Utaratibu wa mtu kulipa michango mbalimbali kwa Elimu ya sekondari ni nchi nzima au?

Amanikwenu

Senior Member
Dec 1, 2009
187
0
Wakuu,

Jana nilitembelewa na jirani yangu mmoja na akanieleza kuwa watoto wake wawili wamefaulu mtihani wa darasa la saba na wamechaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya Zinga iliyoko wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani. Hii ni moja ya shule zetu za kata.

Kitu kilichonistua na kunishangaza katika maelezo yake ni kuwa, pamoja na mambo mengine kama hela ya mlinzi; uji; kuni; ada; karatasi, kila Mwanafunzi anatakiwa AENDE NA KITI NA MEZA YAKE SIKU YA KUFUNGUA SHULE TAREHE 18/01/2010.

Je huu ni utaratibu wa nchi zima kwa shule zetu za kata au ni kwa shule hii ya ZINGA pekee?
 
Hali ndio hiyo kwa Tanzania nzima tena hata kwenye Private Schools zenye majina. Nilidhani ni wakati mzuri sasa serikali ikaunda chombo kinachofanana na EWURA/SUMATRA/TCRA kwenye elimu pia. Vinginevyo iipe meno TEA ifanye kazi hiyo.

Kuna ndugu yangu mmoja kampeleka mwanae BAOBAB. Kwenye Invoice yao ya karo upo mchango wa laki moja ya jengo! Yaani mzazi achangie kumjengea mmiliki binafsi.

Nikamshauri akishachangia aombe shares ili naye awe na umiliki wa kiwango fulani. Karo ya BAOBAB mbali na mchango huo ni milioni mbili na nusu (2,500.000/=) kwa mwaka wa kwanza.
 
Ufisadi umeshamiri kila sekta, lakini sikutegemea sekta binafsi! Wakati umefika wa watu kufichua maovu haya, kama unaona ni kitu cha ajabu na usipokikemea au kukisema watu wakasikia, basi hali hii itaendelea milele! Shule binafsi nyingi wanafanya mambo ya ajabu, lakini wazazi na walezi hawasemi, sijui ni kwanini. Niliwahi kusikia mzazi mmoja anasema alihudhuria mkutano wa wazazi katika shule moja, na alishangaa kuona wazazi wanashauri ada ipandishwe! Akaona aubu kupinga.
 
Hali ndio hiyo kwa Tanzania nzima tena hata kwenye Private Schools zenye majina. Nilidhani ni wakati mzuri sasa serikali ikaunda chombo kinachofanana na EWURA/SUMATRA/TCRA kwenye elimu pia. Vinginevyo iipe meno TEA ifanye kazi hiyo.
Kuna ndugu yangu mmoja kampeleka mwanae BAOBAB. Kwenye Invoice yao ya karo upo mchango wa laki moja ya jengo! Yaani mzazi achangie kumjengea mmiliki binafsi.
Nikamshauri akishachangia aombe shares ili naye awe na umiliki wa kiwango fulani. Karo ya BAOBAB mbali na mchango huo ni milioni mbili na nusu (2,500.000/=) kwa mwaka wa kwanza.

Mzee kwenye bold hapo umeongea point hata mimi niliwaza the same, ila swali ni moja tu unawajua wenye hizo shule???
 
Binafsi utaratibu wa kuchangishana katika fixed assets unabidi uangaliwe upya. Maana kama mtu unasaidia katika cost halafu huwezi realise profit huo ni WIZI. Siwezi kuchangia huduma ninayopata halafu tena nachangia na running cost ya service provider.

Michango ya kanisani, mashuleni, mtaani, yote ni wizi mtupu!

Michango ya makanisani mbali na sadaka ninamaanisha michango ya kusaidia ujenzi wa shule, mabenchi nk.

Kama mtu amejiita local investor halafu anatumia pesa za watu, huo ni WIZI! MWIZI MKUBWA!
 
