Hili la Cleopa ni kama TUSI kwa Jakaya

quimby_joey

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
390
164
Jana ITV nimesikiliza mdahalo uliokuwa ukiilenga Tanzania katika miaka 50 ijayo mmoja wa wageni waaliikwa alikuwa waziri mkuu wa zamani ndg Cleopa Msuya. Katika moja ya hoja zake ilionekana ni kama anauponda waziwazi utawala wa JK, hii ni baadhi ya michango yake;

i. Tz ya miaka 50 ijayo inahitaji Strong leader atakayeweza kusimama na kusema hiki kifanyike na hiki kisifanyike na ambaye ataweza kusimama katika maamuzi magumu (rejea JK kushindwa kuwa na msimamo juu ya matatizo yanayowakabili wa-tz likiwamo umeme)

ii. Tz inakabiliwa na ugonjwa hatari wa malaria, suluhisho sio kwenda kuomba msaada wa vyandarua suluhisho ni kukabili vyanzo vinavyozalisha mbu na vimelea vyake (msaada kutoka serikali ya marekani)

iii. Siku hizi hatuna wataalam wa kutosha katika masuala mbalimbali nchini mfano wa kina Prof. Benno Ndulu na wengine wa miaka ile, leo hii badala ya serikali kupeleka vijana kwa wingi nje ya nchi na kupata wataalam kama vile china na hata kenya, viongozi wamebaki kubuni mbinu mbalimbali zitakazowapeleka nje ili wapate posho kutunisha mifuko yao na kununua magari, nchi haina wataalam wa kutosha kuweza kuleta mabadiliko tunapoingia miaka 50 ijayo.(safari za JK nje ya nchi)

kwa maoni yangu nadhani mzee msuya kaamua kuponda wazi wazi utawala wa JK
 
Yes , kwani C ni wa kwanza kumtukana JK? JK kajitukanisha mwenyewe.
 
Jana ITV nimesikiliza mdahalo uliokuwa ukiilenga Tanzania katika miaka 50 ijayo mmoja wa wageni waaliikwa alikuwa waziri mkuu wa zamani ndg Cleopa Msuya. Katika moja ya hoja zake ilionekana ni kama anauponda waziwazi utawala wa JK, hii ni baadhi ya michango yake;

i. Tz ya miaka 50 ijayo inahitaji Strong leader atakayeweza kusimama na kusema hiki kifanyike na hiki kisifanyike na ambaye ataweza kusimama katika maamuzi magumu (rejea JK kushindwa kuwa na msimamo juu ya matatizo yanayowakabili wa-tz likiwamo umeme)

ii. Tz inakabiliwa na ugonjwa hatari wa malaria, suluhisho sio kwenda kuomba msaada wa vyandarua suluhisho ni kukabili vyanzo vinavyozalisha mbu na vimelea vyake (msaada kutoka serikali ya marekani)

iii. Siku hizi hatuna wataalam wa kutosha katika masuala mbalimbali nchini mfano wa kina Prof. Benno Ndulu na wengine wa miaka ile, leo hii badala ya serikali kupeleka vijana kwa wingi nje ya nchi na kupata wataalam kama vile china na hata kenya, viongozi wamebaki kubuni mbinu mbalimbali zitakazowapeleka nje ili wapate posho kutunisha mifuko yao na kununua magari, nchi haina wataalam wa kutosha kuweza kuleta mabadiliko tunapoingia miaka 50 ijayo.(safari za JK nje ya nchi)

kwa maoni yangu nadhani mzee msuya kaamua kuponda wazi wazi utawala wa JK

Kuna tofauti kati ya kuponda na kumweleza mtu ukweli. Sijaona sehemu aliyoponda katika maelezo yako. Ninaona akiusianisha kinacho fanyika na kile alichotegemea kiwe kinafanyika kwa ajili ya miaka 50 ijayo iliyo myema kwa watanzania.
 
Quimby naomba tuzoee utaratibu wa kumwambia ukweli mtu hata kama ni kiongozi ili tusaidiane kujenga nchi yetu, Niliangalia kipindi kile na nilifurahi kuona sasa watu kama Msuya wana msaidia rais aone mapungufu yake.

Nchi masikini yenye matatizo yasiyohitaji hata secondary education kuyaelewa lakini rais wetu anaona sawasawa tu hii ndo imepelekea hapa tulipo na si kosa wala tusi sasa tumwambie ameshindwa achie ngazi hata September 2011. Hafanyi chochote kazi ya kuzurula tu na kucheka na kama hatuelewi akaulize wenzie wakina Gadafi
 
Acha kiingereza cha kuangalia kwanza kwenye kamusi ndipo uandike sentensi. Kama MSY hakufanya lolote wakati wa enzi zake kama WF, anakiri makosa. Kosa si kosa, kosa kurudia kosa. Binafsi nimefurahishwa sana na kauli yake jana.

MSY hahitaji upendeleo wowote kutoka kwa JK... hivyo wale ambao hawana ajenda za maslahi binafsi wakimwambia JK labda ataona mwanga!!! Hii itamsaidia JK (haambiliki) kufika Septemba 2011, maana naona kama ya Libya yanamnyemelea vile!!!
 
huyu masaburi aliwahi kuwa pm na waziri wa pesa yeye alifanya nini cha mno?

Suala lililopo ni ushauri muhimu ambao kwa watu wanaoangalia mbali miaka 100 ijayo na kwa maslahi ya Taifa lazima ujenge Taifa la wasomi werevu,hali ilivyo sasa na watu wasiopenda kuambiwa ukweli ndo watakaopinga lakini Mfumo wetu wa Elimu uko ICU na hata wanaoiva kwa huo mfumo wako mahututi kiuelevu na soko la Afrika Mashariki linakuja,lazima tuwe mamesenja tuu..
 
he told him what he had to tell him and that to me is the naked truth let Jk swallow it. He has failed us with his bootlickers are heading for a political doom/quagmire
 
Nadhani hajatukana Ila kasema ukweli, Kwa mfano hili la kutokomeza malaria, Alichosema CDM ni sawa kwani mbu wapokila mahali sio mpaka tukiwa tumelala
 
what Msuya said is the TRUTH. Kama tunahitaji kusogea mbele miaka 50 ijayo, hatuna budi kuwa na uongozi imara.

It is the TRUTH, no longolongo
 
@iza..point taken i cant argue simply bcoz nimeishia charge.
AM OUT OF HERE...
 
Jana ITV nimesikiliza mdahalo uliokuwa ukiilenga Tanzania katika miaka 50 ijayo mmoja wa wageni waaliikwa alikuwa waziri mkuu wa zamani ndg Cleopa Msuya. Katika moja ya hoja zake ilionekana ni kama anauponda waziwazi utawala wa JK, hii ni baadhi ya michango yake;

i. Tz ya miaka 50 ijayo inahitaji Strong leader atakayeweza kusimama na kusema hiki kifanyike na hiki kisifanyike na ambaye ataweza kusimama katika maamuzi magumu (rejea JK kushindwa kuwa na msimamo juu ya matatizo yanayowakabili wa-tz likiwamo umeme)

ii. Tz inakabiliwa na ugonjwa hatari wa malaria, suluhisho sio kwenda kuomba msaada wa vyandarua suluhisho ni kukabili vyanzo vinavyozalisha mbu na vimelea vyake (msaada kutoka serikali ya marekani)

iii. Siku hizi hatuna wataalam wa kutosha katika masuala mbalimbali nchini mfano wa kina Prof. Benno Ndulu na wengine wa miaka ile, leo hii badala ya serikali kupeleka vijana kwa wingi nje ya nchi na kupata wataalam kama vile china na hata kenya, viongozi wamebaki kubuni mbinu mbalimbali zitakazowapeleka nje ili wapate posho kutunisha mifuko yao na kununua magari, nchi haina wataalam wa kutosha kuweza kuleta mabadiliko tunapoingia miaka 50 ijayo.(safari za JK nje ya nchi)

kwa maoni yangu nadhani mzee msuya kaamua kuponda wazi wazi utawala wa JK

Haya ni maoni yake, kwa jinsi anavyoona au kulinganaisha na wakati alipokuwa kwenye uongozi. Hata hivyo wote tunakumbuka huyu ni miongoni mwa wanafunzi wa Hayati Mwalimu waliochangia kushindwa kwa sers sahihi za Ujamaa na Kujitegemea.
 
Unachanganya mambo! kwa kadri ulivyomnukuu Msuya kwenye maelezo yako hakumtusi JK bali ameelezea ukweli wa hali ilivyo na jinsi ambavyo ingetakiwa iwe. Wewe ni shahidi kwamba miaka ya sabini na themanini (kama ulikuwepo au kusikia) ugonjwa wa malaria ulikuwa unakabiliwa kwa kuteketeza mazalia ya mbu, ambapo wahudumu wa afya walikuwa wakipita mitaani ku spray mazalia ya mbu.

Sasa wanagawa vyandarua sijui kimoja au 2 kwa kaya : jiulize wastani wa watu kwa kaya ni wangapi hapa nchini ( 4-6people); pili kuna mikoa nimeona hizo neti wanavulia samaki!!; tatu wanadai neti zimewekwa dawa ya kuzuia mbu kwa miaka 5!!

Nimeshuhudia hiyo neti unifunga asubuhi jioni mbu wamejaa!!. Zamani vijana wengi walikuwa wanapelekwa scholarships nje na serikali lakini sasa wale wachache walioko huko wametelekezwa kwa malipo madogo tu ya ada; badala yake viongozi wakiongozwa na JK ndiyo wamekuwa kiguu na njia.

(Si umesikia wale board members wa Ngorongoro waliotaka kwenda Hongkong - watu 10!!- eti kutangaza utalii???) Kwa hiyo haya siyo matusi ni ukweli na kama JK angekuwa na washauri wazuri angewatumia sana hawa wazee.
 
mzee na amua kuropoka bado ana kisasi kushindwa katika mbio za uraisi JK ni kikwazo kwake!!ila nae hana fadhila akiitukana serikali si kamtukana na mwanae ambae ni waziri -Mathayo Dadi
 
Enzi za Ben Mkapa, alizindua kauli mbiu ya uwazi na ukweli. kumwambia mtu ukweli si matusi, bali ni kumsaidia ajitambue na kufanya mabadiliko.
 
Back
Top Bottom