Hili la Fiesta linaonesha kuna tatizo kubwa viongozi Dar na linahitaji hatua za haraka

gango2

JF-Expert Member
Aug 31, 2011
1,941
2,251
Habarini za mchana! (mods naomba thread hii isiunganishwe tafadhari)

Kwanza kabisa napenda kudeclear kuwa mimi ni mpenzi wa burudani na sio Fiesta au wasafi festival, hizi zote mimi nilikuwa naona ni chachu ya maendeleo ya sanaa na burudani Tanzania!

sasa nikija kwenye maada, nimeshangazwa sana na taarifa zilizotolewa hivi karibuni kuhusu hii FIESTA kuahirishwa! Kwa mtu yeyote anayefikiria au anayeangalia investments iliyofanywa hapo ni dhahiri atakuwa amesikitishwa sana na hichi kilichotokea. Hasa ukizingatia muda wa zuio ulipotolewa Nimesema hivi kwa sababu

  1. kwanza kuna investments kubwa imefanywa katika maandalizi, matangazo, gharama zote hizi zinapotea bila sababu ya msingi, na kusababisha hasara kubwa kwa waandaaji
  2. Pili ni usumbufu uliojitokeza kwa wepenzi wa burudani, naamini kuna watu wengi wamejiandaa na wengine labda walisafiri kutoka maeneo ya mbali na hata wengine kuhairisha vitu vingine ili waudhurie tamasha hili
  3. Tatu, ni kwa namna gani wasanii na watumbuizaji walivyojiandaa na wengine walitumia gharama zao na wengine walikataa show sehemu za mbali kwaajili yahili. Najaribu kufikiria tu endapo kungekuwa na mualikwa toka nje ya nchi sijui ingekuwaje
Sasa kwanini naona kuna tatizo kubwa sana ambalo kiukweli litatugharimu siku zijazo kama halitochukuliwa hatua mapema.

  1. kwanza suala Leaders clubs kutumika kwa fiesta au matamasha mengine mengi sidhani kama limeanza mwaka huu, ni zaidi ya miaka 12 sasa linafanyika hapo, bila kipingamizi sasa leo kusema ni kelele ni logic ambayo haileti maana kabisa
  2. Pili kwanini zuio litolewe siku moja kabla wakati maandalizi yameshafanyika, hivi kulikuwa na haja ya kusubiri siku moja kabla ndo zuio litolewe, na je kama kuna malalamiko yametoka wapi na hospitali gani kulalamikia hili
  3. Tatu, hivi unaposema uende Tanganyika Parkers inamaana huko tanganyika Parkers hakuna binadamu wanaoishi huko? tena naamini kawe ndo kuna watu wengi kuliko maeneo ya hapo Leaders! au kwa kuwa watu wengi wanaoishi kawe ni wa vipato vya chini kwa hiyo wao kelele ni kutu cha kawaida
  4. nne mwaka jana tu Rais alibariki hili tamasha lifanyike pale pale na tena mpaka asubuhi, sasa tunashangaa hayo matamko leo kuwa pale ni usumbufu yanatoka wapi? Pia hapo hapo tunaona kiongozi mkubwa wa mkoa anashiriki uhamasishaji lakini leo barua inatoka kwa mtu mdogo kabisa
Hebu viongozi wetu tuwe tunajaribu kufikiri kwanza na kushirikisha hata vyombo vingine kuhusu maamuzi tunayotoa, maana naamini watu kama BASATA, WIZARA hata uongozi wa mkoa sidhani kama wote maamuzi yao yanaweza kuwa sawa!

mwisho! kama tunataka ushindani wenye tija, basi tufanye kwa misingi iliyobora na sio kwa kuwakandamiza wengine, tutakuwa tunafanya kazi ya kukinga maji kwenye kikapu cha makuti!

nawasilisha hoja! naomba tujadili kwa hoja
GanGo
 
Clouds hata siwaonei huruma kabisa! Wameshazingua sana harakati,wameshazingua sana wasanii wengi,siwaonei huruma hata chembe! Acha yawakute!

Karma is a beyach!!

but sis tumeangalia from other side! gharama, na hasara iliyotokea
 
Habarini za mchana! (mods naomba thread hii isiunganishwe tafadhari)

Kwanza kabisa napenda kudeclear kuwa mimi ni mpenzi wa burudani na sio Fiesta au wasafi festival, hizi zote mimi nilikuwa naona ni chachu ya maendeleo ya sanaa na burudani Tanzania!

sasa nikija kwenye maada, nimeshangazwa sana na taarifa zilizotolewa hivi karibuni kuhusu hii FIESTA kuahirishwa! Kwa mtu yeyote anayefikiria au anayeangalia investments iliyofanywa hapo ni dhahiri atakuwa amesikitishwa sana na hichi kilichotokea. Hasa ukizingatia muda wa zuio ulipotolewa Nimesema hivi kwa sababu

  1. kwanza kuna investments kubwa imefanywa katika maandalizi, matangazo, gharama zote hizi zinapotea bila sababu ya msingi, na kusababisha hasara kubwa kwa waandaaji
  2. Pili ni usumbufu uliojitokeza kwa wepenzi wa burudani, naamini kuna watu wengi wamejiandaa na wengine labda walisafiri kutoka maeneo ya mbali na hata wengine kuhairisha vitu vingine ili waudhurie tamasha hili
  3. Tatu, ni kwa namna gani wasanii na watumbuizaji walivyojiandaa na wengine walitumia gharama zao na wengine walikataa show sehemu za mbali kwaajili yahili. Najaribu kufikiria tu endapo kungekuwa na mualikwa toka nje ya nchi sijui ingekuwaje
Sasa kwanini naona kuna tatizo kubwa sana ambalo kiukweli litatugharimu siku zijazo kama halitochukuliwa hatua mapema.

  1. kwanza suala Leaders clubs kutumika kwa fiesta au matamasha mengine mengi sidhani kama limeanza mwaka huu, ni zaidi ya miaka 12 sasa linafanyika hapo, bila kipingamizi sasa leo kusema ni kelele ni logic ambayo haileti maana kabisa
  2. Pili kwanini zuio litolewe siku moja kabla wakati maandalizi yameshafanyika, hivi kulikuwa na haja ya kusubiri siku moja kabla ndo zuio litolewe, na je kama kuna malalamiko yametoka wapi na hospitali gani kulalamikia hili
  3. Tatu, hivi unaposema uende Tanganyika Parkers inamaana huko tanganyika Parkers hakuna binadamu wanaoishi huko? tena naamini kawe ndo kuna watu wengi kuliko maeneo ya hapo Leaders! au kwa kuwa watu wengi wanaoishi kawe ni wa vipato vya chini kwa hiyo wao kelele ni kutu cha kawaida
  4. nne mwaka jana tu Rais alibariki hili tamasha lifanyike pale pale na tena mpaka asubuhi, sasa tunashangaa hayo matamko leo kuwa pale ni usumbufu yanatoka wapi? Pia hapo hapo tunaona kiongozi mkubwa wa mkoa anashiriki uhamasishaji lakini leo barua inatoka kwa mtu mdogo kabisa
Hebu viongozi wetu tuwe tunajaribu kufikiri kwanza na kushirikisha hata vyombo vingine kuhusu maamuzi tunayotoa, maana naamini watu kama BASATA, WIZARA hata uongozi wa mkoa sidhani kama wote maamuzi yao yanaweza kuwa sawa!

mwisho! kama tunataka ushindani wenye tija, basi tufanye kwa misingi iliyobora na sio kwa kuwakandamiza wengine, tutakuwa tunafanya kazi ya kukinga maji kwenye kikapu cha makuti!

nawasilisha hoja! naomba tujadili kwa hoja
GanGo



Nchi inaongozwa na WASHAMBA - Zitto.
 
Clouds hata siwaonei huruma kabisa! Wameshazingua sana harakati,wameshazingua sana wasanii wengi,siwaonei huruma hata chembe! Acha yawakute!

Karma is a beyach!!
Nyie ndo mnasema hivyooo...Huyo diamond kapitia mikono ya Clouds mpaka kufika palee..! Kama huwa hawawalipi mbona hadi jana kulikuwa na wasanii wengi tu wamesajiliwa kuperform??? msifate mkumboo...
 
Nyie ndo mnasema hivyooo...Huyo diamond kapitia mikono ya Clouds mpaka kufika palee..! Kama huwa hawawalipi mbona hadi jana kulikuwa na wasanii wengi tu wamesajiliwa kuperform??? msifate mkumboo...
U just don't know the reality! You are just a boy,rikiboy!
 
U just don't know the reality! You are just a boy,rikiboy!
Acheni kufata mkumbo malipo ya show huwezi kulipwa unavyotaka wewe maana kila mtu akilipwa hivyoo sidhani kama clouds wangeweza kuendesha fiesta hadi leoo...! Diamon alifanikiwa zaidi na akaona hastahili kulipwa kile kidogo angeondoka bilaa kejeli na dharau maana wakati alipokuwa analipwa hizo laki 2 kwa show ndo uwezo wa clouds ulipofikiaa so now anaweza lipwa mil 100 anadharau waliomtoa alipokuwa hana uwezo hata wa Kupiga Show au kuitwa afanye show za malipoo hakuna aliekuwa anamjuaaa....Ni Ujinga na Una Mwisho mbaya...!
 
Acheni kufata mkumbo malipo ya show huwezi kulipwa unavyotaka wewe maana kila mtu akilipwa hivyoo sidhani kama clouds wangeweza kuendesha fiesta hadi leoo...! Diamon alifanikiwa zaidi na akaona hastahili kulipwa kile kidogo angeondoka bilaa kejeli na dharau maana wakati alipokuwa analipwa hizo laki 2 kwa show ndo uwezo wa clouds ulipofikiaa so now anaweza lipwa mil 100 anadharau waliomtoa alipokuwa hana uwezo hata wa Kupiga Show au kuitwa afanye show za malipoo hakuna aliekuwa anamjuaaa....Ni Ujinga na Una Mwisho mbaya...!
Riki,
Sijamuongelea diamond wala sijatoa mfano wowote! Mimi nime refer mbali sanaaa,enzi na enzi! CMG imeshazingua sana wasanii wengi sana,imeshanyonya wasanii wengi sana,imeshazima ndoto za watu wengi sana! Kwahiyo kwa haya wanayopitia siwaonei huruma!

It's all about Karma
 
Mchezo wa hao viongozi ni mbaya sana sana sanaaaa. Haiwezekani wanaifanya hii awamu iwe awamu ya uonevu. Ningefurahi kuona sasa Raisi anaingilia tena au kuwahamisha viongozi wote wa mkoani wanaoharibu biashara za watu makusudi mwishoni na kuikosesha kodi Serikali. Hawajui kuna watu wanafanya mauzo hapo masikini sisi wa nchini kujipatia kipato hata kuuza maji n.k.

Tarehe 22 wanatoa kibali, Jana tarehe 23 wanakifuta. Inaonyesha hakuna mipango ya vibali jijini Dar. Leo ndio ilikuwa Fiesta, kuna matatizo ya kiutendaji na wanafanya kazi kama hawana mipango.

IMG-20181124-WA0040.jpg


Inabidi Raisi sasa afanye jambo la kukomboa wafanya biashara kutoka kwenye mikono ya watu wenye roho mbaya, wanaotumia vyro vyao kwa faida binafsi za kuumiza kazi za watu makusudi.
 
Riki,
Sijamuongelea diamond wala sijatoa mfano wowote! Mimi nime refer mbali sanaaa,enzi na enzi! CMG imeshazingua sana wasanii wengi sana,imeshanyonya wasanii wengi sana,imeshazima ndoto za watu wengi sana! Kwahiyo kwa haya wanayopitia siwaonei huruma!

It's all about Karma
Kweli sikatai maana Kina Jdee mfano ruby naee..shida ukikosana nao wao wanakufanyia mbaya na Unapotea kwenyr Game kwelii..! So hili pia lilikuwa tatzo lakini sio kusema Hawalipi watu kwenye Show ni Uongoo... Ofcoz uwepo wa Tv na Radio kama wasafi kutapunguza ule Umwamba wa Clouds lakini still isiwe sababu kujenga chuki maana Mwisho wake unaweza kuwa mbaya zaidii....
 
Mimi ni mtu wakawaida sana ila nilivyosikia fiesta inakuja mkoani kwangu nilichukua mpka cent ya mwisho nikaenda kununua kuku viazi mkaa mafuta na mambo mengi mengine ya garama nikafatilia na kibali kilikuwa kinatolewa na tbl nikapata nikatoa na ajira kwa vijana kumi wanawake na wanaume tukapiga kazi, hawa niliowaajiri ilibidi niwalipe kiasi flan kwanza waache nyumbani au kujiandaa, apa nawaza lazma apo dar kuna mtu aliwaza kama mimi dah izo garama sijui asee nampa pole sana, kweli ubinadamu kazi na mtu mwenye roho mbaya kweli hanaga mawazo wala huruma asee
 
Back
Top Bottom