Hii ya kugharamia msiba iko siku itabuma tu, anzeni kutafuta mbadala!

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330
Binti Akwilina Akwilini amefariki ni mwezi na nusu sasa hatujasikia Askari waliosababisha kifo chake wakichukuliwa hatua wala yeyote yule kuwajibika kutokana na kifo chake kilichosababishwa na uzembe na matumizi mabaya ya vyombo vya dola.

Kikubwa Serikali walichoona wanaweza kuifanyia familia yake ni kugharamia msiba tena kwa 'kuwachoresha' ndugu zake kwenye mitandao(inauma). Kwa ninavyoijua Tanzania ndo imetoka hiyo. Wakihoji sana ni sisi jamii tutakaowaambia " kwani mkilalamika itamrudisha?"

Kwa mara nyingine tena juzi amefariki kijana Allen huko Mbeya na inasemekana kifo chake kina mkono wa wale wale wahusika wa kwa Akwilina ingawa tofauti na wale wa Akwilina ambao walikiri (Rejea: Polisi yakiri kupiga mtu risasi maandamano ya CHADEMA ) kabla ya kuyakana maneno yao, hawa wamekataa katu katu.

Cha kushangaza, Mkuu wa Wilaya William Ntinika ameahidi Serikali itagharamia msiba na kutoa magari ya kusafirisha wafiwa.

Hivi kama Serikali inashindwa kujua hitaji la mfiwa akiwa katika kipindi kigumu, hasa ambaye kifo cha mpendwa wake kimegubikwa na utata na hisia za unyama je itajua nini tunahitaji nini kama Watanzania?

Wafiwa hawa wanachotaka zaidi ya usafiri wa kwenda kuzika na chakula ni 'closure'. Wajue nini hasa kilitokea, nani alisababisha na ameishia wapi. Wanahitaji pole lakini zaidi wanahitaji SAMAHANI! Na si kuwazidishia unyonge na kuwafanya wajihisi hawawezi kuhoji kitu kwa kuwapa vimsaada.

Je, leo mkisababisha kifo cha mtoto wa jirani yetu Baba Furaha ambaye ana pesa za kukodi hata ndege kumsafirisha mwanae kwenda mkoani mtampa vimilioni vyenu mkitegemea 'yaishe'?
 
Binti Akwilina Akwilini amefariki ni mwezi na nusu sasa hatujasikia Askari waliosababisha kifo chake wakichukuliwa hatua wala yeyote yule kuwajibika kutokana na kifo chake kilichosababishwa na uzembe na matumizi mabaya ya vyombo vya dola.

Kikubwa Serikali walichoona wanaweza kuifanyia familia yake ni kugharamia msiba tena kwa 'kuwachoresha' ndugu zake kwenye mitandao(inauma). Kwa ninavyoijua Tanzania ndo imetoka hiyo. Wakihoji sana ni sisi jamii tutakaowaambia " kwani mkilalamika itamrudisha?"

Kwa mara nyingine tena juzi amefariki kijana Allen huko Mbeya na inasemekana kifo chake kina mkono wa wale wale wahusika wa kwa Akwilina ingawa tofauti na wale wa Akwilina ambao walikiri (Rejea: Polisi yakiri kupiga mtu risasi maandamano ya CHADEMA ) kabla ya kuyakana maneno yao, hawa wamekataa katu katu.

Cha kushangaza, Mkuu wa Wilaya William Ntinika ameahidi Serikali itagharamia msiba na kutoa magari ya kusafirisha wafiwa.

Hivi kama Serikali inashindwa kujua hitaji la mfiwa akiwa katika kipindi kigumu, hasa ambaye kifo cha mpendwa wake kimegubikwa na utata na hisia za unyama je itajua nini tunahitaji nini kama Watanzania?

Wafiwa hawa wanachotaka zaidi ya usafiri wa kwenda kuzika na chakula ni 'closure'. Wajue nini hasa kilitokea, nani alisababisha na ameishia wapi. Wanahitaji pole lakini zaidi wanahitaji SAMAHANI! Na si kuwazidishia unyonge na kuwafanya wajihisi hawawezi kuhoji kitu kwa kuwapa vimsaada.

Je, leo mkisababisha kifo cha mtoto wa jirani yetu Baba Furaha ambaye ana pesa za kukodi hata ndege kumsafirisha mwanae kwenda mkoani mtampa vimilioni vyenu mkitegemea 'yaishe'?
Taifa lenu limejaa wajinga
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, William Ntinika amefunguka na kuweka wazi kuwa serikali itagharamia mazishi ya kijana Alen Achiles (20), aliyefariki muda mfupi baada ya kutoka polisi.

Mkuu wa wilaya huyo ambaye alifika nyumbani kwa wazazi wa marehemu na kutoa rambirambi ya laki mbili na kuahidi kuwa serikali itagharamia mazishi ya kijana huyo ikiwa pamoja na kukodi gari la matangazo pamoja na chakula

Serikali haipaswi kuishia hapo inapaswa kutoa adhabu kali kwa wahusika, na pia kuangalia upya njia mbadala wa kufanya operation zake bila kuathiri maisha ya watu,

Inauma kama mzazi au ndugu wa mtu kupotea alafu majibu ni kwamba watagharamia.mazishi,

FB_IMG_1522222226768.jpg
 
Nenda kabadilishe Pedi huko! Hata wasingetoa ghalama ungekuja kuponda tuu.
 
Nyinyi "mumpyupyu" halafu mugharimie mazishi, hiyo imekaaje Wakuu??
 
hakuna namna ni ishara ya kutapatapa kwa serikali yetu. wanakana hawajahusika na mauaji ila wako tayar kuugalamia msiba wa mtu aliye jifia peke yake. yaan hunidai ila nitakulipa!! hahahahaha nacheka kihutu mimi ila nikicheko cha maumivu
 
Hua sielewi kwa nini mtu awe polisi bado apigwe ili kutoa maelezo.

Kazi ya kukamata, kuhoji, kupeleleza na kupeleka mahakamani.

Cha ajabu polisi wetu kwenye kuhoji wanapiga watuhumiwa ili wawape maelezo zaidi, mwisho ndio hayo ya vifo.

Kuajiri watu wenye shule ndogo ni shida.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom