halafu ilitekekezwaje hapo wizarani kwao? Kwa 100% ? Iliwasaidiaje watanzania kwa kipindi cha 2010- 2015? Ni aibu kulisemea siyo? Siku nyingine ukiwa na bunch of theories na ukaziapply kwa miaka kumi then ukajievaluate na kujikuta efficiency is below average unazitupilia mbali na kuja na idea mpya. Hiyo ilani yenu ilishafeli for almost 50+ years why mnaendelea kuja nazo zilezile?Nadhan ungesikiliza hotuba ya raisi siku wakuu wa wilaya walipokua ikulu usingepata shida. Moja ya majukumu aliyowapa ni kuhakikisha yaliyomo kwenye ilani yanasimamiwa na kutekelezwa. Ilan inayotekelezwa ni ya chama kilichoshinda, kwa hiyo hapo hakuna jipya. Kwa kuweka kumbukumbu sawa mwaka 2010 Mh Magufuli(alipoteuliwa kua waziri wa ujenzi) na Mh. Mwakyembe(alipoteuliwa kua Naibu waziri) wakati wanaenda wizarani kwako mda mfupi baada ya kuapishwa walienda na ilani ya ccm na Mh. Magufuli mwenyewe aliwambia watendaji wakuu waliokuwepo kuipitia vizuri ilani hiyo na kuhakikisha inatekelezwa ndani ya miaka mitano.
Hivi ni kweli? Hivi rais hazioni kasoro hizi za waziwazi? Waziri mkuu yabidi utoe semina elekezi kwa hawa wakuu wako wa mkoa na wilaya vinginevyo ni mahoka haya!
Makonda, hao ni watendaji na waajiriwa wa serkali kuu na siyo makatibu wa ccm. Kuwapa ilani ya ccm ni kuwatuma kuwatumikia wanaccm tu. Hii siyo haki na hsikubaliki. Haijawahi kutokea popote katika historia ya taifa hili tangu ukoloni. Magavana popote duniani hukabidhiwa katiba ya nchi na ilani huikuta kwenye ofisi za chama waendako. Mamlaka husika kemeeni mikurupuko hii kwani hata mkilazimisha kupendwa kwa ccm haiwezekani tena.
Kati ya wale wanaojua wanajua' Kumbe hajui ni pamoja na wewe!Ilan anapewa mtumishi wa chama husika na sio mtumishi wa serikali ndg! Cheo cha mkuu wa wilaya sio chakichama na mtu yoyote anaweza kuwa sio lazima we wa chama tawala hizi ni nafasi za uteuzi
Ni kama alivyoteuliwa mbunge Mbatia na Kikwete halaf apewe ilan ya CCM??
kwa iyo mpaka wale wajeda wa uDC ni lumumba dam damUnapochagu Chama katika Uchaguzi unakua unachagua Ilani.
Chama kinachoshinda Uchaguzi (nafasi ya rais) ndicho amabcho Ilani yake hutumika.
Shangaa sasa mtumishi wa serikali anapewa ilani ya chama hii iko bongo pekee
nimeipenda hii na ndiko tunako elekeaItafika Mahali mtatuambia mkuu wa Mkoa na wilaya+ Jeshi la wanachi na vingozi na watumishi hadi TRA na KADA ZOTE! wapewe Kadi na Irani za ccm
swali la msingi ni je mkuu wa wilaya ni mtumishi wa uma au wa chama?Kwani serikali inatekeleza ilani ya nani? Hata meya wa kinondoni anatekeleza hiyo.
swali la msingi ni je mkuu wa wilaya ni mtumishi wa uma au wa chama?
Umesahau na mabalozi nje ya nchiJamani cheo cha mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa ni vya ma kada tu wa ccm sasa mimi sishangai viongozi wa ccm kuvunja taratibu
Irani?????Irani ya Ccm!!!!!!!!! Naomba kujuzwa kama Chenge.. Tibaijuka... Ngereja... Lugemalira... Seth Singh... First lady aliyechuma ktk Enjios fulani! nk wote wamepewa Irani?