wa bei za mafuta/ petroli lakini njia ya kwenda Kukopa haifai.
Tulikubaliana kama Taifa tutakopa kwa ajili ya miradi ila sio kwa ajili ya kula na mambo kama hayo.
Kwa sasa Tanzania ina nafasi ya kukopesheka na ni fursa ya kuitumia kwa ajili ya kujengea miradi ya kimkakati ya kuchochea uchumi kama Bagamoyo Port,Liganga/ Mchuchuma,Magadi soda Engaruka nk lakini sio Kukopa Ili kulipia mafuta.
Serikali isipende kutafuta njia shortcut ambazo kesho zitaumiza uchumi na maisha ya watu.Nchi nyingi zinaumizwa na mikopo kama Zambia,Kenya,Ghana,Angola,Sri Lanka nk.
Serikali inaweza kabisa kutoa ruzuku kwa kupunguza gharama zake za utawala,kwa kufanya yafuatayo'
1. Kufuta au kupunguza kwa nusu ruzuku za vyama vya siasa.
2. Kuacha kununua Magari ya serikali yanayotumia mafuta mengi kama mashangingi kwa maofisa wake isipokuwa viongozi wa kitaifa tuu.
3. Kupunguza bajeti ya mafuta Kwa viongozi wa serikali maana yanatumika kwa binafsi kuliko kwa Kazi za serikali,na wengine huwa wanaenda kubadilisha kwenye vituo vya mafuta wanapewa pesa wanatafuna.
4. Kubadili mfumo wa magari ya serikali kuwa ya gas au umeme Ili kupunguza au kuacha kutumia mafuta..Hili hata watu binafsi wawekewe hii huduma ila lazima Serikali ionyeshe mfano.
4.Kupunguza au kufuta kabisa ile inayoitwa Mfuko wa Jimbo, yaani serikali inapeleka mabilioni kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya nini hasa?
5. Kupunguza mishahara,marupurupu nk kwa viongozi wote wa juu kuanzia kwa wakuu wa Idara na Taasisi hadi Kwa Rais wakiwemo Wabunge.
6.Kupunguza na kufuta mamikataba yasiyo na tija kwa mfano Ule wa Tanesco na wahindi kwa ajili ya software..
7.Kupunguza Utitiri wa Taasisi za serikali zinazofanya majukumu yanayofanana eg Sido,Tirdo,Temdo,NDC,CAMARTEC,Temesa,Brela,TanTrade,TIC,EPZA,Wakala wa vipimo,TBS,TBA,NHC,Watumishi Housing,Mzinga Corporation,FCC,FCT,NEEC ,kila wizara kuwa na chuo/ vyuo vyake huko kozi zinazofundishwa zipo pia kwenye vyuo vingine nk
7.Kukusanya Kodi stahiki kwa sababu TRA inazembea kukusanya na kubuni vyanzo vipya vya mapato..
Yaani haihitaji Kukopa wala kuondoa Kodi kwenye mafuta au kufuta vyanzo vya maendeleo kama Kodi za Tarura,TanRoads,Fuwasa na Reli..
Tukikomaa na hayo niliyoeleza hapo juu na mengine mtakayoongeza tutaokoa na kupata pesa nyingi sana zaidi ya bil.600 ambayo inaweza kutoa ruzuku walau kwa miezi 5- 7 wakati tunajipanga kwa hatua za mda mrefu.
Wananchi tuungane kupinga na kukataa kuchukua mkopo kwa ajili ya Ruzuku.👇
Tulikubaliana kama Taifa tutakopa kwa ajili ya miradi ila sio kwa ajili ya kula na mambo kama hayo.
Kwa sasa Tanzania ina nafasi ya kukopesheka na ni fursa ya kuitumia kwa ajili ya kujengea miradi ya kimkakati ya kuchochea uchumi kama Bagamoyo Port,Liganga/ Mchuchuma,Magadi soda Engaruka nk lakini sio Kukopa Ili kulipia mafuta.
Serikali isipende kutafuta njia shortcut ambazo kesho zitaumiza uchumi na maisha ya watu.Nchi nyingi zinaumizwa na mikopo kama Zambia,Kenya,Ghana,Angola,Sri Lanka nk.
Serikali inaweza kabisa kutoa ruzuku kwa kupunguza gharama zake za utawala,kwa kufanya yafuatayo'
1. Kufuta au kupunguza kwa nusu ruzuku za vyama vya siasa.
2. Kuacha kununua Magari ya serikali yanayotumia mafuta mengi kama mashangingi kwa maofisa wake isipokuwa viongozi wa kitaifa tuu.
3. Kupunguza bajeti ya mafuta Kwa viongozi wa serikali maana yanatumika kwa binafsi kuliko kwa Kazi za serikali,na wengine huwa wanaenda kubadilisha kwenye vituo vya mafuta wanapewa pesa wanatafuna.
4. Kubadili mfumo wa magari ya serikali kuwa ya gas au umeme Ili kupunguza au kuacha kutumia mafuta..Hili hata watu binafsi wawekewe hii huduma ila lazima Serikali ionyeshe mfano.
4.Kupunguza au kufuta kabisa ile inayoitwa Mfuko wa Jimbo, yaani serikali inapeleka mabilioni kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya nini hasa?
5. Kupunguza mishahara,marupurupu nk kwa viongozi wote wa juu kuanzia kwa wakuu wa Idara na Taasisi hadi Kwa Rais wakiwemo Wabunge.
6.Kupunguza na kufuta mamikataba yasiyo na tija kwa mfano Ule wa Tanesco na wahindi kwa ajili ya software..
7.Kupunguza Utitiri wa Taasisi za serikali zinazofanya majukumu yanayofanana eg Sido,Tirdo,Temdo,NDC,CAMARTEC,Temesa,Brela,TanTrade,TIC,EPZA,Wakala wa vipimo,TBS,TBA,NHC,Watumishi Housing,Mzinga Corporation,FCC,FCT,NEEC ,kila wizara kuwa na chuo/ vyuo vyake huko kozi zinazofundishwa zipo pia kwenye vyuo vingine nk
7.Kukusanya Kodi stahiki kwa sababu TRA inazembea kukusanya na kubuni vyanzo vipya vya mapato..
Yaani haihitaji Kukopa wala kuondoa Kodi kwenye mafuta au kufuta vyanzo vya maendeleo kama Kodi za Tarura,TanRoads,Fuwasa na Reli..
Tukikomaa na hayo niliyoeleza hapo juu na mengine mtakayoongeza tutaokoa na kupata pesa nyingi sana zaidi ya bil.600 ambayo inaweza kutoa ruzuku walau kwa miezi 5- 7 wakati tunajipanga kwa hatua za mda mrefu.
Wananchi tuungane kupinga na kukataa kuchukua mkopo kwa ajili ya Ruzuku.👇