Hiki Kingereza cha Wasanii wetu kwenye Instagram accounts zao ni cha wapi?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,378
26,700
Wakuu, mi nauliza tu!

Hawa ni mastaa wetu, ‘vioo’ vya jamii. Basi wengi wao hupenda ku-name akaunti zao ‘official’.

Yaani kila msanii ana prefix- au suffix- official, hata wale uchwara atajiita ‘officialuchwara’ au ‘utopoloofficial’.

Napata tabu huenda mimi sielewi, na wala siioni huko kwa mabeberu tunakojifunza. Wajuvi nijuzeni, nami nipate kujua.

Nini maana ya kuwa ‘official’ kwenye hizi kurasa zetu?

Asanteni.
 
Wabongo wanapenda kufungua akaunti kwa kutumia majina yao...parody kibao. Wakaona kuweka neno official ndio dawa.
 
Wakuu, mi nauliza tu!

Hawa ni mastaa wetu, ‘vioo’ vya jamii. Basi wengi wao hupenda ku-name akaunti zao ‘official’.

Yaani kila msanii ana prefix- au suffix- official, hata wale uchwara atajiita ‘officialuchwara’ au ‘utopoloofficial’.

Napata tabu huenda mimi sielewi, na wala siioni huko kwa mabeberu tunakojifunza. Wajuvi nijuzeni, nami nipate kujua.

Nini maana ya kuwa ‘official’ kwenye hizi kurasa zetu?

Asanteni.
Kwa wasanii wakubwa let's say Nasibu Abdul (diamond) , Juma Jux na wengineo ukiingia Kwenye mitandao kama IG, FB n.k utakutana na Accounts nyingi zenye majina hayo ambazo nyingi ni "fan pages" ndio maana wakaamua kuweka official ili kutofautisha ama kuonyesha kuwa hizo ni rasmi.

kidogo utakuwa umepata mwanga sio?
 
Kwa wasanii wakubwa let's say Nasibu Abdul (diamond) , Juma Jux na wengineo ukiingia Kwenye mitandao kama IG, FB n.k utakutana na Accounts nyingi zenye majina hayo ambazo nyingi ni "fan pages" ndio maana wakaamua kuweka official ili kutofautisha ama kuonyesha kuwa hizo ni rasmi.

kidogo utakuwa umepata mwanga sio?
Mbona diamond anatumia diamond platinumz na sio official...?
 
Back
Top Bottom