Hii ya Chadema ni "Copy and Paste ya CUF??"

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Jana nilipokuwa nikiangalia taarifa ya habari Startv, viongozi wa Chadema Mwenyekiti Freeman Mbowe na katibu wake Dr. Slaa walidai kutoyatambua matokeo ya uraisi yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi. Matokeo hayo ndio yaliyompa ushindi Jakaya Kikwete wa CCM na hivyo kumfanya kuendelea kuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. CHADEMA wameenda mbali zaidi na kudai kutomtambua raisi Kikwete. Nataka kujua tu kama hili la chadema ndio wanaiga waliyofanya CUF zanzibar walipokataa matokeo ya urais na kutomtambua Karume? CUF wao waligomea hata vikao vya baraza la wawakilishi, Je CHADEMA nao watagomea vikao vya bunge wakati wabunge wao wameshakula kiapo??? Hebu tujadili hii hali..
 
Back
Top Bottom