Lord Diplock MR
JF-Expert Member
- Mar 16, 2015
- 1,393
- 3,234
Je idris Sultan ni jambazi la kutumia silaha? Je ni gaidi? Ni alshababu au alkaida? Na je jambazi hana ndugu na jamaa? Hana ndugu wanaompenda na yeye anawapenda? Je gaidi wa alkaida hana ndugu na jamaa? Alishababu hawana watoto? Mbona amekuwa mpweke hivi? Mbona wasanii wenzake wamemwacha? Mbona hawakujitokeza hata kumpa pole siyo lazima wapost basi si wangehudhuria tu hata mahakamani?
Hivi wasanii wa Tanzania mtamjali nani akipata tatizo? Mtaamka na kupaza sauti nani akiwa matatani kama msanii mwenzenu anapata shida nyie mnajifungia ndani mnawaachia wanaharakati wa Twitter wamtetee?
Kiukweli kwa hili limewavua nguo sana wasanii wa Tanzania na mnaonesha ni jinsi gani msivyopendana huu ni udhaifu mkubwa sana kwa kweli.
Hivi wasanii wa Tanzania mtamjali nani akipata tatizo? Mtaamka na kupaza sauti nani akiwa matatani kama msanii mwenzenu anapata shida nyie mnajifungia ndani mnawaachia wanaharakati wa Twitter wamtetee?
Kiukweli kwa hili limewavua nguo sana wasanii wa Tanzania na mnaonesha ni jinsi gani msivyopendana huu ni udhaifu mkubwa sana kwa kweli.