Hii tabia ya Simba kulaghai kwa wachezaji wameanza lini?

Jamaa ana matatizo sana huyu.
Hawa ni baadhi waliocheza ulaya.
1. Bobani
2.Okwi
3.Samatta
4.Kapombe. Hao ni baadhi ninao wakumbuka.kuna yule Mnaigeria aliyecheza simba kisha kapaa ulaya. Simba haijatoa nje tena wachezaji kwasababu ya kutocheza mechi za kimataifa.Naiona kesho ya hawa ulaya.
1.zimbwe Jr
2. Mkude
3.Ndemla kama watajituma kwenye mechi za kimataifa.




Ukinitajia hao nitakutajia

1. NONDA
2. Nizar
3. Kpah Sherman

Huyo Kapombe hajawahi kuichezea Caen hata game 1 ya ushindani. Alikuwa trial muda wote.

1. Huyo Zimbwe Jr ata kuitwa kwa ajili ya trial imeahindikana ....anangoja azeeke kama Mgosi wampeleke AS VITA ya Congo.

2. Mkude ndio wale wale ....umeenda trial sauz na kurudi Bongo.

3. Hahaha eti Ndemla..sikumbuki ni lini kaenda hata trial....nafasi yenyewe hana kikosi cha kwanza, tena anaingizwa pale MTU wa kupiga mashuti nje ya 18 yard anapotakiwa.
Kakwambia nani wazungu wanahitaji mashuti nje ya 18 yard..
 
Wanafanya vizuri Yanga yaan timu kila mwaka ni bingwa inalipa vizuri inashiriki mashindano makubwa sasa uende ulaya kuuza mchicha kama boban na okwi au????-

Hata YouTube clip zao hamna sasa sijui kama wanacheza mpira au ni mabaa medi huko wakati ukiwa Yanga FIFA INAKUTAMBUA. bora kuuza mchicha ulaya au kucheza timu bora ya Africa???
Acha upimbi kijana. Jifunze kuficha ujinga wako japo kidogo basi. Huyo mwenzio kaongelea nini? Au unakurupuka tu. Jibu swali langu sitaki mbwembwe.
 
photo%281%29.JPG


Twite++na+jezi+ya+Rage.JPG
 
Naomba unijie mchezaji wa kizazi hiki anayefanya vizuri ulaya akitokea Yanga.
Mammiee!

Hii ishu iko general.... Kwanini ufanye sampling ya time kwenye jambo general kama hili.?

Tunazungumzia wakati wote!

Sijui umenielewa hapo...
 
Mada yako inaongelea wachezaji wa ndani. Okwi lini Kawa mtanzania?
Acha kutapatapa simama kwenye Mada yako. Hiyo ni dalili ya kushindwa. Poleee
Usikurupuke soma vizuri....

Ni shabiki mwenzako wa Matopeni FC aliyependekeza jina la Okwi.....
 
Pamoja na utani mwingi baina ya wanazi wa timu hizi lakini kuna baadhi ya facts hazihitaji kubishaniwa.

Simba imetoa wachezaji wafuatao kwenda Ulaya;

1. Haruna Moshi Boban - Ligi Kuu Sweden
2. Henry Joseph - Ligi Kuu Norway
3. Mbwana Samattha - TP Mazembe kisha Genk Ubelgiji
4. Emeh Ezechukwu - Denmark
5. Emmanuel Okwi - Ligi Kuu Denmark
6 Dan Mrwanda - Kuwait kisha Vietnam
7 Shomari Kapombe - AS Cannes - Ufaransa.

Simba imetoa wachezaji wengi kwenda kwenye majaribio kktk nchi zilizoendelea kisoka kama Misri na Afrika Kusini

Wakati Simba ikifanya hivyo, Yanga imetoa wachezaji wawili tu kwenda kwenye majaribio ambao ni Mrisho Ngassa na Nadir Haroub. Huyu Nizar alitokea Moro United kwenda Marekani na baada ya kurudi akafikia Jangwani na sasa yuko Singida Unted.

Badala ya kuleta mabiashano yasiyo na maana, Yanga wakubali wana kitu cha kujifunza Msimbazi, waachane na mfumo mbaya wa kuwabania wachezaji kama walivyofanya kwa Jerry Tegete na wanavyoelekea kufanya kwa Msuva ambao katika viwango vya wanapaswa kupata timu nzuri tu Africa na hata nje ya Africa. Hata huyo Nonda ambaye tunaweza kusema ndio mchezaji mwenye mafanikio zaidi duniani kuwahi kupita ktk timu za Tanzania, aliondoka kwa kutoroka kwenda South Africa, ambaoko kutokea huko ndio akaenda Ufaransa.
 
Mada yako imesimamia wapi? Tuanzie hapo?
Mada inazungumzia kwanini simba SC wanajiona kuwa wao ndio daraja pekee hapa Tanzania la wachezaji kwenda kucheza soka la masrahi nje ya nji?

Na kwanini kuna mtazamo kuwa ukicheza Yanga hakuna hata possibility ya kupata nafasi ya kucheza soka la kulipwa?

Nikauliza naombeni mnitajie idadi hiyo kubwa ya wachezaji wanaozidi idadi ya ile ya Yanga walioenda kucheza soka la maslahi nje...
 
Si unaona sasa Kumbe hata hili la ngasa kucheka Vs Man Utd unabisha?duh mikia akili zenu fupi sana,ndio mana mwenyekiti wenu kawaita mbumbumbu,nyie hamnazo kweli,hizi hasira zenu mngezielekeza kwenye ligi walau mngefanya kitu.
Kama amekuelewa vyema ,basi atakuwa na tatizo la mtindio wa Ubongo.....

Hajui kuwa NGASSA alishawahi cheza vs United.
 
Vizuri sana! Wewe ndio nakuhitaji simba imetoa wachezaji wangapi kwenda nje ya Nchi.?
Wewe nawe kichwa cha mbuzi, soma alichoandika uelewe, alafu uliza swali, usiulize wakati umesoma kwa jazba. Simba haikatalii wachezaji wenye nia, ya kwenda kucheza Clab kubwa nje ya nchi, hiyo ni sera ya Clab, yanga, hilo swala hakuna leo hii Msuva anahitaji kutoka, ila anakumbana na vikwazo sana. Wakati vilabu vya Tanzania kwa sasa tunacheza kujifurhisha tu, simba iitambie yanga yanga iitambie Simba, timu inaweza shiriki miaka minne, mashindano ya kimataifa inaishia raundi ya pili tu, hamna marekebisho wala nini, tukirudi tunajiita wakimataifa, wa kimataifa kwa kutia aibu Taifa. Kama lengo ni kujifurahisha na kushindana kimataifa kwanini tusiachie wachezaji kujaribu bahati zao kwingine nje nchi, wakishindwa washindwe wao.
 
Wewe nawe kichwa cha mbuzi, soma alichoandika uelewe, alafu uliza swali, usiulize wakati umesoma kwa jazba. Simba haikatalii wachezaji wenye nia, ya kwenda kucheza Clab kubwa nje ya nchi, hiyo ni sera ya Clab, yanga, hilo swala hakuna leo hii Msuva anahitaji kutoka, .

Naona umekurupuka na wewe....

Kuna ushahidi gani unaoweza kuondoa shaka kuwa Msuva amezuiliwa na Klabu kwenda nchi za nje hata kama anahitajika...?

Unauwezo wa kutoa huo ushahidi, au hadithi za Facebook ndio unazileta humu JF...
 
Jamaa ana matatizo sana huyu.
Hawa ni baadhi waliocheza ulaya.
1. Bobani
2.Okwi
3.Samatta
4.Kapombe. Hao ni baadhi ninao wakumbuka.kuna yule Mnaigeria aliyecheza simba kisha kapaa ulaya. Simba haijatoa nje tena wachezaji kwasababu ya kutocheza mechi za kimataifa.Naiona kesho ya hawa ulaya.
1.zimbwe Jr
2. Mkude
3.Ndemla kama watajituma kwenye mechi za kimataifa.
Umemsahau henry Joseph (shindika)
 
, mashindano ya kimataifa inaishia raundi ya pili tu, hamna marekebisho wala nini, tukirudi tunajiita wakimataifa, wa kimataifa kwa kutia aibu Taifa. Kama lengo ni kujifurahisha na kushindana kimataifa .

Ukiwa unajadili JF hakikisha akili zako hujaazimisha....

Unaelewa kwanini Yanga wanajiita wakimataifa?.....

Hebu ng'amua tafasiri ya neno wakimataifa , kama ukishindwa nitag nije kukutafasiria.

45bc8311b39e64ad128e6aea1be39f82.jpg


Usipende kukurupuka ...
 
Okwi, boban. Kapombe. Samatta. Kwa siku za karibuni uyo Nonda wengi hatumjui kwa kweli Yanga haina rekodi ya kumuuza mchezaji zaidi ya kuwadanganya kama walivyo fanya kwa Ngasa simba ilikua unamuuza Sudani
 
Ukiwa unajadili JF hakikisha akili zako hujaazimisha....

Unaelewa kwanini Yanga wanajiita wakimataifa?.....

Hebu ng'amua tafasiri ya neno wakimataifa , kama ukishindwa nitag nije kukutafasiria.

45bc8311b39e64ad128e6aea1be39f82.jpg


Usipende kukurupuka ...
Huna hoja zaidi ya kashfa
 
Back
Top Bottom