Hiki anachofanya Masanja Mkandamizaji sio sahihi kabisa

adakiss23

JF-Expert Member
Jan 23, 2011
4,477
4,270
Kuna video imesambaa mtandaoni ikimuonyesha Masanja Mkandamizaji na vijana wengine nadhani ni wafuasi wake katika kanisa lake lile liko pale Leaders club. Clip inaonyesha wako ktk shule fulani nmeshindwa kujua ni shule gani exactly lakini kwa mazingira inaweza kuwa Arusha, anaonekana Masanja anaomba na watoto wanaanguka kimapepo.

Hii kitu sio sahihi kabisa kwa mazingira ya eneo la elimu na pia kwa mazingira ya watoto wadogo. Sijui uongozi wa shule waliweka wapi akili na fikra zao kuruhusu hili.

Binafsi nmeona ni jambo lisilo na mantiki kabisa. Sioni kabisa logic ya hii kitu kabisa. Inaweza kuleta madhara ya kisaikolojia hapo baadae kwa wanafunzi na hata shule husika pia.

Tunajua jinsi baadhi ya watu wanaojiita watumishi wa Mungu kutumia nguvu tofauti tofauti kujifanya wanakemea mapepo na watu wakianguka ovyo, huwa sijui lengo hasa ni lipi lakii kwa watu wazima wenye akili timamu ambayo hawajapelekwa pale kwa bakora, walienda kwa matakwa yao ni sawa.

Lakini kwa watoto wadogo kama wale hakika sio jambo sahihi kabisa. Unless hiyo shule iwe na shida fulani inayohitaji maombi kama yaliyofanywa na Masanja na watu wake.

Lakini kwa uchunguzi kidogo nimebaini ni kama tour huyu Masanja anafanya katika mashule kufanya anachokifanya. Hapa namaanisha kuzunguka katika mashule na kuombea na watoto kuanguka ovyo. Nadhani si sahihi na shule sio eneo sahihi kwa haya anayofanya Masanja.

Naona ni busara kwa wenye mamlaka kuzuia hii kitu kufanyika katika mashule.
 
Hayo hayakua maombi? Labda unataka serikali ipinge marufuku Dini za wenzetu......ndo jinsi wanavo omba brother
Maombi kwa muktadha wa kujua na kueneza neno la Mungu sidhani ni tatizo. Hilo jambo lipo. Mashehe kwa wachungaji kufundisha n kuabudu mashuleni lakini hili ni tofauti. Huku ni kukemea mapepo kwa makanisa ya mitaani yafanyavyo. Nmeshindwa kuiweka hapa ile clip jaribu kuitafuta utaiona then utajua ninachozungumzia
 
Nani alikudanganya kwamba kukemea pepo kwa jina ka Yesu ni kazi ya makanisa ya mitaani ? Unaweza kuniambia hapa nini maana ya makanisa ya mitaani ? Kazi ya kukemea pepo iliagizwa na kufanywa na Yesu mwenyewe, leo unatuambiaje wewe ? Kama huna cha kuposti ni bora ukaacha kuandika upuuzi kama huu. Ninakushauri uokoke ili Yesu awe Bwana na Mwokozi wako.
Maombi kwa muktadha wa kujua na kueneza neno la Mungu sidhani ni tatizo. Hilo jambo lipo. Mashehe kwa wachungaji kufundisha n kuabudu mashuleni lakini hili ni tofauti. Huku ni kukemea mapepo kwa makanisa ya mitaani yafanyavyo. Nmeshindwa kuiweka hapa ile clip jaribu kuitafuta utaiona then utajua ninachozungumzia
 
Sijawahi.kuwa mfuasi wala shabiki.wa hizo mambo zao.
Uko sahihi kabisa. Hawa watu kuna ujanja wanatumia (siyo uchawi). Ni aina ya ''mazingaombwe'' fulani na ndiyo maana anaenda mashuleni kwa sababu anajua ili apate matokeo mazuri sehemu kama shule ni muhimu. Anatakiwa apigwe marufuku kabisa huyu tapeli. Ibada asuburi watu wajinga huko huko kanisani kwake na asipewe nafasi nje ya hapo. Hao watoto kwa makadirio wana umri gani?
 
Nani alikudanganya kwamba kukemea pepo kwa jina ka Yesu ni kazi ya makanisa ya mitaani ? Unaweza kuniambia hapa nini maana ya makanisa ya mitaani ? Kazi ya kukemea pepo iliagizwa na kufanywa na Yesu mwenyewe, leo unatuambiaje wewe ? Kama huna cha kuposti ni bora ukaacha kuandika upuuzi kama huu. Ninakushauri uokoke ili Yesu awe Bwana na Mwokozi wako.
Kwanza usinibwatukie. Nikuulize kitu labda utajielewa na kuacha kubwatuka. Wakati wa ukuaji wako (utoto wako) uliwahi kushuhudia uotaji wa haya makanisa mitaani kama ilivyo sasa? Kulikuwa na makanisa rasmi na yanajulikana. Nadhani jibu umelipata.
 
Lakini kwa uchunguzi kidogo nimebaini ni kama tour huyu Masanja anafanya katika mashule kufanya anachokifanya. Hapa namaanisha kuzunguka katika mashule na kuombea na watoto kuanguka ovyo. Nadhani si sahihi na shule sio eneo sahihi kwa haya anayofanya Masanja.
Waache waanguke tu alimradi awaandalie pakuangukia pawe salama wasije wakabamiza vichwa
 
Back
Top Bottom