Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Una familia au upo singo? Unasomesha? Ugumu ni pale ambapo ada zinakutana na kodi ya kupanga, hapo ndo huwa akili inakukaa sawa. Hiyo kujenga kwa kujinyima huwa inakuja tu automatic na sio kwa kupenda hasa pale unapoona maji yameshazidi unga
Lakini pia inategemeana na kipato chako, kuna wengine wanaweza kujenga mwanzo mwisho bila kujinyima huku wamepanga na mambo mengine yanaendelea kama kawaida
Eeh chukulia mtu ana Mshahara wa 12M kila mwezi huyu anajengaje kwa uchungu sasa? Maana hata akisema avute 100M ya Chap hapo NMB ana uhakika wa kuipewa fasta sababu sio rahisi ku default.

Hata ukiwaambia wakate 6 kila mwezi ndani ya 3 yrs deni limeisha na life linaendelea kama kawaida. Hawa ndio wale wa kuporomosha kitu mwanzo mwisho. Anakamata ground ya 20M fasta akianza hapoi mpaka anahamia ndani ya miezi 6 tu.
 
Huwezi kupata kwanja cha million 6 bila kuwa 30KM+ toka city center.

Kigamboni yenyewe utaambiwa kiwanja kiko 25KM toka darajani. Ukienda upande wa Morogoro Road unazungumzia mbele ya Kibaha ambako ni 30KM+

Ukija Bagaomoyo road Labda bunju ambako nako ni ishu kupata kiwanja sasa. Unazungumzia 25KM+! Goba nako ni ghali sana na hamna tena kiwanja ukibahatisha ni 10M plus na hicho ni high density.

Inshort tumefikia ule wakati ambao kupanga karibu na kazini ni less costful kuliko kuweka mafuta ya gari daily na kulipa kodi.
True man...iko waz
 
Duh bado ana akili za ujana sana
Anyway with time ata badilika japo inaweza kuwa kwa kuchelewa
Dogo anaenifata nae ana mambo kama hayo ya quality life mpaka maza kaingilia kati mshahara ukitoka kuna percent anampa kwa lazima ameanza kujenga,yani ni kwa mbinde mpaka wamefika hapo
Huyo jamaa anahitaji guidance labda pengine ni wa kishua kila kitu kipo
Ahahhaha....sema namuan sna.Gym ni collosium hotel na akina Mo.😎.. jogging asbh company zake akina salama jabir ..😁..apartment yake ya kwanza ku rent majiran zake ni akina wolper 😂 hapo nisikutajie mambo mengine.. kifup namkubali 😆 ..anasema atajenga hata akifa
 
Ahahhaha....sema namuan sna.Gym ni collosium hotel na akina Mo.😎.. jogging asbh company zake akina salama jabir ..😁..apartment yake ya kwanza ku rent majiran zake ni akina wolper 😂 hapo nisikutajie mambo mengine.. kifup namkubali 😆 ..anasema atajenga hata akifa
Atakuja kukumbuka shuka pamekucha, unless awe na mshahara wa level za UN!

Ila kama ni lile kundi la 2.2M kwa mwezi namtakia kila la heri, tukutane 45 yrs hapo akiwa na watoto wawili na mke mpenda starehe!
 
Hawa ndio wanaobwiaga unga, ghafla mkataba umeisha. No more coloseum, no more butters, wana wote wamekata bogi 😂 utajua hujui.
Hapo kazungukwa na marafiki wa uongo, wanamnywea na kumlia hela, wanam-mwambafayi, anajiona Don, ngoja mambo yabadilike, 😂 😂 atatamani hata ajiunge na kanisa la Don Nalimison, awe muimba kwaya tu.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Sehemu zote hata Mbweni palikuwaga mashambani miaka ile ya 2003-2004 ila leo, 2020 ni kama Beverly Hills ya Bongo 😂😂😂 maamuzi ambayo mtu angeweza kuyafanya 2008 tu yangekuwa na manufaa sana leo.
Sahihi sana ujana unakataa mambo mengi ambayo ni manufaa uzeeni
 
Viwanja si vipo Chanika pia 😂 au Vikindu tena vya bei rahisi sana. Million 5 unapata uwanja wa kujigaragaza 😁 ila ndio mbali balaa 25KM+
25km kutoka wapi?
Kuna watu wana biashara/shughuli ambazo zinahamishika kirahisi na wanaweza kufanyia popote na faida ikawepo ila anakomaa kukaa mjini garama kubwa kodi kubwa na anaona kukaa chanika ni mbali wakati umuhimu wa kukaa kati ya mji haupo.
So unavyosema ni mbali itategemea na mishe zako au kazi zako.
Kuna watu wanakaa tabata ila posta sijui k.koo na samaki samaki.Next door mara 1 kwa miezi 4
 
Asilimia kubwa ya wanaokomenti hapa inaonekena wapo chini ya 35yrs, ndiyo maana issue ya kununua kiwanja nje ya mji mnaona ni polini.

Mwaka 2016 kuanzia boko kwenda bunju nje ya barabara ilikuwa mithili ya poli, watu wengi walikataa viwanja maeneo hayo na baadhi walijenga na kuziacha nyumba mikononi mwa walinzi, kipindi hicho viwanja/mashamba yalikuwa bei rahisi sana.

Leo mnajua kinachoendelea na wale mnaokomenti kuwa hamuwezi kujenga nje ya mji, huko ni kukosa maono au akili bado hazijafunguka.

Kwani hapo unapopaita mjini kabla ya kuwa hivyo unadhani nani alianzisha makazi na leo unapafagilia?.
Baba mdogo wangu alihamia dar miaka ya katikati ya 90! Life akaanzia Sinza, maisha yakawa Safi Sana, akataka kujenga akaenda kuoneshwa kiwanja Mbagala eneo la Zakhem pale! Akapaona bush Sana, anatokaje Sinza akajenge kijijini Mbagala! Miaka ya kuanzia 2010 akashtuka amezeeka life linaanza kuyumba, hawezi kupanga katikati ya mji, akaenda kupanga Mbagala Nzasa huko Mbagala ndani ndani! Ndio akili ikamjia inabidi ajitahidi ajenge, maeneo ya kujenga hakuna inabidi aende mbali zaidi!

Kahangaika Sana hatimaye akapata kakiwanja kadoooooogo hapo hapo Mbagala ndio kajenga yaani kadogo balaa, akikumbuka likiwanja aliloonyeshwaga pale Zakhem na akikumbuka ile bei moyo unamuuma anasema kilikuwa pembeni ya barabara tu, angeweka hata frame maisha yangeenda kuliko alipojenga saa hizi! Anasema kwa miaka ile hata huko Tabata huko sijui Chang'ombe, kisukulu kulikuwa bado na mashamba ya mihogo yaani angeweza kununua kiwanja kikubwa tu ila akaona mjini ni Sinza! Imekula kwake!

Bado nakua, bado najifunza!
 
Acha uongo banda hani la mil 20 kuku wa milioni 2. Kuna watu mnakuaga wachawi sana kwenye kushauri mtu . Sijui mnatokaga famikia za kishua sana au ndo kuhikweza tu.
Bila shaka umeanza kusikia kabla ya kusoma, sasa nakushauri anza kusoma mwenyewe kisha usimuliwe.

Wapi nimesema banda la milioni 20?
Unazijua gharama za kuwahudumia kuku wa biashara wewe!
Achana na hawa kuku vitoga, nazungumzia kuku wa biashara unawajua wewe.

Hilo banda hata ukisema la elfu50 ndio ufugie kuku wa kukupa faida?

Acha mihemko utapata tatizo la upumuaji, soma vizuri kisha km huna cha kuandika kukaa kimya nayo ni uungwana.

Andika vizuri kitu unachokusudia kuandika .
Sio HANI bali GANI
Sio FAMIKIA bali FAMILIA
Sio KUHIKWEZA bali KUJIKWEZA.

Uchawi wenu umepitia kwenye ushauri bila shaka.
Uwe na siku njema
 
Ndugu mleta uzi. Upo sahihi but napenda uniruhusu kuwasilisha maoni yangu kama ifuatavyo.
Mtazamo wa maisha ni jambo very tricky sana usipokuwa makini na maamuzi yako unapoamua kufanya mabadiliko ya maisha.

Kuishi kwa unafuu ni jambo moja zuri ila kwa upande mwingine si jambo lenye faida sana ukitazama in the long run.

Hebu watazame kama wahindi wenzetu mathalani..... Wanaishi maeneo gani?! Umeaona bunju, umewaona tegeta umewaona Chanika.....?!

Wanaishi upanga, kwenye flats na apartment na nyumba za national housing. Na ndio wanampunga kutishinda sisi tunaojiita wajanja......

Siri moja kuhusu maisha, ukitaka unafuu wa chini ya tabaka lako (comfort zone) basi jiandae kushuka daraja.

Mfano, umeona kulipa 350,000 ni mzigo na ingawa umeweza kumudu basi wewe unaanza kuishi early retirement wakati haupo katika huo umri wa kuretire. Hayo ni mawazo anatakiwa kuwa nayo mzee wa miaka 85+ ambaye anahitaji utulivu wa kuishi miaka iliyosalia kwa kupumzika na kucheza na wajukuu.....

Kijana wa miaka 20 hadi 70+ unasemaje kuwa unakwenda kujenga nje ya mji kutafuta unafuu wa maisha...... C'amon?!

Nikwambie tu, maisha yanataka katika kila stage unayo graduate au kufika basi usichukulie ndio hitimisho, bali hiyo ni stepping stone ya the following phase ya maisha.... Tena ushukuru umefika hapo kuna mtu akiona wewe unalipa laki tatu na nusu ya kodi anakuona mharibifu sana wa pesa. Sababu yeye ameshajilimit kuwa hatopanga nyumba zaidi ya kodi ya 30,000 kwa mwezi. Huyu mtu unamuonaje hivi?!

Ipo hivi, pesa ndio maana inaitwa "Currency" kutokana na neno CURRENT ambalo humaanisha mkondo. Ukitaka pesa sharti maisha yako yawe na value pesa itakufuata. Kama ninachosema ni uongo tazama uhalisia hivi ukiwa na maisha ya kubana bajeti kesho ukafa ndugu wakagombania muounga wako unakuwa umeacomplish nini kwa mfano?!

Unajua kuna mtu unamfuata unamwambia brother naomba unazime 500,000 chap hapo jibu lake ni okay nikutumie kwenye namba gani?! Unajisikiaje kuongea na mtu wa hivi?!
Mwingine hata elfu 20 tu ataingia kwenye wallet atatoa chap atakupatia.

Mimi as a business person nitavutiwa sana kuongea na mtu anaendesha gari ya wastani 2000, anaishi nyumba ya kupanga hata kama ni 200,000 au 350,000, **** the price what matters upo comfortable na unaishi kwa nafasi nzuri. Ana budget nzuri na haogopi kufikiria chanzo kipya cha mapato kila baada ya miezi kadhaa. Hii itanipa picha kuwa huyu mtu ana discipline ya pesa na anajiamini na yupo positive financially.

Vijana wengi wa bongo atatoka kodi ya chumba kimoja, ataenda chumba na sebule, akishatiana mimba na mwenzake wakapata tutoto tuwili watakodi kanyumba ka vyumba vitatu then wataanza ujenzi wa nyumba nje ya mji then wakishamaliza wanahamia story imeisha wanajiona ni wazee wameshamaliza maisha, watu wa namna hii huwa hata kuongea nao naona kero maana wanajiona safari ya maisha wameifika na wanasubiria wajukuu na uzee ufike wadedi picha liishe.

Hivi mnaona wenzetu rangi nyeupe wanavyofanya?! Wakati sisi goal yetu na accomplishment kubwa na ya mwisho ya average Tanzanian youth ni kuoa, kupata watoto, kujenga nyumba yenye fremu mbele ya fensi huko nje ya mji, kununua gari, kuwa na shamba mlandizi au chanika la kulima viazi gunia mbili, na kuokota maembe kiroba kimoja kisha kuendelea kuishi tukisubiria uzee utuvae huku tukisomesha watoto kwa hela za pension na kujiuguza magonjwa kama kisukari na pressure sababu ya stress za retirement era,..... Tazama wenzetu race nyingine wanafanyaje huo umri?!

Average white race person goal yake kubwa ni kuishi standard ya maisha itakayompa privilege ya kubakia kuwa superior race no matter what it costs. Amini nakwambia hakuna kitu kama gharama katika haya maisha ila kuna choice za gharama gani unataka maisha yako yawe evaluated.

Unataka kuishi maisha ya free from everything?! Yaani mtu anakwambia anajenga ili kukwepa kulipa bili za makazi kama kodi?! Seriously?! Nani alikwambia kuishi katikati ya mji huku unalipa kodi ni sumu ya kufeli maisha....?!

Its okay to own a piece of land ila huwa nashangaa mtu anakimbiaje maisha ya kupambana for the luxury of the comfort zone?! Comfort zone ndipo watu hujitengenezea hell ya uzeeni. Hivi hawa wazee wote wanaodedi kwa pressure, kisukari, msongo wa mawazo, wengi si huwa wana majumba yao ya kuishi, shida huwa ni nini unadhani?!

Ni financial freedom hakuna. Mtanzania average anapoanza kupata access ya kutoka katoka tabaka la chini kuingia la kati anaanza upuuzi huu wa kuishi maisha ya kizee na hatimae kurudi nyuma badala ya kukaza zaidi na kubadili mbinu ilikuwa 100% tabaka la kati yaani tabaka six figures income every month na kurudi chini kwenye tabaka la three to two figures a month.

Walipo wahindi ndio na sisi tunatakiwa kuwapo. Wahindi sasa hivi ni sehemu ya kabila la kitanzania maana wapo waliozaliwa hapa. Why tusiwaige njia zao na sisi tusione shida kwenda kupanga pale upanga kwenye apartments tunaishi maisha ya popo huko vingunguti.

Ukienda nje ya mji barabara mbovu, gari zinaumia, mafuta uhitaji utaongezeka , gharama za vipuli vya gari na services vitakuhusu, plus unaenda kukaa nje ya mji utatakiwa kurejea home mapema sababu ya umbali, pia ni ngumu kuwa karibu na wazee wa connection kupeana connection.....

Nadhani hili hebu tulitazamie upya..... Kila kitu kitawezekana ndani ya muda na sisi tukiwa watu wa kujiongeza na changamoto zetu......
Wahindi zile nyumba wanazoishi zilikua ni za kwao maana zilijengwa na babu zao ni vile tu Nyerere alibinafsisha nyumba zao,viwanda vyao na mashule yao kwa serikali.

Baada ya ubinafsishaji wahindi hawapendelei sana ku invest vitu kama nyumba maana walishaonjeshwa shubiri hapa Tz na Uganda,investment zao nyingi ziko in liquid(cash, money market funds, shares etc).

Pia wahindi hawajioni kama ni watanzania wengi wanajiona ni wahindi na wacanada zaidi na ndio huko wanakojenga majumba yao.Sasa hata wewe sidhani kama ungeona fahari kujenga sehemu unakooana sio kwenu.

So kufananisha wahindi na wabongo ni irrelevant.
 
Back
Top Bottom