Bengalisis
JF-Expert Member
- Jun 8, 2018
- 1,847
- 2,768
JICHO HILI LINAPOTEA
Nikiwa mdogo, Mama yangu alikuwa anawasiliana nami kwa macho, bila kutamka na nilikuwa namuelewa vizuri!!
Jicho hilo silioni siku hizi miongoni mwa akina mama.
Ilikuwa wageni wakija nyumbani, mimi kama narukaruka na kucheza mbele ya wageni bila staha, kulikuwa na namna fulani ya mama kuniangalia ilimaanisha "toka hapa". Nilielewa mara moja na kutii!
Ilikuwa wageni wakila chakula nami kutaka kudowea, basi kulikuwa na uangaliaji wa mama ambao ulimaanisha " ukijaribu tu nitakuchuna ngozi ukiwa hai!" lakini wakati huohuo kwa wageni uso wake ulimaanisha "endeleeni tu, huyu dogo ameshakula."
Ilikuwa mkiwatembelea ndugu na ukataka kulilia kitu cha watu, kulikuwa na jicho fulani hivi toka kwa mama lililoonyesha kuwa "Ukifanya ng'ee tu tukifika nyumbani nitakukaba shingo, sitaki ujinga"
Lakini wanawake wa leo, namaanisha akina mama wa leo ehhh..., vioja. Macho yao yamepofushwa na nini sijui..! Labda ni hizi kope za bandia wanazozivaa au hizi rangi wanazopaka kwenye nyusi!!
Kusema ukweli macho yao hayana mawasiliano na watoto wao.
Wazazi wetu wa zamani, Mungu awajaalie maisha marefu. Ninyi ndo mlitutengeneza tukawa hivi tulivyo leo. Hatuna tamaa ya vitu vya watu.
Nakala:
- Wanaume wote
- Akina mama vijacho wote
Nikiwa mdogo, Mama yangu alikuwa anawasiliana nami kwa macho, bila kutamka na nilikuwa namuelewa vizuri!!
Jicho hilo silioni siku hizi miongoni mwa akina mama.
Ilikuwa wageni wakija nyumbani, mimi kama narukaruka na kucheza mbele ya wageni bila staha, kulikuwa na namna fulani ya mama kuniangalia ilimaanisha "toka hapa". Nilielewa mara moja na kutii!
Ilikuwa wageni wakila chakula nami kutaka kudowea, basi kulikuwa na uangaliaji wa mama ambao ulimaanisha " ukijaribu tu nitakuchuna ngozi ukiwa hai!" lakini wakati huohuo kwa wageni uso wake ulimaanisha "endeleeni tu, huyu dogo ameshakula."
Ilikuwa mkiwatembelea ndugu na ukataka kulilia kitu cha watu, kulikuwa na jicho fulani hivi toka kwa mama lililoonyesha kuwa "Ukifanya ng'ee tu tukifika nyumbani nitakukaba shingo, sitaki ujinga"
Lakini wanawake wa leo, namaanisha akina mama wa leo ehhh..., vioja. Macho yao yamepofushwa na nini sijui..! Labda ni hizi kope za bandia wanazozivaa au hizi rangi wanazopaka kwenye nyusi!!
Kusema ukweli macho yao hayana mawasiliano na watoto wao.
Wazazi wetu wa zamani, Mungu awajaalie maisha marefu. Ninyi ndo mlitutengeneza tukawa hivi tulivyo leo. Hatuna tamaa ya vitu vya watu.
Nakala:
- Wanaume wote
- Akina mama vijacho wote