Hili la abiria kulipa nauli moja bila kujali umbali SUMATRA mnalichukuliaje?

maiyanga1

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
1,317
1,790
Mimi ni mdau wa usafiri wa umma na kwa kiasi fulani nimetembea katika maeneo tofautitofauti. SUMATRA ikiwa ni mamlaka inayosimamia usafiri wa nchi kavu na majini, wanafahamu kwamba maeneo mengi ya vijijini wafanyabiashara ya usafiri huwatoza abiria nauli moja hata kama msafiri hafiki kituo cha mwisho? Na kama wanafahamu wanachukua hatua gani? Nna mifano kadhaa:

1. Abiria anayepanda gari Shinyanga mjini kwenda Munze (wilaya ya Kishapu) analipa sh. 3000 hii haijalishi anashuka katikati au kituo cha mwisho.

2. Abiria anayepanda gari Muheza kwenda Bombani analipa sh. 1000 hata kama anashuka kituo chochote kabla ya Bombani.

3. Abiria anayepanda gari Arusha kwenda Tanga hulipa nauli ya Tanga hata kama anashuka Segera, Hale, Muheza au Pongwe.

Wadau mnaweza kuongezea mifano mingine.

Ninajua kwamba nauli hupangwa kwa kila kilometa, ikitofautisha barabara ya lami na barabara ya vumbi.

Serikali yetu inaongelea wanyonge kwenu SUMATRA mnatuchukuliaje tunaotumia usafiri wa umma?
 
Mwendo kasi mbezi hadi kimara ,hata anayeshuka kibanda cha mkaa analipa hiyo hiyo.
Dara Moro ,anayeshuka chalinze analipa hiyhiyo ya moro
 
Hii ni kweli.....root ya kutoka Mwanza hadi Manyara unalipa elf 35000 sawa na nauli ya mtu anayetoka mwanza hadi moshi ..nilishangaa sana.
 
Viongozi Wapo
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Anakasirishwa Na Mambo Kama Hayo Wakati Mamlaka Zipo, Viongozi Wapo
 
Hilo ni jipu la kufukuzisha watu kazi. Ni dhuluma na ni wizi wa wazi, uliofumbiwa macho muda mrefu kwa ajili ya maslahi ya kujaza matumbo ya watu, wakiwemo viongozi.

Viongozi wanaopewa mamlaka, badala ya kutatua kero, wao aidha huziongezea ama kuacha ziendelee kuumiza wananchi kwa kuwa wanakuwa ni wanufaika wa kero hizo.

Sasa hapo kwa kwa mfano waziri akiulizwa kizushi kama walivyoulizwa wenzao siku ya mkutano wa wafanya biashara, anaweza akajibu nini?

Au akitimuliwa kidhalilishaji atalaumu mtu?

Tunaposema kuwa kuna ombwe kubwa sana la uwajibikaji wa viongozi kwenye serikali hii tunakuwa tupo sahihi.
 
Nauli ya Dar Arusha ni sawa na Nauli ya Dar Moshi lakini kibokobtao inakuja e-Ticketing itaanza hivi karibuni wapiga debe wote kazi hakuna
 
Nilipanda kutoka Tanga - Mwanza kwa Alis Star nikalipa 51,000. Mwezangu akapanda Mombo akalipa 51,000 kama mimi. Linafaa kuongelewa hili.
 
Hii ni kweli.....root ya kutoka Mwanza hadi Manyara unalipa elf 35000 sawa na nauli ya mtu anayetoka mwanza hadi moshi ..nilishangaa sana.
1. Basi likiandikwa Arusha - Dar (express) kinadharia halistahili kusimama simama vituo vya njiani ili kufika katika muda uliopangwa.
2. Tatizo baada ya kudhibiti mwendo kuepusha ajali hiyo concept ya express haipo tena. Matokeo yake abiria wa kujaza basi kila siku wa express wanapungua. Kwahiyo wahusika wanajazia viti kwa abiria wa njiani.
3. Kwahiyo kama unapanda basi ya mbali badala ya ile ya vituo vya njiani mhusika ni hiari yako akutoze nauli ya final destination hana kosa.
 
Umezungumzia kuhusu express, je vijijini, ukiacha daladala mijini?
1. Basi likiandikwa Arusha - Dar (express) kinadharia halistahili kusimama simama vituo vya njiani ili kufika katika muda uliopangwa.
2. Tatizo baada ya kudhibiti mwendo kuepusha ajali hiyo concept ya express haipo tena. Matokeo yake abiria wa kujaza basi kila siku wa express wanapungua. Kwahiyo wahusika wanajazia viti kwa abiria wa njiani.
3. Kwahiyo kama unapanda basi ya mbali badala ya ile ya vituo vya njiani mhusika ni hiari yako akutoze nauli ya final destination hana kosa.
 
Back
Top Bottom