Hili la January Makamba ni hatari zaidi

Pesa za kulipa haya makundi atazitoa wapi?dini sijui biashara mara vijana mmmh!!!Ni nani atakuwa kiongozi wa hilo baraza,mkristu au muislam?Washauri wake hawsmtendei haki au la hataki ushauri wa nje
 
nakusoma vema The Boss

Niseme kuwa katika wagombea wa CCM angalau January katoa 'picha' atakuwa Rais wa namna gani akiweza kufika.....wengine wengi hatujui misimamo yao ya mambo mengi.

Sasa leo katika hotuba yake ya kutangaza nia January kazungumzia 'ufa wa kidini'na kwa mawazo yake akipewa Urais basi ataunda 'baraza maalum la viongozi wa dini'eti kazi yao iwe kukutana kila baada ya miezi miwili na kujadili namna 'ya kutunza amani'na kuondoa huo mgawanyiko wa kidini.

Binafsi naona likifanyika hilo ndio nchi itaingia kwenye mgawanyiko mkubwa zaidi wa kidini umoja wa watanzania, amani upendo na mshikamano haupo sababu ya viongozi wa kidini.

Watanzania wengi wamechanganya dini kwenye familia zao na wanashirikiana vizuri tu kuanzisha Taasisi zitakazo wapa sauti viongozi wa kidini ndio itakuwa 'platform' ya wao ku manipulate 'their influences' na ku gain more voice za kuwagawa wananchi.

Kinachohitajika ni kuwaacha na kuwa na serikali ambayo haiwapi sauti yoyote ile kwenye masuala ya kitaiifa.....'Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi' na viongozi wa dini waondolewe kwenye 'National Affairs' completely.

Tuache kabisa kushirikisha shughuli za kidini na za viongozi wa kitaifa...Sherehe zote za kidini zibaki kuwa za kidini na viongozi wa kitaifa hasa wa serikali.

Wasihusike na wala wasiende kwenda kuhutubbia masuala ya kitaifa ndani ya misikiti na makanisa.

Kama tuko serious na kutenganisha dini na siasa....basi tusiruhusu hizi idea za January kupewa nafasi.

Mawazo ya January kwa juu yanaonekana mazuri sana lakini kiukweli ni mawazo hatari sana sababu yatazidi kuwapa nguvu isiyo ya lazima viongozi wa kidini.

Watu kama Gwajima watajikuta wanapewa 'umuhimu wa kitaifa' usio na lazima kwa kupitia vyombo kama hivyo ambavyo January anataka kushawishi viwepo.

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao.
 
Last edited by a moderator:
nilikuwa naona kama anaomba urais wa serikali ya wanafunzi, sijui kwa nini wazo hili halinitoki!
 
Niseme kuwa katika wagombea wa CCM angalau January katoa 'picha' atakuwa Rais wa namna gani akiweza kufika.....wengine wengi hatujui misimamo yao ya mambo mengi.

Sasa leo katika hotuba yake ya kutangaza nia January kazungumzia 'ufa wa kidini'na kwa mawazo yake akipewa Urais basi ataunda 'baraza maalum la viongozi wa dini'eti kazi yao iwe kukutana kila baada ya miezi miwili na kujadili namna 'ya kutunza amani'na kuondoa huo mgawanyiko wa kidini.

Binafsi naona likifanyika hilo ndio nchi itaingia kwenye mgawanyiko mkubwa zaidi wa kidini umoja wa watanzania, amani upendo na mshikamano haupo sababu ya viongozi wa kidini.

Watanzania wengi wamechanganya dini kwenye familia zao na wanashirikiana vizuri tu kuanzisha Taasisi zitakazo wapa sauti viongozi wa kidini ndio itakuwa 'platform' ya wao ku manipulate 'their influences' na ku gain more voice za kuwagawa wananchi.

Kinachohitajika ni kuwaacha na kuwa na serikali ambayo haiwapi sauti yoyote ile kwenye masuala ya kitaiifa.....'Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi' na viongozi wa dini waondolewe kwenye 'National Affairs' completely.

Tuache kabisa kushirikisha shughuli za kidini na za viongozi wa kitaifa...Sherehe zote za kidini zibaki kuwa za kidini na viongozi wa kitaifa hasa wa serikali.

Wasihusike na wala wasiende kwenda kuhutubbia masuala ya kitaifa ndani ya misikiti na makanisa.

Kama tuko serious na kutenganisha dini na siasa....basi tusiruhusu hizi idea za January kupewa nafasi.

Mawazo ya January kwa juu yanaonekana mazuri sana lakini kiukweli ni mawazo hatari sana sababu yatazidi kuwapa nguvu isiyo ya lazima viongozi wa kidini.

Watu kama Gwajima watajikuta wanapewa 'umuhimu wa kitaifa' usio na lazima kwa kupitia vyombo kama hivyo ambavyo January anataka kushawishi viwepo.

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao.

Naye si kilaza tu!!
maana anshindwa kuwa Tanzania ni scular state. serikali Hian Dini ila watu wake wana dini na uhuru wa dini. kashindwa dogo kupamabanua hilo. wamemdanga akaropke hilo!!
 
Tunalo tatizo tuliowengi tunafikiri Tanganyika ilipoumbwa iikabidhiwa hiyo C C M kiasi kwamba tukiachana nayo basi nchi itayeyuka kubwa hapo ni kuachana na hizi porojo za watia nia wa ccm wamechoka hawana namna mpya ya kufikiri tuwape nafasi wengine mbona nchi zingine zimeachana na mazoea na afadhali kwao zinaonekana kwani ccm ndio niniiii+++
 
Niseme kuwa katika wagombea wa CCM angalau January katoa 'picha' atakuwa Rais wa namna gani akiweza kufika.....wengine wengi hatujui misimamo yao ya mambo mengi.

Sasa leo katika hotuba yake ya kutangaza nia January kazungumzia 'ufa wa kidini'na kwa mawazo yake akipewa Urais basi ataunda 'baraza maalum la viongozi wa dini'eti kazi yao iwe kukutana kila baada ya miezi miwili na kujadili namna 'ya kutunza amani'na kuondoa huo mgawanyiko wa kidini.

Binafsi naona likifanyika hilo ndio nchi itaingia kwenye mgawanyiko mkubwa zaidi wa kidini umoja wa watanzania, amani upendo na mshikamano haupo sababu ya viongozi wa kidini.

Watanzania wengi wamechanganya dini kwenye familia zao na wanashirikiana vizuri tu kuanzisha Taasisi zitakazo wapa sauti viongozi wa kidini ndio itakuwa 'platform' ya wao ku manipulate 'their influences' na ku gain more voice za kuwagawa wananchi.

Kinachohitajika ni kuwaacha na kuwa na serikali ambayo haiwapi sauti yoyote ile kwenye masuala ya kitaiifa.....'Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi' na viongozi wa dini waondolewe kwenye 'National Affairs' completely.

Tuache kabisa kushirikisha shughuli za kidini na za viongozi wa kitaifa...Sherehe zote za kidini zibaki kuwa za kidini na viongozi wa kitaifa hasa wa serikali.

Wasihusike na wala wasiende kwenda kuhutubbia masuala ya kitaifa ndani ya misikiti na makanisa.

Kama tuko serious na kutenganisha dini na siasa....basi tusiruhusu hizi idea za January kupewa nafasi.

Mawazo ya January kwa juu yanaonekana mazuri sana lakini kiukweli ni mawazo hatari sana sababu yatazidi kuwapa nguvu isiyo ya lazima viongozi wa kidini.

Watu kama Gwajima watajikuta wanapewa 'umuhimu wa kitaifa' usio na lazima kwa kupitia vyombo kama hivyo ambavyo January anataka kushawishi viwepo.

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao.

ni ukweli tupu Mkuu! akifanikiwa atajuwa rahisi wa ajabu kabisa! Hivi hajui hatari tarajiwa no ule UFA unaopanuka kati ya walionacho na ziada na wasio nacho hata cha kupepea?? hapo haijalishi seen, kabila, rangi, wala lugha mpaka kieleweke..:msela:
 
The Boss

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao
Unajua mnachekesha sana kuwasoma wakati mwingine. Nirahisi sana kumuona January Makamba amekosea kusema hivyo wakati kila mkutano niliwahi kuhudhuria wa vyama au sherehe za Kitanzania lazima muanze na Asalaam Aleikum - Asifiwe bwana Yesu Kristo, sasa kama mliona kuna makosa ya matumizi ya dini kwa nini hamkuanza na salaam zenu wenyewe mkaweka maneno jingine badala yake?.

Kumbukeni jamani sisi sote tuna dini zetu ambazo ndio mwongozo wa maisha yetu na hakuna kitu kibaya kama serikali ikipoteza mila na desturi za wale inaowaongoza kwa visingizio vya 'Separation of Church and State" kwa sababu wenzetu walifanya hivyo kwa sababu maalum wakipinga sheria moja tu ya Blasphemy ilowanyima Uhuru wa kutoa maoni. Sisi hatuwezi kuepuka Custom law maana ni sehemu ya jamii yetu na hakuna kitu kizuri kama kuwakutanisha viongozi wa Dini inapohitajika.

Hivi tunavyozungumza hufanyika vikao na mara nyingi vimetoa suluhu ya mambo mengi yalokuwa yakichukuliwa kama chuki baina ya imani zetu jambo ambalo lingeweza kabisa kuleta madhara makubwa kama lingepuuzwa. Isipokuwa nakubaliana na wewe sana tu pale serikali inapowaruhusu viongozi wa dini kutoa mwelekezo kwa kisiasa kwa serikali, kinachotakiwa ni wao kupewa maelekezo na serikali wao ni kama Polisi wetu wana serve na ku protect kwa kufundisha mema na kuonya mabaya.. kazi yao sio kutunga sheria bali wanawajibika kufuata sheria.

Dini haiwezi kubakia kama imani ya mtu binafsi ikiwa sisi wenyewe tunatambulishana juu ya Waislaam/Wakristu kama kwamba ni wafuasi wa ama society fulani. And for that needs to be controlled maana Wayahudi wameweza kudai nchi ni yao kwa kutumia dini na ikahalalishwa dunai nzima na sasa tumeona ISIS wakianza kudai nchi... ni mwanzo wa marudio ya kuhalalisha dini kumiliki nchi - Tujihadhari.[/QUOTE]

Mkuu maelezo ya The Boss ni sahihi kabisa.

Mambo ya dini yanatakiwa yasipewe nafasi katika serikali kama alivyoeleza kwa kirefu mtoa uzi huu. Nashangaa kuona wengi tunashindwa kujifunza kwa yanayotokea kwingine. Mifano yako ya Israel na ISIS inatosha kutuonyesha madhara ya kutukuza dini katika siasa.

Tatizo kuu la dini ni watu kusukumwa na imani bila Logic, na hapa ni dini zote (Mifano ni watendayo wakristo kwa waisalam huko Afrika ya Kati, ISIS watendayo kwa wakristo huko mashariki ya kati na Budha watendayo kwa waislam huko Maynmar).
 
January seems to lack appreciation of the time tested concept of "Separation of Church and State" and the need to maintain a secular state.

I suspect though, this proposal of his, is just a ploy to appease and appeal for the support of all faiths and religions, in his quest for the highest office in the country. Based on what I have seen so-far (e.g the cyber crimes Act that he championed) January is not the kinda person who will seek anybody's input on how to maintain peace in the country.If he becomes President, I bet he won't give a rat's ass about what any religious leader has to say, with regard to maintaining peace in the country. He will do as he sees fit, regardless of the consequences.

This January fellow is one to be wary of, as he clearly habors dictatorial tendencies (again this can be inferred from the cybercrimes ACT he championed). He comes across as a Mr know it all. If he becomes President, he will probably suppress a lot of our civl liberties, and if we complain, he will simply tell us he knows what is best for us, so we should just put up or shut up. January appears to be so full of himself!! He strikes me as a very corky fellow, hot headed and immature. Both not qualities befitting a head of state. In my considered judgement, January is not yet presidential material. Maybe in 10 years time, he might by then be mature enough to run a country.

i support at least one of his proposals though:- empowering the PCCB to institute charges before any court in the country, without having to go thru the DPP. This is long overdue!

I fully concur with you. January is not presidential material. Even after 10 years I would still not opt for January as president. At the moment the fellow is still fairly young but he comes across as the all-knowing type. He appears to believe that his stint at state house, writing JK's speeches made him know everything to do with running of government! The other day at one of the debates at Nkurumah's Hall I saw him on tv asking Mzee Butiku rather mockingly, why the first phase government did not build as many secondary schools as done by the fourth phase administration. When he got into parliament, because he knows everything, his first agenda was the Downs power generating plant. His argument was that it was stupid for the country to go without power while there was the Downs plant lying idle! It was as if there was no cost to be incurred by generating power from that plant! He does not seem to know that from independence Tanzanians learnt to be a proud people despite their poverty. For the period that he led the Parliamentary Energy committee he made it look like an executive organ of government. As for the PCCB, methinks the problem is not the procedure involving the DPP. The problem is lack of political will to tackle corruption. Lack of political will makes our politicians use the office of DPP as a filter to check what goes to court and what does not. Once there is political will the office of DPP will cease to be seen as stumbling block. Remember the Richmond scandal? Was the DPP involved in anyway? Was it not the PCCB themselves who cleared the process as clean, presumably owing to pressure from the politicians?
 
Mkuu maelezo ya The Boss ni sahihi kabisa.

Mambo ya dini yanatakiwa yasipewe nafasi katika serikali kama alivyoeleza kwa kirefu mtoa uzi huu. Nashangaa kuona wengi tunashindwa kujifunza kwa yanayotokea kwingine. Mifano yako ya Israel na ISIS inatosha kutuonyesha madhara ya kutukuza dini katika siasa.

Tatizo kuu la dini ni watu kusukumwa na imani bila Logic, na hapa ni dini zote (Mifano ni watendayo wakristo kwa waisalam huko Afrika ya Kati, ISIS watendayo kwa wakristo huko mashariki ya kati na Budha watendayo kwa waislam huko Maynmar).
Mifano ya Israel na ISIS ni mifano ambayo waumini wa dini hizo walipuuzwa na serikali hivyo kuanzisha makundi yanayopingana na serikali. Wewe nambie dunia hii ya leo kuna nchi gani isoweka mawasiliano na viongozi wa dini? Na mahala popote kulipotokea matatizo yoyote ya kidini ni kutokana na serikali kuchukua upande mmoja maana kumbuka serikali inaongozwa na watu wenye nimani zao na huwezi kumtenganisha kiongozi na dini yake hata mseme nini.

Akiingia Lowassa atayaona ya upande ule maana ndio anawasiliana nao, Akiingia January naye atawasilikiza wa upande wake maana ndio huwasiliana nao akienda kusali. Inawezekana pia watu wake wa karibu na washauri wakawa wa dini yake ndivyo binadamu tulivyoumbwa unachagua marafiki kutokana na kukaribu wenu na kuelewana na yote nimatokeo ya mawasiliano.

Unaweza kumundoa Simba Serengeti lakini huwezi kuondoa Unyama wake. Simba atabakia kuwa Simba. Nasi kama binadamu imani za dini zimo ndani ya hisia zetu maana unaposema serikali kumbuka serikali ni WATU wenye imani zao, makabila yao na hata jinsia. Siri kubwa ya kuondosha Ubaguzi iwe Udini, Ukabila na Jinsia nchini ni uwezo wa kuchanganyikana na tukawasiliana kwa lugha moja tunayoifahamu sote kama jamii moja.
 
Niseme kuwa katika wagombea wa CCM angalau January katoa 'picha' atakuwa Rais wa namna gani akiweza kufika.....wengine wengi hatujui misimamo yao ya mambo mengi.

Sasa leo katika hotuba yake ya kutangaza nia January kazungumzia 'ufa wa kidini'na kwa mawazo yake akipewa Urais basi ataunda 'baraza maalum la viongozi wa dini'eti kazi yao iwe kukutana kila baada ya miezi miwili na kujadili namna 'ya kutunza amani'na kuondoa huo mgawanyiko wa kidini.

Binafsi naona likifanyika hilo ndio nchi itaingia kwenye mgawanyiko mkubwa zaidi wa kidini umoja wa watanzania, amani upendo na mshikamano haupo sababu ya viongozi wa kidini.

Watanzania wengi wamechanganya dini kwenye familia zao na wanashirikiana vizuri tu kuanzisha Taasisi zitakazo wapa sauti viongozi wa kidini ndio itakuwa 'platform' ya wao ku manipulate 'their influences' na ku gain more voice za kuwagawa wananchi.

Kinachohitajika ni kuwaacha na kuwa na serikali ambayo haiwapi sauti yoyote ile kwenye masuala ya kitaiifa.....'Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi' na viongozi wa dini waondolewe kwenye 'National Affairs' completely.

Tuache kabisa kushirikisha shughuli za kidini na za viongozi wa kitaifa...Sherehe zote za kidini zibaki kuwa za kidini na viongozi wa kitaifa hasa wa serikali.

Wasihusike na wala wasiende kwenda kuhutubbia masuala ya kitaifa ndani ya misikiti na makanisa.

Kama tuko serious na kutenganisha dini na siasa....basi tusiruhusu hizi idea za January kupewa nafasi.

Mawazo ya January kwa juu yanaonekana mazuri sana lakini kiukweli ni mawazo hatari sana sababu yatazidi kuwapa nguvu isiyo ya lazima viongozi wa kidini.

Watu kama Gwajima watajikuta wanapewa 'umuhimu wa kitaifa' usio na lazima kwa kupitia vyombo kama hivyo ambavyo January anataka kushawishi viwepo.

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao.

Mkuu,
Kwanza nikupongeze kwa kusikiliza ile speech ya jana. Na bila kumung'unya maneno ndio speech bora kabisa kuliko zote za watangaza nia. Natumaini utakubaliana na hilo. Sasa kwenye hiyo hoja yako. Hebu soma alivyosema jana. Nanukuu

"Kipaumbele cha tano ni amani, umoja na usalama wa mali na maisha ya Watanzania. Amani na umoja wa nchi yetu ni tunu na urithi tulioachiwa na waasisi wa nchi yetu. Marais wote waliopita wamefanya kazi kubwa ya kuzilinda tunu hizi. Serikali yangu haitakubali urithi huu upotee. Tutafanya jitihada zote ili kujenga maridhiano mapya na upendo miongoni mwa makundi mbalimbali katika jamii yetu. Nitawahusisha viongozi wa dini zote katika hili. Nitaanzisha Jukwaa la Rais na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Jumuiya ya Wakristo Tanzania (CCT) na Baraza la Waislam Tanzania (BAKWATA) litakalokutana kila miezi miwili kujadili na kupanga mikakati ya kuendeleza amani, umoja, upendo na maadili ya jamii. "


Sidhani kama maana yake ni kama ulivyoweka wewe hapo wewe. Kumbuka vizuri sana jinsi Mwalimu Nyerere alivyotumia Bakwata na TEC kuijenga amani yetu NA kuinua maadili ya kiujamaa kipindi kile. Vile vile, kanisa na msikiti kuna intellectual heavyweights ambao sio mbaya Ndugu Rais akiwapa jukwaa kusikiliza shida zao.

Speech yote bado inapatikana hapa

January Makamba - Presidential Campaign Launch on Livestream
 
Wakuu..naomba mwenye namba ya simu ya january makamba anisaidie..tafadhali..asante sana
 
Mkandara, kwa maoni yangu tatizo la udini hapa kwetu siyo kubwa kwa kiasi amabacho baadhi ya watu wanataka lionekane. Tulishajenga msingi mzuri wa kutenganisha dini na serikali na tukapiga hatua kubwa. Tumerudishwa nyuma na wanasiasa wababaishaji ambao wameingiza dini kwenye siasa kwa maslahi yao binafsi. Ufumbuzi mzuri wa tatizo lililosababishwa na wanasiasa ni kurudi kwenye misingi tuliyoanza nayo; siyo majaribio myepesi kama haya ya January. Kusalimia Aleikhum salaam au Bwana Yesu asifiwe kwenye majumuiko ya kijamii siyo udini hata kidogo na hakuna tatizo. Sijui kama January amefanya uchambuzi wowote kuhusu tatizo la udini na kubaini kwamba linasababishwa na masheikh na maaskofu? Mbali na wanasiasa muflisi, tatizo la udini pia linatoka nje; itikadi kali za kidini.
 
Lakini mbona huwa tunaambiwa jamaa ni kichwa sana.

Sasa kama ni kichwa kwa nini mtihani wa fom foo akwapue:becky:?
hamna lolote ! sifa za uzushi tu , kichwa gani kimeshindwa hata kugundua mashine ya kubangua madafu , siasa za ccm ni ujanjaujanja tu .
 
Hii ni mada bora kwa uhai na ustawi wa Taifa la Tanzania na watu wake.

Kuwaweka viongozi wadin kwenye attention nikulipeleka Taifa kuzimu. Madai kadhaa yatazua migogoro hatimae machafuko na mwisho vita kamili.

1. Madai ya migawanyo ya madaraka kwa kuzingatia uwiano wa kidin badala ya taaluma za wahusika yatazuka huko.

2. Madai ya haki za kuchinja yataibukia hukohuko

3. Madai ya usawa wakumiliki resources kwa mitazamo ya din yataibuliwa mf. Mahospital, mashule, miradi nk

4. Madai ya migawanyo ya ruzuku bila kufuata utaratibu wala vigezo yataibuliwa ilmradi kila din ipate.

5. Madai ya kutofuga au kufuga baadhi ya wanyama yataibuliwa hatakama katiba inaruhusu.

6. Madai ya zamu yetu kupata urais siyo din yenu yatazuka nk

Kunamigogoro mingi itaibuka nakulitetemesha Taifa na kufarakanisha mtu na mtu, jiran na jiran, mkowa na mkowa nk.

Hili jambo nilakuliogopa kama ukimwi maana unapoingilia nipatamu sana kwa maambukizi mengi ukiachiambali ajali nk lakin UKIMWI UKIINGIA BALAA, KUTOKA NI MATANGA yaan vilio nakusaga meno.

Tusishabikie na kushangilia kifo tujiweke mbali na madhila balaa na hila za ibilisi. Viongozi wadin waache mbali kabisa na serikali isijingize kubeba gunia lililojaa na lijivuja tindikali aina ya cynide (udin) itatuangamizia Taifa letu.

Hongera The Boss hii ni mada bora na muhim sana kwetu na uhai Taifa kwa ujumla.
 
Sijui kama alijiuliza kwamba Bakwata haiwakilishi waislamu wote na wengine hawaikubali kama mwakilishi wao halali. Na pia hata hizo taasisi za kikristo haziwawakilishi wakristo wote, kuna madhehebu ya kikristo hayatangamani na taasisi hizo. Nakubaliana na maoni ya Boss, mtazamo wa Makamba ni too simplistic na itaongeza nyufa.
 
Umeshaambiwa hata mtihani wa fomu foo alikwapua pepa.
Rais gani hajui hata katiba yake inasemaje kuhusu dini.
Laiti Nyerere (R.I.P Mwalimu) angekuwepo akaona uozo unaoendelea.

Ha ha ha,January awe Rais?...sipati picha ya mambo yatakavyokuwa.Hajaomnesha ukomavu ktk maeneo aliyopewa.
 
Kwa kweli inanishangaza kuona viongozi wa serikali wakiapishwa na vitabu vitakatifu vya dini bilakuwa na kipimo cha imani ya mhusika kuhusu vitabu hivyo. Hii ni kulazimisha ndoa ya dini na siasa bila maridhiano. Ingefaa kuapa kwa kutumia katiba. Jambo jingine dini niuhusiano wa mtu na Mungu. Kwa nini dini iruhusiwe kuwa chanzo cha chuki na mifarakano hadi kufikiriwa kuundiwa chombo cha kushughulikia mahusiano ya Mungu na watu?
 
Kwa kweli inanishangaza kuona viongozi wa serikali wakiapishwa na vitabu vitakatifu vya dini bilakuwa na kipimo cha imani ya mhusika kuhusu vitabu hivyo. Hii ni kulazimisha ndoa ya dini na siasa bila maridhiano. Ingefaa kuapa kwa kutumia katiba. Jambo jingine dini niuhusiano wa mtu na Mungu. Kwa nini dini iruhusiwe kuwa chanzo cha chuki na mifarakano hadi kufikiriwa kuundiwa chombo cha kushughulikia mahusiano ya Mungu na watu?
Mkuu kuna mengine tunayachukua kama yalivyo maana ukiingia kwa undani zaidi ya imani za dini utagundua kwamba Yesu hakuwa Mkatoliki wala Mrutheri na hata Muhammad hakuwa Sunni wala Shia bali mcha Mungu, haya madhehebu ya dini tumeanzisha wenyewe na hatari yake ni kubwa toka kuanzishwa kwake hivyo bora kuwepo mawasiliano mazuri baina ya vyombo hivi na serikali kama mshauri. Tunachopinga ni serikali kushirikiana na imani hizi ila huwezi kataza mtu na imani yake utakuwa unaondoa uhuru na haki yake.

Uingereza wameweza tu kukomesha Ugaidi wa IRA kwa kuanzisha mawasiliano bora baina ya vyombo vya dini na serikali. leo wameshindwa kuleta salama huko Mahsariki ya kati kwa sababu serikali zinajaribu kuwasiliana zenyewe dhidi ya dini pasipo kufahamu kwamba chimbuko la misukosuko yote hiyo yote ni mawasiliano mabaya yaliyopo baina ya madhehebu na nasaba zao.

Mahala popote pakisha anza ubaguzi wa aina yoyote iwe dini, Ukabila ama rangi basi ni vizuri sana serikali kuwa karibu na vyombo hivyo, kuwasilikiza na hata kuwashauri juu ya sheria na misngi ilojenga Utaifa wao sio dini zao.
 
62 Reactions
Reply
Back
Top Bottom