....the show continues!!!!
Ma-ghembe hebu baelezee bananji hii mradi ya mendeleo kwa mishule yetu ni ya nini tena vile? SEDP na PEDP,

haya, kama huna jibu nenda kachume fimbo uje nayo hapa sasa hivi!!
 
Mzee kwenye bold hapo umeongea point hata mimi niliwaza the same, ila swali ni moja tu unawajua wenye hizo shule???
Tukitaka kuwafahamu ni rahisi tu. Yupo anayewapa usajili pale wizarani. Lililo wazi ni kwamba WANASIASA wetu wengi sana wamewekeza kwenye miradi hii ya shule. Ndio maana wanafanya wanavyotaka. Wengine kwenye uwekezaji huu wa mashule ni watumishi waandamizi serikalini. Kazi ipo. Hili hata kulipeleka BUNGENI ni kazi bure. Wabunge wengi wetu wanamililki au ni wawekezaji humo. Tufanyeje? Elimu bora inatolewa huko sasa hivi. Primary na Secondary za serikali zinahujumiwa kwelikweli. Walimu wazuri waliosoma kwa gharama zetu wanakimbilia huko.
 
Hali ndio hiyo kwa Tanzania nzima tena hata kwenye Private Schools zenye majina. Nilidhani ni wakati mzuri sasa serikali ikaunda chombo kinachofanana na EWURA/SUMATRA/TCRA kwenye elimu pia. Vinginevyo iipe meno TEA ifanye kazi hiyo.---
.
WildCard,

Nakuunga sana mkono kwenye hili la kuwa na Tanzania Education Regulatory Authority (TERA). Ila bado tatizo langu linabaki palepale. Hivi kweli tumeshindwa kununua madawati ya kutosha kwa ajili ya shule zetu za sekondari za kata wakati bajeti ya sekta ya elimu kwa mwaka huu wa fedha ni zaidi ya shilingi bilioni 1,743. Kama tumeshindwa madawati je vitabu tutaweza? Aliye na breakdown ya bajeti ya elimu naomba atusaidie katika hili.

Pia ni muhimu sana Waziri muhusika akatoa kauli ya serikali kuhusu wanafunzi wa shule zetu za kata kutakiwa kwenda na kiti na meza shuleni wanaopoanza kidato cha kwanza.
 
Na bado kuna siku titaambiwa inabidi tuingie kwa wallet kuwalipa walimu!

YOU CANT TAX UNTAXABLE SOCIETY
 
Tukitaka kuwafahamu ni rahisi tu. Yupo anayewapa usajili pale wizarani. Lililo wazi ni kwamba WANASIASA wetu wengi sana wamewekeza kwenye miradi hii ya shule. Ndio maana wanafanya wanavyotaka. Wengine kwenye uwekezaji huu wa mashule ni watumishi waandamizi serikalini. Kazi ipo. Hili hata kulipeleka BUNGENI ni kazi bure. Wabunge wengi wetu wanamililki au ni wawekezaji humo. Tufanyeje? Elimu bora inatolewa huko sasa hivi. Primary na Secondary za serikali zinahujumiwa kwelikweli. Walimu wazuri waliosoma kwa gharama zetu wanakimbilia huko.

Yapo malalamiko mengi ya jinsi usajili wa kulipua unavyofanyika pale wizarani.Kwamfano, kule tanga kuna chuo fulani cha ualimu kisicho na kiwango kimelalamikiwa sana na wananchi lakini mkubwa wa wizara kwakuwa ni kabila moja na mwenye chuo hakijafungwa na mambo yanaendelee, ndo elimu ya bongo hiyo!
 
Wakuu,

Jana nilitembelewa na jirani yangu mmoja na akanieleza kuwa watoto wake wawili wamefaulu mtihani wa darasa la saba na wamechaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya Zinga iliyoko wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani. Hii ni moja ya shule zetu za kata.
Kitu kilichonistua na kunishangaza katika maelezo yake ni kuwa, pamoja na mambo mengine kama hela ya mlinzi; uji; kuni; ada; karatasi, kila Mwanafunzi anatakiwa AENDE NA KITI NA MEZA YAKE SIKU YA KUFUNGUA SHULE TAREHE 18/01/2010.
Je huu ni utaratibu wa nchi zima kwa shule zetu za kata au ni kwa shule hii ya ZINGA pekee?


Hii ndiyo sera safi ya CCM kwamba kila kata lazima kuwe na sekondary ifikapo 2010 na haya ndiyo matunda yake.

Shule za kata za style kama Zinga zipo nyingi sana.
 
Hali ndio hiyo kwa Tanzania nzima tena hata kwenye Private Schools zenye majina. Nilidhani ni wakati mzuri sasa serikali ikaunda chombo kinachofanana na EWURA/SUMATRA/TCRA kwenye elimu pia. Vinginevyo iipe meno TEA ifanye kazi hiyo.

Mbona hicho chomo kipo wanaitwa Wakaguzi wa Elimu hata hapo wizarani kitengo hicho kipo na kina bajeti yake tatizo linabaki palepale mambo yanaendeshwa kisiasa zaidi.

Hizi shule za kata zinaruhusiwa kuanza siku waziri anapotembelea kuweka jiwe la msingi bila kujua itaisha lini kujengwa walimu watapatikana wapi madawati na kadhalika. Shule nyingi hasa hizi za kata zilianzishwa haraka haraka ili kuwafurahisha wadhamini Tanzania ionekane imepiga hatua katika elimu matokeo yake ndo kuleta walimu wa Voda fasta umemaliza form two yako unapelekwa kozi ya ualimu mwezi mmoja next month ni mwl. haijalishi kama ulichelewa kwenda chuo kwa wiki mbili twende tu nasikia kuna wengine walikuwa wanawakuta wenzao wiki ya mwisho wanaagwa na kujiunga nao.

Hii ndio elimu ya Tz iko kisiasa zaidi matokeo yake shule inakuwa na walimu wawili tu tena hawajui hata ethics za ualimu.
 
Hii ndio serikali ya tanzania bwana.Mambo yote mtelezo
Siyo serikali bali sema hii ndio hulka ya watanzania. Hizi shule binafsi walianza vizuri tena serikali ikawapa nafuu ya kodi lakini SUSTAINABILITY inawashinda.

Hata hizo 'Academy' zenye majina makubwa kumbe ilikuwa nguvu ya soda, hawalipi wafanyakazi wao vizuri kama ambavyo ungetegemea kwenye private sector; tangia ajira za walimu zilipopatikana serikalini, nyingi ya shule hizi siku hizi ni dhofulhali!
 
LOL!....ar u for real? kiti na meza tena, litakuwa darasa au warehouse kila mtu akenda na furniture zake?
 
in such kind of situation other peoples are building houses of 1.2 billion and their kids are in up countries. is there any equality.
 
in such kind of situation other peoples are building houses of 1.2 billion and their kids are in up countries. is there any equality.
Big "NO" Mwanangwa. Wanasema hata vidole hutofautiana urefu japo vyote ni vidole. Katika mazingira kama haya kuna umuhimu wa mabadiliko.
 
Shule za serikali kweli huu utaratibu uangaliwe upya.

Kwa shule binafsi sioni tatizo la kupanga bei yoyote wanayotaka kama soko lipo, ndo biashara inavyoenda. Pale IST ni kama $13,000 na watu bado wanalipa.
 
Mzee kwenye bold hapo umeongea point hata mimi niliwaza the same, ila swali ni moja tu unawajua wenye hizo shule???

Ni kweli tunahitaji regulator kwenye hii biashara ya shule. Wamiliki wanadai hela kwa nguvu tena sio hiari .Eti mtoto atarudishwa shule kama hajalipa mchango wa majengo. Hata wamiliki wangekuwa marais wote wastaaf na J.K juu, hawana haki juu ya haya.

Tunahitaji mtu kama Dokta Magufuli. Period
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom