Hiki ni kiti cha dhahabu alichokalia Malkia Victoria wakati anaapishwa

View attachment 2224792
Ilibidi miguu ya kiti itengenezwe mifupi kwasababu Malkia Victoria alikua mwanamke mfupi kwa umbo, wasingeweza kuweka miguu ya kiti mirefu na kumuacha Malkia akining’inia.

Baada ya Victoria alitawala mtoto wake Edward, nae alipokewa na mtoto wake George V aliyerithiwa na mtoto wake Edward ambae ilibidi aachie kiti baada ya kumuoa mwanamke wa Kimarekani tena aliyetalakiwa. Kitendo hiki kilisababisha Albert ambae ni baba yake Malkia Elizabeth kuapishwa kama Mfalme George wa sita.

Sasa hivi Malkia Elizabeth katika umri wa miaka 96 jua limezama na nguvu za kutawala zimemwishia. Mtoto wake Charles anajiandaa kuapishwa. Nimeona kiti cha enzi kimetolewa inawezekana kinapigwa msasa kwa maandalizi ya sherehe ya kusimikwa rasmi kwa Charles kama Mfalme.

Charles atataka miguu ya kiti iongezwe? Wakati kiti kinatengenezwa Uingereza ilikua na Madola 3/4 ya dunia, hivyo kupata dhahabu ya kutengeneza kiti cha Enzi haikua shida. Sasa hivi mambo yamebadilika. Hata dhahabu ikipatikana wana harakati watapaza sauti na kuhoji ulazima wa kutumia dhahabu kutengeneza miguu ya kiti cha Mfalme.
USA ilikuwa koloni kubwa la UK, kwanini sio mwanachama wa jumuiya ya madola ?
 
Na mzungu alitengeneza hizi whsp insta style na the likes plus malinks kuwakamata wavivu wa kiafrika wasioependa kusoma wenye kupenda summary badala ya details.
Na anatupiga sana kwa kutoyachimba maarifa
Mbona wao wako addicted na hayo makitu kuliko sisi tena sisi tuko na poor access ya hayo matknolojia yao tuache unyonge wakujisingizia kila kitu chenye side effects kwa wanadamu kimeletwa kuwalemaza waafrika
 
USA ilikuwa koloni kubwa la UK, kwanini sio mwanachama wa jumuiya ya madola ?
Nashukuru sana hata mimi sijawahi kupata wazo la kufiria jambo hili.Pia huwa nawaza NATO kirefu chake ni Northen Atlantic Treaty Organization yaani mkataba wa muungano wa nchi zilizo Kaskazini mwa bahari ya Atlantic sasa huwa nawazaga inakuwaje nchi za ulaya ziko umoja huu lakini kiramani bahari ya Atlantic haiko kwao.Hebu ngoja nichimbe nitarudi baadae nianike majibu kwenye mkeka.Huu ndio uzuri wa JF
 
USA ilikuwa koloni kubwa la UK, kwanini sio mwanachama wa jumuiya ya madola ?
Nashukuru sana hata mimi sijawahi kupata wazo la kufiria jambo hili.Pia huwa nawazo NATO kirefu chake ni Northen Atlantic Treaty Organization yaani mkataba wa muungano wa nchi zilizo Kaskazini mwa bahari ya Atlantic sasa huwa nawazaga inakuwaje nchi za ulaya ziko umoja huu lakini kiramani bahari ya Atlantic haiko kwao.Hebu ngoja nichimbe nitarudi baadae nianike majibu kwenye mkeka.Huu ndio uzuri wa JF
 
Why USA is not part of Commonwealth?


While the USA was a part of British empire but it did not leave like other countries like Canada, new Zealand. USA Gaines independence way earlier than those countries, so when commonwealth was formed, USA had moved far away from culture, political influence of Britain, so they did not join.
 
Incase akidondoka haya yafuatayo yameshaandaliwa.

Baada ya kifo cha Malkia mtu wa kwanza kupewa taarifa ukitoa wanafamilia na madaktari, atakuwa ni secretari wa Malkia mwenyewe Sir Christopher Geidt. Baada ya hapo atamtarifu waziri mkuu na baadae maafisa waandamizi wa serikali kwa kutumia sentensi THE LONDON BRIDGE IS DOWN taarifa hii ataituma kwa kutumia simu maalumu.

Baada ya hapo ofisi ya mambo ya nje itatoa taarifa kwa nchi zote wanachama wa jumuia ya Madola ambazo Malkia ndio kiongozi mkuu, vyombo vya habari vitatarifiwa kupitia Umoja wa vyombo vya habari, shirika la habari la Uingereza( BBC) na baada ya kupata taarifa hizo waendesha vipindi watalaazimika kupiga wimbo maalumu kama maandalizi ya kutoa habari hiyo! Kuna habari kuwa vyombo vya habari vya The Times na Sky News vimekuwa vikifanyia mazoezi oparesheni hiyo huku wakitumia jina Mrs Robinson badala ya Malkia Elizabeth II.

Baadae taarifa ikiwa kwenye karatasi itawekwa kwenye geti la kuingilia kasri la Buchngham ambayo ndo offisi kuu ya ufalme wa Uingireza na muda huo huo tovuti ya Buchngham itaweka taarifa hiyo na Bunge litaitishwa ikiwezekana ndani ya saa moja ambapo waziri mkuu atalihutubia bunge la makabwela( The House of Commons). Siku moja baada ya kifo cha Malkia Elizabeth II baraza maalumu kwa ajiri ya kumuidhinisha Mfalme au Malkia mpya litakutana katika kasri la S. James na jioni ya siku hiyo bunge litakutana kwa ajili ya kumuidhinisha Mfalme au Malkia mpya!

