Hili chuma hadi kukamilika kuwa road niandae bajet kiasi gani

Land Cruiser aisee Mjapan alijitahidi sana. Ninalo la mwaka 1996 na mpaka leo liko imara ajabu. Vinaharibika vitu vya pembeni tu lakini injini iko ngangari ajabu mpaka fundi ananiambia Land Cruiser hizi za mwanzo mwanzo injini zake zilikuwa imara sana na hutakaa uiharibu. Mpaka nimeamua kuligeuza pick up lipige shughuli za kubeba nyanya na dengu huko vijijini.

Nilisikitika niliposikia kuwa wameachana kuyatengeneza rasmi labda tu kwa oda maalum.
 
Kusema maigizo ya wasanii ndio umbea mkuu? Hivi uliona marehemu kanumba mambo yalivyokuja kuwa wazi? Alikuwa hana hata kiwanja cha miguu 15 kwa 20 halafu kwa nje alikuwa na Ma prado party za hatari,enzi zile 2009-2012 viwanja vilikuwa bei rihisi sana.
Wasanii sijui wanakwama wapi
 
Hiyo 109 hapo ni pamoja na kodi au bado hujalipa kodi?. Maana kwa Tz kodi ndio ununuzi wa gari lenyewe,achilia mbali ununuzi wa gari Japan na usafirishaji wake. Hizi gari zozote kwa wamalawi na zambia ni kama kuokota tu. Kodi iko chini kabisa,jiulize hapo hawana bandari. Sisi wenye bandari ni kama wakimbizi ndani ya nchi yetu kwa kodi za ajabu
Mimi huwa nashangaa sana kusikia mtu anatetea hii serikali ya tanzania, ukweli ni kwamba serikali inasababisha pakubwa sana ugumu wa maisha, hayo makodi yamekuwa yakitajwa kuwa makubwa sana kwenye kila eneo la maisha ya kila siku ya mtanzania, (sio kwenye magari tu).

Angalia sakata la cement, kuna uzembe na uhuni umefanyika na umepelekea kupanda kwa bei ya cement kwa wiki mbili sasa, Tra wameshindwa kutatua tatizo la mtandao kuwawezesha Dangote kuprint risiti za kielektroniki, anayeumia ni mwananchi maskini.

(Nafahamu kwamba wao wanaweza kununua cement hata kwa bei hii ya juu na hata ikipanda zaidi ya hapa, sijui sana kuhusu mambo ya zambia na malawi, lakini kamaulivyosema inaonesha kwamba huko wenzetu kodi zao ziko chini, ukiondoa kodo za ovyo zilizopo hapa nchini pana uwezekano makali ya maisha yakapungua.
 
habari wadau?

Katika kuperuzi kwenye site mbalimbali zauuzaji wa magari online nimekutana nahizi gari za wakubwa Toyota land cruiser V8 model ya 2017

Befoward wanataka kiasi cha pesa ML:109 na cent zake iliwakutumia hii gari je hapa kwetu Tanzania hawajamaa Kodi inaweza kukadiliwa kiasi gani? View attachment 1603807
Jibu nimelipata kudadekiiiii hiii nnchi yani kodi sawa nagari
Screenshot_20201118-120349.jpg
 
Mkuu mtazamo unatofautiana ndugu,,usifikiri kila mtu kwake kipaumbele ni ardhi na mashamba au nyumba wengine vipaumbele vyao biashara kwanza na magari halafu baadae ndo unakuta ana nunua hayo mashamba na viwanja.

Kanumba alikua na magari zaidi ya mawili na kampuni lakinaliishi kwenye nyumba amabayo alikua analipa pesa si chini ya laki kamakodi unataka kuniambia alishindwa kujenga nyumba angalau ya milioni 20? Au kuwa na kiwanja cha milioni 3?

Mfano mwinginekwa sasa huyu Diamond ana kampuni ambayo ina media na lebo ndani yake ,pia mwanamuziki na biashara zingine tusizozijua ana magari ya bei ndefu kwa pesa ya kibongo(hata kama ni ya mkopo) lakini amepanga jumba la kifahari usidhani kama labda hana nyumba au anashindwa kujenga nyumba ya milioni hata 50 bali mtu ana mipango yake.

Mfano wa mwisho mimi mwenyewe hapa sina mawazo kabisa ya kujenga lakini nina bishara ambayo nikigeuza kuwa kiwanja na pesa naweza jenga nyumba hata milioni 15M hivyo tuheshimu mitazamo na maisha ya watu wengine tuache kufuata ya mitandao.
Kusema maigizo ya wasanii ndio umbea mkuu? Hivi uliona marehemu kanumba mambo yalivyokuja kuwa wazi? Alikuwa hana hata kiwanja cha miguu 15 kwa 20 halafu kwa nje alikuwa na Ma prado party za hatari,enzi zile 2009-2012 viwanja vilikuwa bei rihisi sana.
 
Mkuu mtazamo unatofautiana ndugu,,usifikiri kila mtu kwake kipaumbele ni ardhi na mashamba au nyumba wengine vipaumbele vyao biashara kwanza na magari halafu baadae ndo unakuta ana nunua hayo mashamba na viwanja.

Kanumba alikua na magari zaidi ya mawili na kampuni lakinaliishi kwenye nyumba amabayo alikua analipa pesa si chini ya laki kamakodi unataka kuniambia alishindwa kujenga nyumba angalau ya milioni 20? Au kuwa na kiwanja cha milioni 3?

Mfano mwinginekwa sasa huyu Diamond ana kampuni ambayo ina media na lebo ndani yake ,pia mwanamuziki na biashara zingine tusizozijua ana magari ya bei ndefu kwa pesa ya kibongo(hata kama ni ya mkopo) lakini amepanga jumba la kifahari usidhani kama labda hana nyumba au anashindwa kujenga nyumba ya milioni hata 50 bali mtu ana mipango yake.

Mfano wa mwisho mimi mwenyewe hapa sina mawazo kabisa ya kujenga lakini nina bishara ambayo nikigeuza kuwa kiwanja na pesa naweza jenga nyumba hata milioni 15M hivyo tuheshimu mitazamo na maisha ya watu wengine tuache kufuata ya mitandao.
Sawa mkuu nimekupata!! Naheshimu mawazo yako!
 
Back
Top Bottom