JEKI
JF-Expert Member
- Aug 16, 2013
- 4,846
- 2,936
Jana katika pita pita yangu mjini nikabahatika kukutana na binti mmoja, tukabadilishana namba za simu, time za jioni nikaamua kumrukia hewani tukutane town tufahamiane zaidi, akaibuka na rafiki zake wawili, ikawa timu ya watu watatu, tumekaa kunywa mabinti wale wakaanza kuagiza vinywaji vya bei kubwa kubwa, mwenyewe nikaagiza maji tu, wanywaji mnajua kuna kakinywaji nikawa nasikia nipimie nzima, hapo Tsh 12,000 cash, mwingine nipatie henken. Kana kwamba hiyo haitoshi ulipofika wakati wa msosi, mwanamke anaagiza mnavu kuku mzima peke yake, huku kichwa kinaniuma nawaza kumbe wanawake wa mujini ndo wana matumbo makubwa hivi, kumbe ndiyo maana wanawake wengi sasa hivi wana vitambi. Pigo la mwisho ni wakati wa kuondoka, wanaagiza vinywaji na chakula cha take away, kidogo niumbuke ila uzuri bar ile wanapokea hela kwa tigo pesa, nimeondoka pale sina hamu, nimeinamisha kichwa na wala sina hamu tena na mwanamke yule. Hii tabia unapopewa offer ndo unaagiza kinywaji cha bei mbaya, mtu kila siku anakunywa fanta, siku hiyo anataka redbull, vipi wakuu wangu?