Utaratibu kama Malkia atafia nje ya Kasri la Kifalme la Buckngham Kama atafia kwenye kasili la Windsor ambalo ni sehemu ya Mali za ufalme au kwenye Nyumba ya Sundningham ambayo ni Nyumba binafsi ya Malkia Elizabeth II, basi mwili wa Malkia utapelekwa Buchngham kwa gari. Kama Malkia atafia nje ya Uingereza basi mwili utapelekwa Uingereza na kikosi cha “The No:32 (the Royal) Squadron” ambalo ni jeshi maalumu la anga kwa ajiri ya familia ya kifalme kupitia uwanja maalumu ulioko eneo la South Ruislip!! Kama Malkia atafia kwenye kasri la Balmoral liliopo Scotland mwili utapelekwa kwenye Cathedral ya mtakatifu Giles na baadae kuchukuiliwa na treni maalumu ya kifalme na kuletwa mjini London! Katika mazingira yoyote yale mwili utachukukiwa na kupelekwa katika kasri la Buckingham ndani ya siku 4.

Mwili wa Malkia utaagwa kitaifa katika eneo la “Westminster abbey” siku tisa baada ya kifo na baadae atazikwa kwenye Jeneza katika kanisa la Mtakatifu George lililopo kwenye Kasri la Windsor.[

/QUOTE]Waingereza ni watu wanaojipenda na wanaheshimu mila na desturi zao sana.
Ni watu smart na nadhifu mno.
 
Daah malkia anaishi maisha magumu sana kiroho akifahamu wengi wanasubiria kifo chake kwa hamu. Kishuhudia maandalizi ya warithi wake,akishuhudia eneo atakalozikwa.

Utajiri pekee ni Amani ya moyo.
Mkuu umewaza kiroho na kitakatifu zaidi.
 
Incase akidondoka haya yafuatayo yameshaandaliwa.

Baada ya kifo cha Malkia mtu wa kwanza kupewa taarifa ukitoa wanafamilia na madaktari, atakuwa ni secretari wa Malkia mwenyewe Sir Christopher Geidt. Baada ya hapo atamtarifu waziri mkuu na baadae maafisa waandamizi wa serikali kwa kutumia sentensi THE LONDON BRIDGE IS DOWN taarifa hii ataituma kwa kutumia simu maalumu.

Baada ya hapo ofisi ya mambo ya nje itatoa taarifa kwa nchi zote wanachama wa jumuia ya Madola ambazo Malkia ndio kiongozi mkuu, vyombo vya habari vitatarifiwa kupitia Umoja wa vyombo vya habari, shirika la habari la Uingereza( BBC) na baada ya kupata taarifa hizo waendesha vipindi watalaazimika kupiga wimbo maalumu kama maandalizi ya kutoa habari hiyo! Kuna habari kuwa vyombo vya habari vya The Times na Sky News vimekuwa vikifanyia mazoezi oparesheni hiyo huku wakitumia jina Mrs Robinson badala ya Malkia Elizabeth II.

Baadae taarifa ikiwa kwenye karatasi itawekwa kwenye geti la kuingilia kasri la Buchngham ambayo ndo offisi kuu ya ufalme wa Uingireza na muda huo huo tovuti ya Buchngham itaweka taarifa hiyo na Bunge litaitishwa ikiwezekana ndani ya saa moja ambapo waziri mkuu atalihutubia bunge la makabwela( The House of Commons). Siku moja baada ya kifo cha Malkia Elizabeth II baraza maalumu kwa ajiri ya kumuidhinisha Mfalme au Malkia mpya litakutana katika kasri la S. James na jioni ya siku hiyo bunge litakutana kwa ajili ya kumuidhinisha Mfalme au Malkia mpya!

Utaratibu kama Malkia atafia nje ya Kasri la Kifalme la Buckngham Kama atafia kwenye kasili la Windsor ambalo ni sehemu ya Mali za ufalme au kwenye Nyumba ya Sundningham ambayo ni Nyumba binafsi ya Malkia Elizabeth II, basi mwili wa Malkia utapelekwa Buchngham kwa gari. Kama Malkia atafia nje ya Uingereza basi mwili utapelekwa Uingereza na kikosi cha “The No:32 (the Royal) Squadron” ambalo ni jeshi maalumu la anga kwa ajiri ya familia ya kifalme kupitia uwanja maalumu ulioko eneo la South Ruislip!! Kama Malkia atafia kwenye kasri la Balmoral liliopo Scotland mwili utapelekwa kwenye Cathedral ya mtakatifu Giles na baadae kuchukuiliwa na treni maalumu ya kifalme na kuletwa mjini London! Katika mazingira yoyote yale mwili utachukukiwa na kupelekwa katika kasri la Buckingham ndani ya siku 4.

Mwili wa Malkia utaagwa kitaifa katika eneo la “Westminster abbey” siku tisa baada ya kifo na baadae atazikwa kwenye Jeneza katika kanisa la Mtakatifu George lililopo kwenye Kasri la Windsor.
Asante,Huu muongozo wa kifo huwa upo wazi sikuzote?na kwanini atazikwa kanisani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom