Hii ya Kibamba Serikali Imeyakoroga

longalonga

Member
Aug 22, 2007
17
2
Ndugu Zangu wana JF siku zote nimekuwa ni msikilizaji tu wa mambo humu ndani zaidi ya kuchangia threats zinazowekwa na wanamapambano wenzangu.

Labda nianze kwa kusema kuwa wengi wenu mnaifahamu vizuri ishu ya uchukuaji na uthaminishaji ardhi kwa wananchi wa kibamba,binafsi naipongeza serikali kupitia mipango miji kwa kutaka kuanzisha satelite city eneo la kibamba kwani hii pamoja na mambo mengine itasaidia kupunguza mrundikano wa shughuli zote katikati ya mji kwa sababu kulingana na masterplan niliyoichungulia nimeona hata stendi kuu ya mabasi itahamia huko pamoja na central facilities zote.

Tatizo lililonikera sana ni juu ya uthaminishaji na ulipaji wa fidia kwa wananchi ambao wamefanyiwa eviction hii kwa kweli imenisikitisha sana, mimi si mmoja wa waliokumbwa na mkasa huo na wala siishi maeneo hayo ila nimeshindwa kulifumbia macho kabisa.Kwa ufahamu wangu finyu wa sheria ya ardhi ya mwaka 1999 na Town Planning Ordinance serikali ikiamua kuchukua ardhi(acquisition)basi wananchi walio eneo hilo hukadiriwa malipo kulingana na bei iliyopo kwenye soko kwa muda huo.Chaajabu nikuwa pamoja na wathamini ardhi ambao wamesomea taaluma hiyo kufanya uthamini ambao ni Tsh 3000/= kwa mita moja ya mraba, serikali ilipangua uthamini huo na kupunguza hadi kufikia pungufu ya sh 500/=ambayo ni valuation rate ya miaka mingi iliyopita,na hivyo kuwanyonga sana wananchi ambao walikuwa na mategemeo makubwa kulingana na bei ya soko,mtu badala ya kulipwa lets say million thelathini (30,000,000/=) mtu analipwa chini ya milioni tano.(5,000,000/=).Eti wizara wanajisifu kuwa wamesave zaidi ya billion moja sijui ni kwa manufaa ya nani.

Hivi leo asubuhi jopo lote la wizara magufuli inclusive linaenda kibamba kuongea na wananchi baada ya kitimoto kikali sana jana wizarani.
Mimi kwa mtazamo wangu wana JF hili jambo si la watu wa kibamba tu, tusilifumbie macho hata kidogo sababu hii ardhi kwa sera zetu tumepangishwa tu, leo ni wale wa kibamba kesho ni sisi,serikali wataendelea kujineemesha kupitia migongo yetu daima.
Dodoma nao wanafuatia nina hakika wao ndo itakua worse kabisaaa.
Naomba Kuwasilisha.
 
Ndugu Zangu wana JF siku zote nimekuwa ni msikilizaji tu wa mambo humu ndani zaidi ya kuchangia threats zinazowekwa na wanamapambano wenzangu.

Labda nianze kwa kusema kuwa wengi wenu mnaifahamu vizuri ishu ya uchukuaji na uthaminishaji ardhi kwa wananchi wa kibamba,binafsi naipongeza serikali kupitia mipango miji kwa kutaka kuanzisha satelite city eneo la kibamba kwani hii pamoja na mambo mengine itasaidia kupunguza mrundikano wa shughuli zote katikati ya mji kwa sababu kulingana na masterplan niliyoichungulia nimeona hata stendi kuu ya mabasi itahamia huko pamoja na central facilities zote.

Tatizo lililonikera sana ni juu ya uthaminishaji na ulipaji wa fidia kwa wananchi ambao wamefanyiwa eviction hii kwa kweli imenisikitisha sana, mimi si mmoja wa waliokumbwa na mkasa huo na wala siishi maeneo hayo ila nimeshindwa kulifumbia macho kabisa.Kwa ufahamu wangu finyu wa sheria ya ardhi ya mwaka 1999 na Town Planning Ordinance serikali ikiamua kuchukua ardhi(acquisition)basi wananchi walio eneo hilo hukadiriwa malipo kulingana na bei iliyopo kwenye soko kwa muda huo.Chaajabu nikuwa pamoja na wathamini ardhi ambao wamesomea taaluma hiyo kufanya uthamini ambao ni Tsh 3000/= kwa mita moja ya mraba, serikali ilipangua uthamini huo na kupunguza hadi kufikia pungufu ya sh 500/=ambayo ni valuation rate ya miaka mingi iliyopita,na hivyo kuwanyonga sana wananchi ambao walikuwa na mategemeo makubwa kulingana na bei ya soko,mtu badala ya kulipwa lets say million thelathini (30,000,000/=) mtu analipwa chini ya milioni tano.(5,000,000/=).Eti wizara wanajisifu kuwa wamesave zaidi ya billion moja sijui ni kwa manufaa ya nani.

Hivi leo asubuhi jopo lote la wizara magufuli inclusive linaenda kibamba kuongea na wananchi baada ya kitimoto kikali sana jana wizarani.
Mimi kwa mtazamo wangu wana JF hili jambo si la watu wa kibamba tu, tusilifumbie macho hata kidogo sababu hii ardhi kwa sera zetu tumepangishwa tu, leo ni wale wa kibamba kesho ni sisi,serikali wataendelea kujineemesha kupitia migongo yetu daima.
Dodoma nao wanafuatia nina hakika wao ndo itakua worse kabisaaa.
Naomba Kuwasilisha.

Ni kweli kabisa.

Hili suala linahitaji mjadala wa kina kwa kuwa uhamishaji kama huu haujitokezi Kibamba tu, upo maeneo mbalimbali nchini.

Mosi, kuna suala la kutafuta suluhisho la muda mfupi katika sakata hili la Kibamba- jana nilitoa mapendekezo yangu kadhaa kuhusu nini ambacho ni vyema Waziri Magufuli akazingatia rejea http://www.chadema.net/blogu/mnyika/ inaelekea pia pamoja na mapungufu ya kisheria, kuna vitendo pia vya ufisadi na/au matumizi mabaya ya madaraka katika mchakato wa mradi hasa mintaarafu barua ya wahanga wa eneo hilo ya tarehe 3 Januari 2008 rejea http://www.ubungo.blogspot.com/ ; haya ni masuala ambayo yanaweza kufanyiwa kazi kwa haraka.

Pili; kuna masuala sasa ya kisera na kisheria- haya yanapaswa kujadiliwa kwa kina na kufanyiwa maamuzi kwa ajili ya faida ya baadae. Kuna suala la City Plan ya jiji la DSM na Manispaa zake; ingefikiriwa miaka mingi nyuma kwamba pangekuwa baadae na Sattellite City pale Kibamba tayari ardhi ingekuwa imeshatengwa na kusingekuja suala hili la mgogoro wa fidia kwa wananchi. Lakini pia kuna haja ya kuvijadili vipengele vya sheria vinavyohusu fidia kama vinakidhi haja.

JJ

Ps: Labda pia niwe wakili wa shetani- kwa misingi ya ukuaji wa DSM; je, kuna haja tena uwe Mkoa? Kwa nini tusiwe na Mkoa wa Kinondoni, Mkoa Wa Temeke, Mkoa wa Ilala? Ili kwa mfano wa Kinondoni; tuwe na wilaya ya Ubungo, Wilaya ya Kawe, na Wilaya ya Kinondoni?(kutokana na Jimbo la Kinondoni); Kama kukiwa na wilaya ya Ubungo, pengine hiyo sattellite town inayopangwa kujengwa Kibamba ndio ibebe makao makuu ya wilaya? je, mfumo utasaidia vipi katika kupeleka muundo wa kiserikali karibu zaidi na wananchi na kurahisha uratibu? Je, kwa vigezo vya mgawanyo wa wilaya; halmashauri ya Kinondoni inastahili bado kuwa wilaya au imeshavuka mipaka ya wilaya? Je, ni vyema kuwa na jimbo la Uchaguzi kama Ubungo ambalo linawapiga kura zaidi ya laki 3(kwa mwaka 2005) wakati majimbo yaliyomengi nchini yanawapiga kura si zaidi ya laki mbili? Tujadili!
 
nauunga mkono mpango wa kujenga satelite city kimara ..nasikia inakuwa wilaya ya KIMARA...tayari kuna chuo kikuu cha muhimbili wametoa tenda ya michoro kwa ajili ya chuo kikuu pale...pia catholics wana chuo kikuu pale cha st joseph engneering..so many prospects eneo lile hongera magufuli na rais wako jk....

nimetembea duniani nimeona miji inayojengwa kwenye vilima kama vya kibamba ..huwa inakuwa na scenery nzuri sana sana...tena kama wataweka open space za kutosha....pia napendekeza kibaha mjini iwe sehemu ya hii satelite city na makao makuu ya mkoa yahamie chalinze ,...pale wilaya ya kibamba makao makuu yawe kibaha mkoani....kuna barabara pia ya kufika bagamoyo toka kibamba ..another destination of satelite city....

lakini pia kuna umuhimu wa watu kulipwa kihalali...
 
nauunga mkono mpango wa kujenga satelite city kimara ..nasikia inakuwa wilaya ya KIMARA...tayari kuna chuo kikuu cha muhimbili wametoa tenda ya michoro kwa ajili ya chuo kikuu pale...pia catholics wana chuo kikuu pale cha st joseph engneering..so many prospects eneo lile hongera magufuli na rais wako jk....

nimetembea duniani nimeona miji inayojengwa kwenye vilima kama vya kibamba ..huwa inakuwa na scenery nzuri sana sana...tena kama wataweka open space za kutosha....pia napendekeza kibaha mjini iwe sehemu ya hii satelite city na makao makuu ya mkoa yahamie chalinze ,...pale wilaya ya kibamba makao makuu yawe kibaha mkoani....kuna barabara pia ya kufika bagamoyo toka kibamba ..another destination of satelite city....

lakini pia kuna umuhimu wa watu kulipwa kihalali...

Kaka

Hilo la wilaya ya Kimara, hata mimi nililisikia chini ya carpet. Lakini kuna watu wamefuatilia kwa karibu kwa Waziri husika na halmashauri inaelekea kuwa bado ni mazungumzo ya kwenye corridors tu; hakuna maamuzi ya mpango kama huo mpaka sasa.

Ingawa binafsi naunga mkono wazo kama hilo- ila sikubaliani na jina- wilaya ya Kimara; logically and administratively inapaswa kuwa wilaya ya Ubungo.

Ni kweli Muhimbili watajenga kule Kibamba milimani-si unakumbuka lile sakata la kumamishwa kwa wananchi wa Kwembe? Lakini hiyo Sattellite town haitakuwa kwenye vilima- kwa kuwa wamechagua haya maeneo ya karibu na barabara kuu- luguruni nk ambayo hayatapendeza sana kama wangepanda juu kidogo.

St Joseph haiko kimara wala kibamba; ipo Kata ya Mbezi- ndio maana mimi naona kama ni wilaya, basi inapaswa kuwa na wilaya ya Ubungo itakayounganisha yote haya kwa pamoja.

Kibaha walishakuwa na mipango yako ya kuhamamisha makao makuu ya wilaya; natumai walioko watatumwagia hapa. Na ndipo hapo kunapozuka tatizo la kufanya mambo kwa patches kutokana na kukosa well elaborate and long term master plan!


Tujadili

JJ
 
safi mheshimiwa john mnyika....katika hili naomba uwe sambamba na hawa wananchi ....na ikiwezekana serikali ishauriwe ifanye kongamano la wadau ili ipatikane a really nice satelite city.....nadhani pia wasikusahau na wewe kwani kila mtu anajua pale UBUNGO walikufanyia RAILASM.....nina jamaa zangu kule kila mmoja anashangaa kwanini hukushinda wewe wakati kila mtu anasema kura alikupa wewe...

usikate tamaa ...2010....MUNGU MKUBWA ...sauti itasikika!!!
 

Kwa ufahamu wangu finyu wa sheria ya ardhi ya mwaka 1999 na Town Planning Ordinance serikali ikiamua kuchukua ardhi(acquisition)basi wananchi walio eneo hilo hukadiriwa malipo kulingana na bei iliyopo kwenye soko kwa muda huo.Chaajabu nikuwa pamoja na wathamini ardhi ambao wamesomea taaluma hiyo kufanya uthamini ambao ni Tsh 3000/= kwa mita moja ya mraba, serikali ilipangua uthamini huo na kupunguza hadi kufikia pungufu ya sh 500/=ambayo ni valuation rate ya miaka mingi iliyopita,na hivyo kuwanyonga sana wananchi ambao walikuwa na mategemeo makubwa kulingana na bei ya soko,mtu badala ya kulipwa lets say million thelathini (30,000,000/=) mtu analipwa chini ya milioni tano.(5,000,000/=).Eti wizara wanajisifu kuwa wamesave zaidi ya billion moja sijui ni kwa manufaa ya nani.

Hapo kuna ulazima wa sheria za ardhi kuwekwa bayana... sheria nyingi na kanuni mbalimbali zimeendelea kufaidi vumbi makabatini. Ni kuziuja sheria hizo na kanuni, kwani itasaidia kuondoa dhuluma na aina zingine za ufisadi.

Pengine nifahamishwe ni nani mmiliki wa ardhi Tanzania Bara. Kule Tanzania Visiwani ardhi yote ni mali ya serikali(SMZ). Na iwapo itaichukua ardhi hiyo, fidia hulipwa kwa vipando vilivyomo tu ndani ya ardhi hiyo.
 
Hili katika yote limenipita , Mnyika go ahead na fanya mambo yako tunakusikilizia .
 
Ningependa kuwauliza, hivi DSM itaendelea kupendelewa mpaka lini?

Msongamano wa DSM hauwezi kupungua iwapo miji mingine haipewi kipa umbele. Kwanini mradi mzima usipelekwe Tanga, Mwanza, Mbeya au Bukoba.

Cha kushangaza zaidi ni kuwa wanaopanga mipango hiyo, wanatoka mbali na DSM na hata siku moja hawafikiri kuwa sehemu walizotoka zinahitaji miji vilevile.
 
Ningependa kuwauliza, hivi DSM itaendelea kupendelewa mpaka lini?

Msongamano wa DSM hauwezi kupungua iwapo miji mingine haipewi kipa umbele. Kwanini mradi mzima usipelekwe Tanga, Mwanza, Mbeya au Bukoba.

Cha kushangaza zaidi ni kuwa wanaopanga mipango hiyo, wanatoka mbali na DSM na hata siku moja hawafikiri kuwa sehemu walizotoka zinahitaji miji vilevile.

Wewe bepari kweli? Tangu lini katika mfumo uupendao serikali ikamuamulia mwekezaji mahali pa kuweka? Unaamini kweli huko uliko Bush anaweza kumuamrisha Toyota mahali pa kujenga kiwanda?
 
Wewe bepari kweli? Tangu lini katika mfumo uupendao serikali ikamuamulia mwekezaji mahali pa kuweka? Unaamini kweli huko uliko Bush anaweza kumuamrisha Toyota mahali pa kujenga kiwanda?

Katika ubepari miji inajengwa kwenye uzalishaji. Ukuaji wa DSM unatokana fikra potofu za Ujamaa ambavyo mapato yote ya nchi ni lazima yaendee DSM na baadaye kuanza kugawiwa. Hivyo ata mji usiozalisha unakuwa na access sawa ya mapato kama sehemu zenye uzalishaji.

Vile vile serikali ikiweka mazingira ya miji mingine kuwa mazuri wawekezaji watakwenda huko.
 
tatizo la kibamba ni UTAPELI both from baadhi ya wananchi wakishirikiana na maafisa ardhi kwenye zoezi hilo..............wananchi waliosaini utathmini feki kukiona na maafisa ardhi waliohusika kukiona pia.....i know Magufuli atakula nao sahani moja

Serikali si mara yake kwanza kufanya hili zoezi, na sehemu nyingi lilikofanyika zoezi lilienda vema bila matatizo
 
Katika ubepari miji inajengwa kwenye uzalishaji. Ukuaji wa DSM unatokana fikra potofu za Ujamaa ambavyo mapato yote ya nchi ni lazima yaendee DSM na baadaye kuanza kugawiwa. Hivyo ata mji usiozalisha unakuwa na access sawa ya mapato kama sehemu zenye uzalishaji.

Vile vile serikali ikiweka mazingira ya miji mingine kuwa mazuri wawekezaji watakwenda huko.

Katika ubepari wa kimarekani, miji inajengwa na mabepari (wawekezaji) kutokana na vivutio ambavyo wenye sehemu wanatoa. Angalia historia ya Las Vegas uone kama kuna mkono wa federal government pale! Kwa misingi hiyo, serikali haiwezi kuwaamulia mabepari wapi kwa kuwekeza bila kuweka vivutio. Huko uliko. states zinashindana kwa kuweka vivutio ili vivutie wawekezaji sio kutoka nje ya nchi tu bali hata kutoka state nyingine. Kama tunataka tuwe hivyo, inabidi mikoa yetu ianze kushindana yenyewe na kila mmoja ijitahidi kuweka vivutio bila kusubiri serikali kuu. Serikali kuu na yenyewe inabidi iachie baadhi ya mamlaka yake ili mikoa ipate uwezo zaidi wa kujiamulia yenyewe.Tatizo ni kuwa watu wataona tunaelekea kwenye majimbo. Tukirudi kwenye mada hii, inaelekea hapa mwekezaji(wenyewe wanamuita mfadhili) ameishapatikana na kinachogomba ni hiyo fidia. Hiyo ikitatuliwa jamaa anamwaga vitu na Dar inapata Manhattan yake! Wengi wetu watafurahia hilo wakiona hayo ndiyo maendeleo lakini ukweli ni kuwa kwa mara nyingine tena tutakuwa tumeweka rehani vizazi vijao kwa uroho wa makombo wanayotutupia hao tunaowaona ni wafadhili wetu!
 
Katika ubepari wa kimarekani, miji inajengwa na mabepari (wawekezaji) kutokana na vivutio ambavyo wenye sehemu wanatoa. Angalia historia ya Las Vegas uone kama kuna mkono wa federal government pale! Kwa misingi hiyo, serikali haiwezi kuwaamulia mabepari wapi kwa kuwekeza bila kuweka vivutio. Huko uliko. states zinashindana kwa kuweka vivutio ili vivutie wawekezaji sio kutoka nje ya nchi tu bali hata kutoka state nyingine. Kama tunataka tuwe hivyo, inabidi mikoa yetu ianze kushindana yenyewe na kila mmoja ijitahidi kuweka vivutio bila kusubiri serikali kuu. Serikali kuu na yenyewe inabidi iachie baadhi ya mamlaka yake ili mikoa ipate uwezo zaidi wa kujiamulia yenyewe.Tatizo ni kuwa watu wataona tunaelekea kwenye majimbo. Tukirudi kwenye mada hii, inaelekea hapa mwekezaji(wenyewe wanamuita mfadhili) ameishapatikana na kinachogomba ni hiyo fidia. Hiyo ikitatuliwa jamaa anamwaga vitu na Dar inapata Manhattan yake! Wengi wetu watafurahia hilo wakiona hayo ndiyo maendeleo lakini ukweli ni kuwa kwa mara nyingine tena tutakuwa tumeweka rehani vizazi vijao kwa uroho wa makombo wanayotutupia hao tunaowaona ni wafadhili wetu!

Federal Government kwa mabepari wa marekani inashughulika sana maendeleo ya miji. Kuna Highway zinazoitwa Interstate. Hizi Highway ziko chini ya Federal government. Kuna Airport Authority ambayo ipo chini ya Federal na yenye kushughulikia Airport.

Las Vegas ni Jangwani na kama kusingekuwepo na interstate au airport, ni bepari gani angeenda huko? Miji kama vile New York, Washington DC ikionyesha miradi ya Mass Transit yenye kuhudumia kiasi fulani inapata msaada kutoka Federal.

Ukweli wa mambo DSM inakula resource za nchi kuliko miji mingine.

Hakuna mji wowote uliondelea kwa kupewa misaada. Na kama hupo basi tungejifunza kutokana matokeo ya kitongoji cha Sinza.

Mji unaendelea kwa Circulation ya pesa inayoendelea katika mji huo na sio blah blah za kusubiri wadhamini.

Nimezaliwa DSM na connection zangu katika mji huu ni zaidi ya vizazi vitano lakini nimekulia Mwanza. Pamoja na connection zangu na jiji la DSM, ninaamini kabisa deal wanaopata watu wa mikoa ya Kanda ya Ziwa sio nzuri. Ukitembelea Musoma au Mwanza na ilivyokaribu ya Ziwa victoria, utajua kuwa toka tupate uhuru miji hii ilisahuliwa.

Hoja za ukabila zinatolewa na waliopo madarakani ili tuogope kuuliza. Itakuwaje kuwepo miji Tanzania ambayo toka mkoloni aondoke hakijafanyika kitu?
 
Las Vegas ni Jangwani na kama kusingekuwepo na interstate au airport, ni bepari gani angeenda huko? Miji kama vile New York, Washington DC ikionyesha miradi ya Mass Transit yenye kuhudumia kiasi fulani inapata msaada kutoka Federal.

Bepari aliyeenda huko wakati kalikuwa kajimji tu anaitwa Bugsy Siegel ambaye alikuwa mshiriki wa Lucky Luciano na Meyer Lansky. Huyu na wenzake ndiyo waliongoza maendelezi makubwa ya Las Vegas na kuufanya uwe mji ulivyo sasa. Kilichowavuta ni sheria ya kuruhusu kamari na sio airport na vinginevyo. Sasa mbona unajikanganya? Federal Government inasaidia tu pale ambapo miji imeishaanzisha miradi. Federal government haianzishi miradi ya biashara kama Mass transit ndiyo maana haina shirika la ndege, haina viwanda vya silaha, haina makampuni ya treni. Haya yote ni makampuni ya kibiashara ambamo Federal government inanunua huduma. Najua unaona sisi tulio bongo ni wakuja lakini si kwa kila kitu. Serikali ya Tanzania ilikuwa inawekeza kwa misingi ya kuleta maendeleo ( Diamond cutting Iringa wakati almasi iko Mwadui, Steel Mill Tanga, Musoma Textile, Tabora Spinning, n.k) na mara nyingi havikufanikiwa. Cha msingi ni kuweka vivutio kama infrastructure nzuri, sheria pendelevu, elimu bora na wawekezaji watakuja. Hawa tunaowaita wawekezaji wengi wao ni matapeli ambao interest yao ni kuvuna chap chap na kuondoka with minimal investment. Na sisi kwa bahati mbaya tumebaki kuwa rahisi mno kuwaamini.
 
Bepari aliyeenda huko wakati kalikuwa kajimji tu anaitwa Bugsy Siegel ambaye alikuwa mshiriki wa Lucky Luciano na Meyer Lansky. Huyu na wenzake ndiyo waliongoza maendelezi makubwa ya Las Vegas na kuufanya uwe mji ulivyo sasa. Kilichowavuta ni sheria ya kuruhusu kamari na sio airport na vinginevyo. Sasa mbona unajikanganya? Federal Government inasaidia tu pale ambapo miji imeishaanzisha miradi. Federal government haianzishi miradi ya biashara kama Mass transit ndiyo maana haina shirika la ndege, haina viwanda vya silaha, haina makampuni ya treni. Haya yote ni makampuni ya kibiashara ambamo Federal government inanunua huduma. Najua unaona sisi tulio bongo ni wakuja lakini si kwa kila kitu. Serikali ya Tanzania ilikuwa inawekeza kwa misingi ya kuleta maendeleo ( Diamond cutting Iringa wakati almasi iko Mwadui, Steel Mill Tanga, Musoma Textile, Tabora Spinning, n.k) na mara nyingi havikufanikiwa. Cha msingi ni kuweka vivutio kama infrastructure nzuri, sheria pendelevu, elimu bora na wawekezaji watakuja. Hawa tunaowaita wawekezaji wengi wao ni matapeli ambao interest yao ni kuvuna chap chap na kuondoka with minimal investment. Na sisi kwa bahati mbaya tumebaki kuwa rahisi mno kuwaamini.


Fundi Mchundo:

Kabla Las Vegas Strip kuanza (1941). Federal governemnt ilishajenga HighWay (Route 91). Na hii highway ilikuwepo toka 1926. Mtaa wa Las Vegas (Las Vegas Boulevard) ni eneo lililopo kwenye highway ambayo zamani ilikuwa inajulikana route 91. Hakuna bepari anayeanzisha biashara bila kujua wateja wake watapatikana vipi.

Kuna kitongoji kinaitwa Dumila katika barabara ya kwenda Dodoma kutokea Morogoro. Kabla ya kumalizika barabara ya kutoka hiyo wakazi wa pale walikuwa chini ya 100.

Kuwepo kwa barabara kumewafanya hata wale waliokuwa kwenye vijiji vya ujamaa kuacha vijiji vyao na kuhamia pale. Hivyo hata mwenye kuwekeza hoteli pale anajua wateja wake watapatikana wapi.
 
Biashara kuu ya Las Vegas ni kamari. Pamoja na kuwako bwawa la Hoover na hiyo barabara unayoizungumzia ni sheria ya kuruhusu kamari ndiyo iliyowavuta wakina Bugsy na wenzake. Las Vegas ukatangazwa kuwa ni mji usio na Familia na ndipo biashara ya kamari ikapanuka. accessibilty na sheria vyote vilichangia kuvuta mabepari. Nilivyokuelewa mwanzoni (niwie radhi kama nimekukosea)ni kuwa serikali ipeleke wawekezaji kule ambako hakuna maendeleo. Kama hiyo ya Dumila. Serikali walijenga barabara na wawekezaji wakaanzisha soko la mahindi na kadhalika, mji ukajikita. Hapa Kimara kuna infrastucture tayari (kwa hali ya kiTanzania) na inaelekea tayari ameshapatikana muwekezaji atakayejenga hiyo satellite city. serikali haiwezi kumwambia kuwa ati badala ya kujenga hapo aende mathalani Kwimba, Kibondo au hata hapo Dumila. Njia pekee ya kumpeleka huko ni kumwekea mazingira mazuri ambamo ataweza kufanya biashara. Mimi tatizo langu ni aina ya uendelezaji atakaofanya huyu bwana/bibi hapo Kimara. Tuna kawaida ya kumwogopa yule tunayemwita mwekezaji kiasi cha kumpa blank cheque afanye chochote atakacho. Maendelezi kama haya yanatakiwa yajadiliwa kwa uwazi na jamii nzima kabla ya utekelezaji kuanza.

Nitakupa mfano wa New York. Sehemu kubwa iliyobaki inayoweza kuendelezwa Manhattan ni eneo la railyards lijulikanalo kama Hudson Yards. Mipango ya awali ilikuwa ni kujenga stadium kwa ajili ya timu ya the Jets ambayo ingegharimu zaidi ya $1.2 billion. Wakaazi waliipinga kutokana na sababu za kimazingira( ongezeko la magari wakati wa mechi, kelele, historia ya pale mahali n.k). Mpango huu umekufa. Sasa mpango ni kujenga business centre nyingine ( kama hii sisi tunayoiita satellite City) juu ya hizo railyards. Watu wa mipango miji wa jiji la New York wameishatayarisha ramani zao za awali ya nini wanachotarajia pale KABLA ya kupapiga mnada kwa waendelezaji. Wao wanataka maofisi,sehemu za burudani, sehemu za wazi, sehemu za tamaduni na makazi. Wananchi wanaoishi jirani wanataka wahakikishiwe kuwa patukuwa na makazi kwa ajili ya wale wasio na uwezo. Sasa kwa vile patakuwa na public review za mradi mzima ni lazima muwekezaji ahakikishe kuwa patakuwa na haya makazi ama sivyo mradi utakufa. Makisio ni kuwa mradi utachukua si chini ya miaka 10 kutekeleza. Sasa sisi ( nasikitika kuwa na wengi humu JF mmo) tunagombea hicho tunachoita fidia bila kuuliza ni kitu gani kinachokusudiwa kujengwa. Je wakija jenga sehemu ambayo wakina yakhe hawana nafasi(Tumeona haya kwenye mahoteli ya ufukweni ambapo wavuvi wenyeji hawaruhusiwi kuendelea na shughuli zao ati kwa sababu watawabughudhi watalii)tutamlaumu nani? Si tumeshachukua vipande vyetu vya fedha? Kabla ya hata kuzungumzia hiyo fidia ilibidi mamlaka husika ituelezee hiyo satellite city hasa inahusu nini? Kutakuwa na nini pale? na sisi kama jamii tutafaidika vipi? Maelezo haya yasiwe kwa maneno tuu bali maandishi na michoro. Baada ya hapo ndiyo tugombee hayo makombo.
 
Biashara kuu ya Las Vegas ni kamari. Pamoja na kuwako bwawa la Hoover na hiyo barabara unayoizungumzia ni sheria ya kuruhusu kamari ndiyo iliyowavuta wakina Bugsy na wenzake. Las Vegas ukatangazwa kuwa ni mji usio na Familia na ndipo biashara ya kamari ikapanuka. accessibilty na sheria vyote vilichangia kuvuta mabepari. Nilivyokuelewa mwanzoni (niwie radhi kama nimekukosea)ni kuwa serikali ipeleke wawekezaji kule ambako hakuna maendeleo. Kama hiyo ya Dumila. Serikali walijenga barabara na wawekezaji wakaanzisha soko la mahindi na kadhalika, mji ukajikita. Hapa Kimara kuna infrastucture tayari (kwa hali ya kiTanzania) na inaelekea tayari ameshapatikana muwekezaji atakayejenga hiyo satellite city. serikali haiwezi kumwambia kuwa ati badala ya kujenga hapo aende mathalani Kwimba, Kibondo au hata hapo Dumila. Njia pekee ya kumpeleka huko ni kumwekea mazingira mazuri ambamo ataweza kufanya biashara. Mimi tatizo langu ni aina ya uendelezaji atakaofanya huyu bwana/bibi hapo Kimara. Tuna kawaida ya kumwogopa yule tunayemwita mwekezaji kiasi cha kumpa blank cheque afanye chochote atakacho. Maendelezi kama haya yanatakiwa yajadiliwa kwa uwazi na jamii nzima kabla ya utekelezaji kuanza.

Nitakupa mfano wa New York. Sehemu kubwa iliyobaki inayoweza kuendelezwa Manhattan ni eneo la railyards lijulikanalo kama Hudson Yards. Mipango ya awali ilikuwa ni kujenga stadium kwa ajili ya timu ya the Jets ambayo ingegharimu zaidi ya $1.2 billion. Wakaazi waliipinga kutokana na sababu za kimazingira( ongezeko la magari wakati wa mechi, kelele, historia ya pale mahali n.k). Mpango huu umekufa. Sasa mpango ni kujenga business centre nyingine ( kama hii sisi tunayoiita satellite City) juu ya hizo railyards. Watu wa mipango miji wa jiji la New York wameishatayarisha ramani zao za awali ya nini wanachotarajia pale KABLA ya kupapiga mnada kwa waendelezaji. Wao wanataka maofisi,sehemu za burudani, sehemu za wazi, sehemu za tamaduni na makazi. Wananchi wanaoishi jirani wanataka wahakikishiwe kuwa patukuwa na makazi kwa ajili ya wale wasio na uwezo. Sasa kwa vile patakuwa na public review za mradi mzima ni lazima muwekezaji ahakikishe kuwa patakuwa na haya makazi ama sivyo mradi utakufa. Makisio ni kuwa mradi utachukua si chini ya miaka 10 kutekeleza. Sasa sisi ( nasikitika kuwa na wengi humu JF mmo) tunagombea hicho tunachoita fidia bila kuuliza ni kitu gani kinachokusudiwa kujengwa. Je wakija jenga sehemu ambayo wakina yakhe hawana nafasi(Tumeona haya kwenye mahoteli ya ufukweni ambapo wavuvi wenyeji hawaruhusiwi kuendelea na shughuli zao ati kwa sababu watawabughudhi watalii)tutamlaumu nani? Si tumeshachukua vipande vyetu vya fedha? Kabla ya hata kuzungumzia hiyo fidia ilibidi mamlaka husika ituelezee hiyo satellite city hasa inahusu nini? Kutakuwa na nini pale? na sisi kama jamii tutafaidika vipi? Maelezo haya yasiwe kwa maneno tuu bali maandishi na michoro. Baada ya hapo ndiyo tugombee hayo makombo.

We are on the same page. Kuna siku nilikuwa nasoma historia ya San Francisco. Mji huu ulikuwa ni kijiji kidogo sana lakini ulibadilika pale fortune hunters walipogundua dhahabu. Mji ukaendelea na kufikia hatua tunayoijua sasa.

Historia ya mjini huu inanikumbusha kijiji cha Mererani. Fortune hunters wa kitanzania bila msaada wa serikali ambayo ilikaa bure tu, waliweza kugundua upatikanaji wa Tanzanite. Uchimbaji wa Tanzanite uliwasaidia wao na familia zao na vilevile kukifanya kijiji cha Mererani kuanza kuwa mji.

Tofauti kubwa kati ya Mererani na San Francisco ni kuwa serikali ya Marekani haikuingilia kati speculation ya watu kutafuta na kuchimba dhahabu. Wachimbaji na wafanyabiashara wengine waliweza kutumia capital itokanayo na dhahabu kufungua biashara nyingine na kuujenga mji.

Serikali ya Tanzania ilichofanya ni kutaifisha machimbo na kuwapa wawekezaji wa kigeni. Na serikali haikutumia juhudi zozote kutafuta hazina ya Tanzanite huko Mererani. Lakini kwa sababu kuna watu walioona kuwa wakimpa mwekezaji wa kigeni watapata 10%, juhudi zote za wazawa za kutafuta mali zimeishia ukingoni.

Tukirudi kwenye mada kwanini watu walipwa fidia na kuondoka? Kama wananchi wanamiliki ardhi kwanini basi wawekezaji wasikodi hiyo ardhi na kujenga wanachotaka kujenga na baadaye wawalipe wenye ardhi kodi ya kutumia vipande vya ardhi. Na yakifanyika hayo basi mtanzania kwa namna fulani atafaidika katika uwekezaji huo.

Suala la kulipa fidia linamfanya mwekezaji amiliki ardhi na akishindwa kwenye miradi yake bado atakuwa anamiliki kipande cha ardhi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom