Bi. Kiroboto
Member
- Dec 22, 2011
- 36
- 6
Tangu mwaka jana kumekuwa na taarifa kwamba serikali inafanya utaratiwa utakaoiwezesha kudhibiti ulipaji mishahara kwa watumishi hewa. Njia pekee na rahisi iliyokusudiwa kutumika ni kupanga siku ambapo watumishi wote watatakiwa kufika katika maeneo yao ya kazi. Itakuwa ni mwisho wa mwezi ambapo watumishi watapokelea mishahara yao ofisini kwa mwajiri wao badala ya pesa kuingizwa ktk akaunti zao; ni kwa utaratibu huu ambapo mtu/watu maalum watakuwa wanaorodhesha watumishi wote ambao watapana nafasi ya kuhudhuria kusanyiko hili. Haijaeleweka vizuri kwa watumishi wote iwapo zoezi hili litaanza na kumalizika lini. Binafsi mimi nimeongea na mwajiri wangu na amenidhibitishia kuwa ameishapokea barua kutoka wizarani na kwamba zoezi hili litafanyika hapa halmashauri kwetu mwishoni mwa mwezi huu(Jan). Binafsi, siungi mkono malipo kwa watumishi hewa. Ila tatizo langu lipo kwenye gharama na usubufu ambao baadhi ya watumishi watapata.Kwanza haijaeleweka zoezi hili litadumu kwa muda gani. Kinachofahamika ni kwamba endapo mtumishi atashindwa kuhudhuria zoezi hili, mshahara wake utasitishwa na atalazimika kufuatilia kwa gharama zake mwenyewe hadi hazina kuu ili kurejeshewa. Haijafahamika iwapo kutakuwepo na faini yoyote kwa wale watakaoshindwa kutekeleza kwa wakati zoezi hili au utaratibu utakaotumika ili kuwarejeshea tena ujira wao.Pili haijafahamika iwapo serikali itafidia gharama na usumbufu kwa baadhi ya watumishi wake waliopo likizoni, safarini, masomoni na baadhi ambao kwa bahati mbaya wakati wa zoezi hili watakuwa wagonjwa(mahututi) vitandani. Nimefikiria mtumishi ktk halmashauri ya wilaya Mafia ambaye yuko likizo Bukoba, mwenye mshahara wa Tsh 250000/= Na vipi mtumishi wa kipato kama hicho aliyefuata taratibu zote na kufanikiwa kwenda masomoni let's say Arusha wakati yeye anafanya kazi Mafia au Tandahimba. Ikubukwe kwamba tuna watumishi wengi sana wanaojisomesha kwa gharama zao wenyewe baada ya waajiri wao kuwaruhusu na kusema hawana hela ya kuwasomesha. Sitaki kuamini kwamba serikali hailitambui hili. Kimsingi kinachoonekana hapa ni kwamba mwanzo serikali imeishakiri kushindwa kudhibiti tatizo hili la watumishi hewa kwa kutumia utaratibu uliokuwepo miaka mingi. Sasa imeamua kumtwisha zigo mtumishi aliyejitolea kufanya kazi ktk mazingira magumu ambayo wengine wameyakimbia na ndio hao wanaoitwa hewa! Kwamba mtumishi wa Halmashauri ya wilya Mafia ambaye yupo masomoni Kilimanjaro atumie zaidi ya Tsh 200,000/= kusafiri kuja kusaini cheki ya Tsh 250,000/=??! This is nonsense. Hii ina tofauti gani na adhabu ya kawaida? Huyu mtumishi masikini kaikosea nini serikali yake? Mimi naona kosa lake ni pale alipokubali kufanya kazi katika mazingira ambayo wengine(wajanja) wamekimbia.Lakini, ndio tuamini kwamba serikali imekosa njia nyingine ya kudhibiti tatizo hili hadi imeamua kugawana zigo hili na watumishi wake-tena waaminifu kabisa? Je, tuamini kuwa hii ndiyo suluhu ya kudumu kwa tatizo hili? Je, haitakuja kuwa routine kila baada ya miaka kadhaa? Ushauri wangu kwa serikali, naamini inatambua adha ambayo baadhi ya watumishi watapata kutokana na zoezi hili, ijaribu kutumia njia mbadala ambayo haitaleta usumbufu kwa watumishi wake. Itazame gharama, usumbufu na muda atakaopoteza mtumishi wakati wa zoezi hili. Lakini pia itambue kuwa vyovyote itakavyokuwa bado lazima kutakuwepo na watumishi kadhaa watakaoshindwa kuhudhria zoezi hili. Fikiria mtumishi aliyelazwa mahututi hospitali, sina hakika ana nafasi gani ktk zoezi hili.Mimi nadhani serikali ni taasisi kubwa, ina uwezo mkubwa. Kwani inashindikana vipi hao watu watakaohusika na uhakiki huu ktk taasisi fulani kushugulikia watumishi wote bila kujali wanatokea wapi. Naamini siku hizi kuna maendeleo makubwa katika information technology. Watumishi wote wa serikali wamo kwenye database, sioni mantiki ya kunisafirisha kutoka Musoma kwenda Tandahimba kuhakikiwa ilhali nina kitambulisho na nyaraka zote muhimu za kiofisi zinazohalalisha uwepo wangu pale Musoma.Kama huamini fuatilia kwa muajiri wangu. Kwa mfano, ina maana serikali haijui idadi ya watumishi wao waliopo masomoni na vyuo walivyodahiliwa? Inashindwa vipi kuwahakiki huko waliko? Mimi nadhani umefika wakati iheshimu maslahi kidogo wanayopata watumishi wake. Sipendi kuona zoezi hili limekamilika likiwa limeacha mifuko ya watumishi mitupu.Hii haina tofauti na kulipia haki ya msingi ya mtumishi. Ningependa kuona zoezi hili likifanyika kwa utaratibu ambao utakuwa wa kudumu na njia ya kuhakiki watu iwe ya kisasa zaidi sio ya namna hii vijana wa kileo wanaita kuuza sura. Sipendi kuona zoezi hili muhimu kuendeshwa kwa zima moto.Mungu ibariki Tanzania...