Hii tabia ya wamiliki wa mabasi yanayosafiri safari ndefu

ndege joni

JF-Expert Member
May 23, 2017
673
1,082
Je kwa nini wanapenda kupeleka abiria kwenye hoteli za gharama kubwa sana na ambazo zipo porini kusipopatikana vyakula vya bei nafuu?


Juzi nilisafiri kutoka Morogoro kwenda shinyanga kwa usafiri wa basi ya Abood... baada ya kufika wilaya ya Bahi Dodoma, walishusha abiria kwa ajili ya chakula cha mchana mda wa saa tano na robo ivi.
Kutokana na safari yangu ilikuwa ya dharura na sikuwa na pesa nilipanga njiani nitumie pesa isiyozidi 3000/=
Tuliposhuka pale nilienda kuulizia wali nikaambiwa sahani ni 5000/=
Nikaona niachane nao nikaenda kununua andazi mbili nikatoa 2000 nikijua haizidi buku kwa zote mbili. Nikashangaa naambiwa andazi moja ni 1000 af bayaaa.

Hii tabia sio ya abood pekee ni mabasi karibia yote ya masafa marefu.

Je ni sahihi? Mana niliangalia abiria wengi hawakula na kati ya basi zima hawafiki 10 waliokula pale. Na abiria wanaopanda mabasi haya wengi ni wa kipato cha kawaida. Kwa upande wangu huu ni unyanyasaji wa abiria na wizi wa lazima
 
Anza kisafiri na miwa kwenye begi.

Huko kwenye bei kubwa angalau huwa kuna hali ya unadhifu wa kuridhisha kila abiria. Basi inabeba abiria wengi, hauwezi kusimamisha hotel ya hovyo hovyo kisa bei yao ni rahisi, kuna watu wayashindwa kula.

Lakini pia mkuu, kula kula safarini mbona sio lazima!! Labda kama una tatizo la kiafya la kukufanya usikae njaa muda mrefu, la sivyo mtakuja kulishwa vyakula vya ajabu mdhurike.
 
Hawa watu hufikiri wasafiri ni manyama fulani kutoka sayari ya pluto, hayajui bei ya vyakula na ni majinga yakiuziwa chakula chochoye kwa bei yoyote wananunua
Inapaswa tuongee hili life, hata kwa kutumia vyombo vya dola
 
Dawa yao basi zima mnabeba vyakula kama ndizi,mihogo,viazi nyama ya kuchoma kwenya take away juice,soda take away,

mkifika pale nyie hamshuki
Maisha ya sasa ni kuliana timing tu
Hahaaaa hii nilifanya siku moja nikabeba chips kuku kutoka moro kwa bei ya 2500. Waliposhusha kula mie nikavuta msosi wangu wa nguvu
 
Anza kisafiri na miwa kwenye begi.

Huko kwenye bei kubwa angalau huwa kuna hali ya unadhifu wa kuridhisha kila abiria. Basi inabeba abiria wengi, hauwezi kusimamisha hotel ya hovyo hovyo kisa bei yao ni rahisi, kuna watu wayashindwa kula.

Lakini pia mkuu, kula kula safarini mbona sio lazima!! Labda kama una tatizo la kiafya la kukufanya usikae njaa muda mrefu, la sivyo mtakuja kulishwa vyakula vya ajabu mdhurike.
Wabalance tu, au wawe wanatuacha ata mjini ili watakaokula vya gharama wanunue na wa bei chee pia
 
Back
Top Bottom