Hii ya Kaburu Imeekaaje?

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,141
13,215
Huyu ni Kiongozi wa TFF........................tutafakari kidogo
kaburu.JPG
 
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Geoffrey Nyange 'Kaburu' katikati akiwa na fulana iliyoandikwa ujumbe wa kumbeza mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Emmanuel Okwi aliyehamia Yanga. Kaburu ambaye ni Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Simba SC, amebeba ujumbe unaosema wakati wote anamkumbuka marehemu Patrick Mafisango, Okwi kitu gani. Wengine kulia ni Kocha wa Simba, Mcroatia Zdravko Logarusic na kulia na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe
 
Hayo ni mambo ya utani tu, ndo maana Okwi alipoonana naye ilibidi aishie kucheka tu.

kaburu&okwi.JPG
 
hoja yangu ikiwa kiongozi wa TFF anaweza kuingiza ushabiki kupindukia kiasi hiki si ya utani

Mkuu si afadhali yeye kaingiza ushabiki katika mavazi tu halafu uwanjani tena kwenye match ya nani mtani jembe kuliko Angetile na Mgongolwa waliokuwa wanaingiza ushabiki kwenye maamuzi yanayofaidisha klabu, lakini hii ya Kaburu haifaidishi chochote zaidi ya utani tu.
 
huo ndio ukweli Mafisango was genuinine compared to Okwi . Pumzika kwa amani Mafisango.
 
sawa nimekusoma mkuu
Mkuu si afadhali yeye kaingiza ushabiki katika mavazi tu halafu uwanjani tena kwenye match ya nani mtani jembe kuliko Angetile na Mgongolwa waliokuwa wanaingiza ushabiki kwenye maamuzi yanayofaidisha klabu, lakini hii ya Kaburu haifaidishi chochote zaidi ya utani tu.
 
hoja yangu ikiwa kiongozi wa TFF anaweza kuingiza ushabiki kupindukia kiasi hiki si ya utani

Hata mm inanipa shida kidogo. Najaribu kujiuliza kwa mfano Kaburu angekuwa ndio kiongozi mkuu wa TFF sijui ingeleta picha gani kwa jamii
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom