MO11
JF-Expert Member
- Mar 23, 2014
- 18,857
- 38,605
kwa soka la bongo mkude ni patrick vieraKwani hata Jonas Mkude amefikia ukubwa huo?
kwa soka la bongo mkude ni patrick vieraKwani hata Jonas Mkude amefikia ukubwa huo?
Nenda kamshtaki CASJana nilipata nafasi ya kuzama Kambini kwa timu ya Taifa.
Nikiwa Bongo mara nyingi napenda kujibanza na watu wa soka ili kujua mambo mbalimbali ambayo kwa namna moja au nyingine siyatambui.
Kwa bahati nzuri/mbaya mwamba mmoja hivi kutoka pande za Msimbazi akaingi akiwa amependeza kinoma. Nadhani aliutumia vyema ule wakati wa alasiri wa siku ya jana kufanya yake.
Labda huenda alidhani ameonja kidogo na hakuna mtu angeshindwa kumtambua, kwa bahati mbaya mwana alionekana dhahiri hata na wachezaji wenzake kuwa Jey yuko pombe.
Mwalimu hakuweza kulitambua hilo mapema ila baadhi ya maafisa wa benchi la ufundi la Stars waliligundua hilo.
Nikaona Nadir Cannavaro akimuita kando na kuzungumza na mkude kwa dakika kadhaa kabla drill ya kupasha misuli haijaanza.
Baadaye nikapewa taarifa kuwa Nadir alikuwa anamsaidia Jey ili hadha ili isije kujulikana kwa Kocha, Nadir akamshauri kuwa ajifanye kama anaomba ruhusa ya kwenda nyumbani ya kuwa kumetokea na dharura.
Jey akasaidiwa na baadhi ya maafisa wengine hadi akapata ruhusu ya kuondoka.
Ni kocha pakee ambaye mpaka sasa hajafahamu kuwa Mkude alikuja kambini amelewa. Baadhi ya viongozi wengine wa benchi hilo hilo hawakupendezewa kabisa kwa Jey kuja amelewa, waliona kama ni kitendo cha dharau na ukosefu wa heshima kwa kazi.
Leo Nikiwa naongea kwa simu na mmoja wa afisa niliyekutana naye jana kambini jana, akanitaarifu kuwa Kocha ameambiwa mchezo wote ulio tokea. Huenda ametonywa na lile kundi dogo ambalo walichukizwa na lile tukio.
Akaongeza zaidi kwa kuniambia kuwa Kocha ameanza kujenga "kutokuwa" na uaminifu na baadhi ya watu katika benchi la Ufundi. Akasema nisisangae kama baada ya game ya Benin kukawa na mabadiliko katika benchi hilo.
Nashauri:- Ni wakati sasa Jonas Mkude asitishe kuichezea Taifa Stars na awape nafasi Vijawa wengine chipukizi.
Si kweliNaona kapata watetezi !!. Unadhani ni kwanini wabongo wanashindwa kucheza Europe ?!. Nidhamu zero .
Ukweli ni nini ?! Sema.Si kweli
Kwa wakati huo sawa ila sio Sasa.Ukweli ni nini ?! Sema.
Waliwahi kupelekwa kina A. China, E. Lunyamila etc wakiwa katika kiwango cha juu lakini walishindwa.
WaTz ni waswahili na ndiyo maana hatuwezi . Kama unashabikia na hili la gongo, atapata wapi uwezo wa kucheza majuu ?!Kwa wakati huo sawa ila sio Sasa.
Wafuasi wa gongo wamo wengi humu . Tz yangu masikini. Kwanini Benin asijipigiekacheze wewe tuone au wewe sio mbongo?
Simba walishampima akili,ila sikumbuki matokeo ya vipimo.Siku moja Asubuhi ataamka Jonas Mkude pale kambini kwao Bunju na atachoma moto kambi nzima ndio watajua mwamba ana matatizo makubwa ya kisaikolojia
Mbona Samatta na Kelvin John wameweza?...wewe ndio huweziWaTz ni waswahili na ndiyo maana hatuwezi . Kama unashabikia na hili la gongo, atapata wapi uwezo wa kucheza majuu ?!
Hawawezi kuweka majibu yake wazi mkuuSimba walishampima akili,ila sikumbuki matokeo ya vipimo.
moja kati ya sifa kuu ya mzushi ni kukosa consistencyKwani wewe unaamini kuwa lwanga ni bora kuliko mkude?
Ndiyo maana viwango vyao vilikuwa vile vilivyokuwa tofauti kabisa kwa Cristian Ronaldo na Messi.Mwisho wao mbaya katika sokawachezaji wakubwa wa uingereza walikuwa walevi mbwa wakiongozwa na steve g na jt