Hii teknolojia ya “ceremic liquid” ya screen protector kwenye simu kitalaamu ni salama kweli?

Bakulutu

JF-Expert Member
Nov 30, 2011
2,541
1,756
Habari za hapa,
Jana nilikuwa Mororogo Mjini nikapita mahali nikaona kijana moja akielezea teknolojia mpya ya kulinda kioo cha simu ya Ceremic Liquid na nyingine ya protector fulan hivi ngumu.

Hii teknolojia ya ceremic anatumia vimiminika fulani hivi vya aina kama 4 alafu anaweka simu kwenye ki mashine kama picha inavyo onyesha na baada ya dakika 10 inakuwa tayari hapo anajaribu ikitoboa na hiyo drili mashina na simu haitoboki wala kuchubuka pia hata misumari na vitu vyenye ncha havichubui.

Ya pili baada ya Ceremic anaweka hiyo Protector ngumu (extreme lamination)na kioo kinakuwa strong kiasi kwamba anapigilia msumari kwenye hicho kibao na simu kabisa kwa upande wa kioo.

Sasa niliangalia nikiwa na maswali hii ni salama kwa simu kweli ? Baadae haitaleta madhara kama kuondoa sensitivity ya kioo ? Na nilimuuliza inaweza toka akasema hapana labda utoe kioo chote!

Naamini hapa kuna wataalamu walisha iona hata kuijua vyema wanaweza elezea zaidi CHIEF MKWAWA pia natumai ulisha sikia hii
IMG_2100.JPG

IMG_2101.JPG
 
Sasa kama ikapasuka inapasuka na kioo si bora nibaki na kioo tu pekee

Napenda zile protector za kawaida zenyewe huwa hazijakaza sana hata simu ikipata shock yenyewe ina act as shock absorber ina crack haraka kioo kinabaki safe

In short protect huwa ni kwa ajili ya kukinga scratches kwenye kioo na sio kuzuia kioo kupasuka!

Kinachokilinda zaidi kioo kisipasuke ni zile kava za juu hata simu ikidondoka toka height flani!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama ikapasuka inapasuka na kioo si bora nibaki na kioo tu pekee

Napenda zile protector za kawaida zenyewe huwa hazijakaza sana hata simu ikipata shock yenyewe ina act as shock absorber ina crack haraka kioo kinabaki safe

In short protect huwa ni kwa ajili ya kukinga scratches kwenye kioo na sio kuzuia kioo kupasuka!

Kinachokilinda zaidi kioo kisipasuke ni zile kava za juu hata simu ikidondoka toka height flani!.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna mteja nilimuwekea kioo complete nikamshauri aweke kava pamoja na protector ya kawaida akasema ngoja kwanza aitumie aone. Baada ya siku tatu akiwa hana hili wala lilez simu ikaanguka kwenye kigae, glass touch yote haitamaniki maana ilianguka toka umbali kama mita moja au zaidi (ni mzee wa mneso) alikuja akaniambia, fundi zawadi yako hiyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom